ATCL jirekebisheni vinginevyo mtapoteza wateja

ATCL jirekebisheni vinginevyo mtapoteza wateja

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Tunayo Shirika letu la Ndege la ATCL na sasa hivi kwa safari za humu nchini haina ushindani kabisa kwa lugha ya kimombo ina (monopoly). (1) Kwanza nianze na gharama zao mfano Mwanza mpaka Dar.

Gharama zao ni kubwa sana na kama ndege zilinunuliwa kwa ajili ya watanzania kwa nini sasa manufaa ya hizi ndege ni kwa matajiri tu?. (2) Huduma kwenye ndege zao haziridhishi kabisa.

Niwape mfano hai. Tarehe 17/9/2020 nilisafiri kwa ndege ya ATCL na muda wa kufika uwanjani nilielezwa ni saa 5.25 asubuhi. Nilifika muda muafaka na tukapaa saa 7.25 juu ya alama.

Kwa kawaida muda kama huo msafiri anatakiwa apewe chakula akiwa safarini hata angalau kinywaji lakini cha kushangaza tulipewa maji ya chupa ya ml.300 ikizingatiwa tulifika Dar es Salaam saa 9.45. Muda huu wote hatukupewa chochote.

Leo tarehe 23.9.2020 pia nimesafiri na ATCL na muda wa kufika kiwanjani ulikuwa saa 6.00 mchana na tumeondoka Dar kuja Mwanza saa 8.00 kamili juu ya alama. Tulitakiwa tuwe tumepatiwa chakula kama wasafiri lakini tuliambulia maji ya mil.300 aina ya Afya.

Leo nimeuliza hivi kwa nini hawatoi chakula kwa wasafiri, jibu nililopata eti ni kwa sababu ya corona. Nikawauliza hivi Ethiopian, Kenya Airways, Swiss Air hawatoi chakula kwa wasafiri kwa sababu ya corona?.

Wakanyamaza kimya. Kitendo wananchofanya ATCL kwa wasafiri ni kitendo cha kinyama na inabidi wabadilike.
 
Wameshajijua kuwa wapo peke yao kwenye local flights ndiyo maana wameanza kiburi. Flights za Nje ya nchi hata hapo Comoros tu hawawezi fanya huo ujinga.
 
Serikalini vs Vya watu binafsi.

Mimi nachagua vya watu binafsi kwasababu ni rahisi kuwajibika.
 
HV ukitoka ubungo Hadi chalinze unatumia masaa mangali. Hapo Kati huwa umepewa chakula chochote? Tho ATCL muangalie Hiki wadanganyishie ata na biscuit tu na kijoti kwani bei gani.
 
Hakuna biashara inayoendeshwa na serikali 100% ikafanikiwa. Mataifa yaliyoendelea yanajua hili ndio maana British Airways, Lufthansa, KLM, Emirates, American Airways na mengine yanamilikiwa kwa kiasi kikubwa na watu binafsi. ATCL ni tembo mweupe mwenye hasara kwa nchi yetu.
 
Kwahiyo mkuu unapoteza nauli ya kumwaga kisa tu upewe chakula kwenye ndege?
 
Ulienda kula kwenye ndege au kusafr tu nyie ndo uwa mnalilia chakula msibani
 
Nashangaa wanao mponda mwandishi aache ulafi..mna jua nauli ya izo ndege nyie, famba kabsa nyie
 
Mashirika kama fastjet yaliweka bayana kwamba ticket yako inakupa siti kwenye ndege na x amount ya kg za mzigo.. Ukitaka chakula unalipia separate na hata mzigo ukizidi unalipia peke yake pia.. Ili kuweza kufikia malengo yao, walifanya bei za ticket ziwe chini wakijua wanajazia kwenye mizigo.

Mashirika ambayo yanacharge bei za kawaida na kwenda juu za ticket za ndege maana yake kwenye mizigo wanaruhusu required weight na wanatoa chakula.. Hivyo wateja wao huwa wanajua bei zipo juu ila wanaruhusiwa uzito mkubwa kidogo na chakula (plus kinywaji) wanapewa kizuri.

Kwahiyo muandishi hakuandika akimaanisha amepanda ndege akale chakula.. Ticket ya hiyo ndege ukute ni Tshs 250,000 au zaidi kwa safari moja.. Hapo angepanda mabasi trip atakazo na kula vizuri tena best luxury bus.. Ila anachosema ni kwa bei aliyolipia, kuna huduma ANATAKIWA (sio favour au bonus) kupata.

Kama haupati hizo huduma ni dalili shirika linayumba kiuwezo au kihuduma.. Walitakiwa waweke tangazo kwa nini hawatoi chakula.. Vilevile, wangeweza kuwapatia wasafiri chakula kwa kutumia njia nyingine ambazo ni salama.

Tunapopanda mabasi tusihesabie ni ndege na tunapopanda ndege tusidharau wapanda mabasi.. Hivyo likiwekwa swali (au hoja) ubaoni, ijibiwe hoja na sio kuandika mengine ambayo hayahusiki..
 
Mkuu hiyo Atcl wasoipo angalia itaenda na JPM refreshment, time keeping hospitality ni sehemu ya customer care kwenye route yoyote kwenye ndege, ATCL katika customer care ni 0% wanalindwa tu na kodi ya wananchi,

ili ushindani ukilatikana wana kufa mapema tu, hao wanao kuponda wamazoea maisha magumu ya kula milo miwili kwa siku hawajui maana ya refreshment meals ndo maana unakuta mtu wa miaka 50 anaonekana kama babu wa miaka 70 refreshment.
 
Mkuu mimi binafsi sijawaho panda ndege...sasa hapa sijaelewa ulitaka ukiwa huko angani utengewe sinia la wali na kibakuli cha mboga kati kati au msosi upi ulikuwa unataka wewe??
 
Back
Top Bottom