Athari za mikopo ya Serikali kwa umma

Athari za mikopo ya Serikali kwa umma

chamilo nicolous

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2016
Posts
2,097
Reaction score
1,457
Serikali inapoendelea kukopa, jamii inaathirika vipi? Je, waziri wa fedha yuko sawa sawa kujitokeza adharani, na kukiri kuwa wataendelea kukopa na hakuna atakaeathirika?

Mchango wangu kuhusu hii mada ya mikopo ya Serikali katika sekta binafsi. Sekta inayo wahusu Watu binafsi na mashirika binafsi!

Kanuni za Kiuchumi zinatanabaisha Uchumi wa nchi siku zote serikali ndio mteja mkubwa. Ukisoma Dira na Mpango wa III wa maendeleo wa Taifa ukisoma na Sera zote za kisekta zinaitaja Sekta Binafsi kuwa mhimili wa Uchumi wa nchi.

Sekta ya Fedha kama jamii zingine za Biashara na Uwekezaji siku zote hupendelea kufanya Kazi na mteja wa uhakika mteja anayeaminika na huyu ni pamoja na Serikali.

Moja ya ATHARI ambazo ni za lazima pale Serikali inapojiendesha kwa mikopo au serikali anapokuwa mkopaji mkubwa Kwenye Sekta ya Fedha matokeo ni kwamba Benk nyingi zitapunguza mikopo Kwa Wajasiriamali, Wafanyabiashara na Wawekezaji Binafsi Ili kuikopesha Serikali.

Matokeo yake Sekta Binafsi haitapata Fedha za kutosha kuendesha shughuli zake na hivyo:

1. Uwekezaji wa ndani utapungua.

2. Ubunifu utapungua na Sehemu kubwa ya Uchumi wa nchi utajielekeza kwenye trading tukitegemea sana bidhaa Kutoka nje ya nchi. Viwanda vya ndani vitashindwa kujiendesha. Ndo sababu kukopa kopa huku kwa Serikali ya Samia, husikii tena, nchi ya viwanda, oooh uchumi wa kati!

3. Tatizo la Ajira litaongezeka, viwanda vitakufa, umasikini utaongezeka na Pesa itakosa thamani.

Nashauri nafasi ya Gavana wa Fedha itazamwe upya na Wizara ya Fedha kama Wizara mama inayosimamia Uchumi wa nchi Nafasi ya Waziri itazamwe upya. Katika hili Waziri wa fedha umefeli.
 
Wasomi tusiwaachie wanasiasa kuongea, wasomi tulikombowe hili taifa.
Hatuwezi kuwaachia wazee makada wa chama kutupoteza hilihali maarifa na uelewa wa mambo tunao, eeti tunaogopa
 
Mikopo ina condition moja kubwa..DISCIPLINE kwenye matumizi ya ulichokopa na kurudisha, awamu ya 3 ya Mzee Mkapa, nchi yetu ilikuwa kwenye nchi za HIPC na haikuwa inakopesheka tena..tulifikaje huko na rasilimali zote hizi ardhi, madini, maji, watu nk zilikuwepo.

Pamoja na sababu zingine, moja ni mipango mibaya ya matumizi ya pesa za mikopo, bado tunarudia yale yale..hivi kuna haraka ya kujenga SGR kwenda Kigoma kutoka Tabora km 506 au hata TBR-MZA wakati umeshapunguza robo tatu ya umbali wote toka DSM,

Kwanini usijenge dry port Tabora na utumie reli ya zamani kufikisha mizigo ya ndani na nje Kigoma na Mwanza wakati unajenga SGR taratibu kwa resource za ndani hasa kutokana na ufanisi wa mizigo kadiri inavyopatikana? Kwa nini kujitwisha mzigo mzito wa madeni bila uhakika wa uwezo wa kuyalipa? Haraka ya nini?
 
Hapa naona tunapigwa kwa style ya "Confessions of An Econonic Hitman".

Kukopa si issue. Tena mikopo mingi inaanza kwa masharti nafuu. Na "debt to GDP ratio" yetu bado si mbaya sana.

Tatizo mikopo inatumiwa kwenye nini? Inaweza kutupa return on investment nzuri? Tunaweza kuirudisha? Kipindi cha masharti nafuu kikiisha, tutaweza kutupa riba kubwa mpaka kumaliza mikopo?
 
... shangaa na hili, jana tulihabarishwa kwamba "... hadi reli hii itakapokamilika itatumia kiasi cha TZS 23.3 tr/- na fedha zote ni mkopo". Ila miaka ile tulihakikishiwa kwamba "... serikali inajenga reli hii kwa fedha za ndani ..."; sasa, which is which?
 
Hii ndo shida ya kutembelea ulaya kila mara. Wanakupa kila aina ya sifa ili wakukung'ote.

Baadae kabisa tutaanza kuomba kusamehewa madeni na hapo ndo tutakuwa watumwa wao tena.
 
Kuna siku tutashindwa kulipa na yakatokea kama ya Sri Lanka. Hizo habari za tunakopesheka, deni linahimilika ni siasa tu. Hali ngumu itatukuta ghafla sana. Leo itasemwa deni linahimilika na kesho tunadefault.
 
Back
Top Bottom