ATCL yaanzisha kibubu kwa abiria wanaotaka kulipia nauli kidogo kidogo

ATCL yaanzisha kibubu kwa abiria wanaotaka kulipia nauli kidogo kidogo

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165

ATCL yaanzisha kibubu kwa abiria wanaotaka kulipia nauli kidogo kidogo​



THURSDAY SEPTEMBER 09 2021​

ATCL pc

Summary

  • Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) imeanzisha mpango wa "kibubu" utakaowawezesha wananchi kulipia kidogo kidogo mpaka atakapo kamilisha malipo ya tiketi yake ya ndege.


By Waandishi Wetu
More by this Author

Dar es Salaam. Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) imeanzisha mpango wa "kibubu" utakaowawezesha wananchi kulipia kidogo kidogo mpaka atakapo kamilisha malipo ya tiketi yake ya ndege.


Katika mpango huo, mwananchi atatakiwa kuweka Sh50,000 kwa mara ya kwanza na kiasi kinachobakia atatakiwa kulipa kidogo kidogo kwa kiwango anachokimudu mpaka safari yake itakapofika.


Akizungumza na vyombo vya habari leo Septemba 9 jijini Dar es Salaam, mkuu wa kitengo cha mawasiliano - ATCL, Josephat Kagirwa amesema mpango huo utawawezesha wananchi kupangilia safari zao kwa kulipia tiketi zao kidogo kidogo.

Soma hapa: Kamati ya Bunge yang’aka deni, uendeshaji ATCL

"Tumeweka mpango huu ili kuwasaidia wananchi kuweka fedha kidogo kidogo ili kulipia tiketi ya ndege ndani ya muda ambao amepanga kusafiri," amesema Kagirwa.


Kwa upande wake, meneja wa mtandao wa safari na usimamizi wa mapato katika kampuni hiyo, Edward Nkwabi amesema kwa kuanzia wananchi watafanya malipo ya awali ya tiketi zao (booking) katika ofisi za ATCL lakini baadae wataweza kulipia kwa njia ya benki.

Amesema masharti yanayotumika katika mpango huo ni kama yale yale yanayotumika kwenye tiketi za kawaida. Amesema mteja akiahirisha safari yake, watazingatia vigezo na masharti kabla ya kumpangia safari nyingine.


"Shirika letu lina safari za ndege kila kona ya nchi hii na pia tunakwenda baadhi ya nchi kama vile Burundi. Kwa hiyo, mpango huu utatumika pia katika safari za kimataifa," amesema Nkwabi.

Soma hapa: Bosi wa zamani ATCL kulipa Sh8m au kwenda jela miaka minne

Naye Ofisa Masoko wa ATCL, Grace Magubo amesema kampuni hiyo itatoa zawadi kwa wateja ambao watahamasisha watu zaidi ya watano kutumia mpango huo wa kibubu na zawadi yao ni kujipatia tiketi ya ndege kwa nusu bei ya mahali anakotaka kwenda.

Imeandikwa na Peter Elias na William Bukoli.
 
Huu ndo ujinga wa atcl.
Yaani hakuna watu wabunifu.
Hii kibubu ni copy paste ya ile huduma ya "Dunduliza fare " ya precision air waliyozindua two months ago.

Yaani wamekopi kila kitu hata hiyo kiasi cha elfu 50 kutangulizwa.

Atcl wana copy paste hadi routes .

Precision akianzisha ruti flani na wao siku inayofata wanaianzisha.

Precision wakianzisha dunduliza fares" wao wabaibadilisha wanaiita "kibubu"...alafu wakati maelezo ya kibubu ni kuweka kidogo kidogo.

Kwa kukosa kwenu maarifa ,kila siku mtapata hasara tu.
 
Huu ndo ujinga wa atcl.
Yaani hakuna watu wabunifu.
Hii kibubu ni copy paste ya ile huduma ya "Dunduliza fare " ya precision air waliyozindua two months ago.

Yaani wamekopi kila kitu hata hiyo kiasi cha elfu 50 kutangulizwa.

Atcl wana copy paste hadi routes .

Precision akianzisha ruti flani na wao siku inayofata wanaianzisha.

Precision wakianzisha dunduliza fares" wao wabaibadilisha wanaiita "kibubu"...alafu wakati maelezo ya kibubu ni kuweka kidogo kidogo.

Kwa kukosa kwenu maarifa ,kila siku mtapata hasara tu.
Kama ndo hivyo Basi wamekosa ubunifu! Hivi SI watualike wabunifu tukawape maujuzi yetu ya ubunifu!!! Sijui ni ubahili wakutulipa wabunifu au Nini???
 
Serikali ilisema kuwa hilo shirika litakufa muda wowote,halafu mnataka life na hela yangu? Wode saa!
 
Bila shaka hii itaisadia shirika kutokujiendesha kwa hasara.kila la kheri
 
Atcl anzishen ruti ya kubeba wanyama kutoka mikoan kuja dar!!! Nguruwe hatafaid sana
 
Wazo zuri ila ghafla bin vuu wanaweza kuvunja kibubu na wakampa mama. Mi ningedunduliza 2030 nina mpango wa kwenda US
Nalog off
 
Back
Top Bottom