Athari za Kutohimiza Kiingereza

Nini kinachokuzuia usijifunze hio lugha wakati ndio lugha kuu ya kufundishia kulinganisha na kiswahili.
Yani mtu huko shule alikuwa analeta mzaha na hio lugha hatimae amemaliza bila kui master anatafuta wa kumlaumu.
Umefundishwa kingereza miaka 7+4+2+2/3+ kwa masters ongeza 2 na Phd ongeza3 .
Umeondoka bilabila halafu unailamu serikali.
Suala ka elimu asilimia kubwa ni juhudi binafsi mwalimu ni 20% tu.
 
Kweli kabisa sasa hivi kuwekeza kwenye lugha kuu ni muhimu
Wasiasa wanatupoteza sana ilihali watoto wao wanawapeleka international school
 
unaonaje kwenye katiba yetu tuweke Kingereza iwe Lugha rasmi ya Taifa?[emoji1787][emoji1787]
 
Daah umetumia nishati kubwa sana kunielewesha. Ungeweza kuihifadhi hii nishati kwa matumizi mengine ya muhimu siku za baadae
 
Zaidi ya yote ni kukosa 'personal confedance'..... wtzania tunao kutana nje ya nchi hawajamini ipesavyo kwasabb are not fluent in English language.
 
Sikubaliani nawe kwamba tuna IQ ndogo. Yaani IQ zetu zimeshuka? Maana miaka ya huko nyuma tulikuwa tunakimudu Kiingereza vizuri. Na hata sasa wanaosoma nje wanakimudu Kiingereza. Kwani IQ zao ni kubwa zaidi?
Lakini pamoja na kutojua kiingereza je kiswahili chenyewe tuna kimudu vizir au na ni ubabaishaji pia mtupu.
 

Kwani Prof. Ndalichako au rire jiwe renyewe ririkuwa rinasemaje kuhusu hili la lugha za mabeberu?
 
Kweli we binti kiziwi
 
Shile za academy zina ajili walimu hao hao wa serikali kwa asilimia kubwa. Hivyo hoja ya kuwa walimu wa academy wanajua zaidi kingereza sio kweli bali walimu wa academy wanatumia zidi kingereza zaidi ya kayumba.
Jambo la pili huko huko kayumba school wapi wanafunzi wanaweza kuongea kingereza vizuri je wao wana nini mpaka mwingine ushindwe kabisa.
Jambo la tatu kuna tuition centre nyingi sana ambapo unayonafasi ya kumtafuta mwalimu mahili akufundishe.
Shule ni complex term hivyo usiichukuli kirashisi na kutoa majawabu marahisi tu.
Katika karne ya 21 mwaka 2021 mtu kuendelea kuilaumu serikali ni ni kupoteza muda na kutojitambua.
Kuna infrastructure za kutosha hata kusoma Phd bila kufika darasani.
Tumieni internet, fundisheni watoto kutumia internet, download education apps kwa ajili ya watoto wenu na nyie wenyewe.
Tumia you tube kuna competent teacher ambao shuleni kwako hawapo au ngumu kuwapata.
Traditional methods of learning are out of date tumieni njia janja, elimu janja kws vifaa janja
Mnataka serikali isisitize nini ambacho haijafanya, iwalazimishe kutumia mifumo?
 
Hivi JF wakisema kitumike kiingereza tu, mijadala na maarifa yaliyomo humu tungepata? Kiingereza ni moja ya mambo yanayofanya tusiendelee
 


Utumwa wa fikra ni mzigo mkubwa sana kama umasikini na ukosefu wa ajira msingi wake uwe kutojua kingereza basi bara Arabu wengekua masikini wa kutupwa heri hata tanzania tunajitahidi kuongea kingererza kuliko wao lakini unawasikia jinsi wanavyo fanya mambo mazito na kiarabu chao huko kwa waongea kingererza. Na nimwenyeafaya mbaya tu ya akili atampima mwenye PhD kwa kuongea kingereza badala ya kumpima uwezo wake wa kufukiri uwezo wake wa utendaji kazi na uwezo wake wa kuleta mabiliko
 
Mimi naona kuna kitu hakijakaa vizuri kuhusu lugha ya Kingereza kwa Wa-Tz. Zamani early 80s wahitimu wa kidato cha NNE walikuwa wanaongea kingereza fluent bila shida yoyote akifanikiwa akasogea hadi A-level ndo kabisa humkaribii.Baadae mifumo yetu ya elimu iliyumba especial miaka ya elfu mbili mwanzoni,Shida kibwa niliyoiona ni kasi ya kuchanganya Siasa na mambo nyeti yanayohitaji utaalam. Jinsi unavyoona Leo wanasiasa wanavyoshawishi watu kukataa chanjo ambayo hawana utaalam nayo ,vivyo hivyo siasa kwenye sekta nyingine ni hivyo tu.MWISHO TUNA SAFARI NDEFU.
 

Sera ya kukuza kiswahili na kukipa nafasi ya kwanza nadio sera aliokua nayo Kambarage Nyerere na hao unaosema walikua wanaongea kingereza ilikua ni mazao ya shule za Semenary na Muslim schools Nyerere alipozitaifisha Kiswahili lugha yetu adhimu ikachukua nafasi yake
 
Hivi kama IQ yako inaruhusu kuna shida kujifunza lugha yoyote ya kigeni Aidha ya kwako?.Mimi sioni kuwa ukijifunza kingereza unatelekeza kiswahili no ,no. Kuna kaukweli kuwa mifumo yetu ya ufundishaji na namna nchi inavyo handle mambo yake vimeathiri ukuaji wa kingereza nchini.Usome kingereza kama medium of instruction form one to PHD,Then lugha ikushinde.
Muhimu tusisitize Kiswahili na tucheze kwa nafasi yake tusisitize Kiswahili kwa vile hatujui Kingereza.
 
Shida yangu ni hii
Mbona kingereza nchini kinafundishwa kila siku mbona hatukielewi...Tena udhaifu unajionyesha kabisa hata mtaani,Unakuta MTU kang'ang'ania kuandika bango kwa kingereza humo kakosea spelling kiasi cha kujichoresha. Kama we kinyozi mtaani si uandike bango kwa kiswahili after all unanyoa waswahili INA bore sana.Si lazima uandike BARBER Ya nini !
 

Tatizo ni uongozi mbovu. Mzee wangu aliishia darasa la sita lakini alikuwa anaandika na kuongea kiingereza na watu wa mataifa mengine bila taabu.

Baada ya kuharibu elimu kiasi kikubwa wamefanya kuwa suala la kisiasa. Eti Kiswahili pekee ni kipimo cha uzalendo. Na Kiswahili chenyewe hakifundishwi vizuri. Kimeharibika sana. Matumizi ya l, r, tabu. “Hana” inaandikwa “ana”! Halafu wamefundishwa dawa ni “kujiamini”; yaani kuwa wabishi kufa wakikosolewa. Kujitetea na “uzalendo” bila kujali kuwa wanaangamizwa kwa kukosa fursa.

Kujua lugha nyingi za kimataifa ni faida. Kuna watu toka DR Congo wana nyadhfa katika serikali za Afrika ya Kusini, US, Uingereza. Walisoma shule kwa kifaransa lakini wana kiingereza cha uhakika na Kiswahili pia.

Tanzania hatuna teknolojia wala utajiri wa machapisho ya taaluma kwa Kiswahili. Hatulingani na wachina, wafaransa, wajerumani, warusi. Na hao wengi wanajua lugha za kimataifa zaidi ya moja. Wengi kiingereza wanacho ingawa sio lugha yao ya kujifunzia. Wanakitumia inapobidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…