Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini aomba serikali ifanye utafiti mahususi kuhusu lugha ya kufundishia nchini Tanzania

Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini aomba serikali ifanye utafiti mahususi kuhusu lugha ya kufundishia nchini Tanzania

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
FQx9EohXIAIUPur.jpeg

Mbunge wa Tabora Kaskazini, Mh. Athuman Maige ameitaka serikali kufanya utafiti wa kina kuhusu lugha ya kufundishia nchini Tanzania. Mbunge huyo amesema "Ziko tafiti zaidi ya 40 zimefanyika na zote zinasema lugha inayofaa kufundishia Tanzania ni Kiswahili, naomba serikali ifanye tena utafiti mahususi kwa ajili ya lugha ya kufundishia kwa Tanzania,"

Aidha Mh. Maige ameongeza kwa kusema "Duniani kote hakuna nchi iliyoendelea kwa kutumia lugha ya watu wengine, Uingereza wanatumia kiingereza, Wachina kichina, lakini Tanzania tunatumia lugha ya kufundishia ni Kiingereza, watoto wanasoma Kiswahili darasa la kwanza hadi la 7,"

Kauli hii inakuja baada ya mjadala mkali unaoendelea kuhusu ipi ni lugha sahihi ya kufundishia nchini Tanzania ambapo baadhi ya wadau wakitaka jitihada zaidi iwekwe kwenye kuwafundisha watoto kiingereza huku wengine wakitaka lugha ya kufundishia ibadilishwe na kuwa kiswahili kwa ngazi zote kuanzia Shule za awali mpaka chuo kikuu huku lugha ya kiingereza ikifundishwa kama somo.
 

Mbunge wa Tabora Kaskazini, Mh. Athuman Maige ameitaka serikali kufanya utafiti wa kina kuhusu lugha ya kufundishia nchini Tanzania. Mbunge huyo amesema "Ziko tafiti zaidi ya 40 zimefanyika na zote zinasema lugha inayofaa kufundishia Tanzania ni Kiswahili, naomba serikali ifanye tena utafiti mahususi kwa ajili ya lugha ya kufundishia kwa Tanzania,"

Aidha Mh. Maige ameongeza kwa kusema "Duniani kote hakuna nchi iliyoendelea kwa kutumia lugha ya watu wengine, Uingereza wanatumia kiingereza, Wachina kichina, lakini Tanzania tunatumia lugha ya kufundishia ni Kiingereza, watoto wanasoma Kiswahili darasa la kwanza hadi la 7,"

Kauli hii inakuja baada ya mjadala mkali unaoendelea kuhusu ipi ni lugha sahihi ya kufundishia nchini Tanzania ambapo baadhi ya wadau wakitaka jitihada zaidi iwekwe kwenye kuwafundisha watoto kiingereza huku wengine wakitaka lugha ya kufundishia ibadilishwe na kuwa kiswahili kwa ngazi zote kuanzia Shule za awali mpaka chuo kikuu huku lugha ya kiingereza ikifundishwa kama somo.
Hizo ndo athari zakua na wa bunge ni dhaifu na wenye elimu ya kuungauga, katika ulimwengu hu unaweza kubeza lugha ya kiingereza, kwenye nxhi yetu usio weza hata kutegeneza tooth pick, kweli tutaweza kufundisha physics chemistry biology kwa lugha ya kiswahili kweli? Kwa vitabu gani? Huyu dakitari wa kiswahili atafanya kazi wapi kwenye hospitali ya nani?
 
Watoto wa matajiri na wanasiasa wote wanasoma shule za kiingereza, shule za kiswahili ni kwa watoto wa masikini. Kwa ufupi lugha ya kiswahili ni kwa ajili ya maskini na kiingereza kwa ajili ya matajiri.
Na ni mtoto yupi wa tajiri umemuona anafanya kazi serikalini?
 
Hizo ndo athari zakua na wa bunge ni dhaifu na wenye elimu ya kuungauga, katika ulimwengu hu unaweza kubeza lugha ya kiingereza, kwenye nxhi yetu usio weza hata kutegeneza tooth pick, kweli tutaweza kufundisha physics chemistry biology kwa lugha ya kiswahili kweli? Kwa vitabu gani? Huyu dakitari wa kiswahili atafanya kazi wapi kwenye hospitali ya nani?
Dawa zote zimeandikwa kwa kiingereza sijui kutakuwa na wakalimani?
 

Mbunge wa Tabora Kaskazini, Mh. Athuman Maige ameitaka serikali kufanya utafiti wa kina kuhusu lugha ya kufundishia nchini Tanzania. Mbunge huyo amesema "Ziko tafiti zaidi ya 40 zimefanyika na zote zinasema lugha inayofaa kufundishia Tanzania ni Kiswahili, naomba serikali ifanye tena utafiti mahususi kwa ajili ya lugha ya kufundishia kwa Tanzania,"

Aidha Mh. Maige ameongeza kwa kusema "Duniani kote hakuna nchi iliyoendelea kwa kutumia lugha ya watu wengine, Uingereza wanatumia kiingereza, Wachina kichina, lakini Tanzania tunatumia lugha ya kufundishia ni Kiingereza, watoto wanasoma Kiswahili darasa la kwanza hadi la 7,"

Kauli hii inakuja baada ya mjadala mkali unaoendelea kuhusu ipi ni lugha sahihi ya kufundishia nchini Tanzania ambapo baadhi ya wadau wakitaka jitihada zaidi iwekwe kwenye kuwafundisha watoto kiingereza huku wengine wakitaka lugha ya kufundishia ibadilishwe na kuwa kiswahili kwa ngazi zote kuanzia Shule za awali mpaka chuo kikuu huku lugha ya kiingereza ikifundishwa kama somo.

Hatuna wabunge makini Tanzania tunatakiwa kufundisha lugha zote Kiswahili na kingereza kuanzia msingi. Tatizo kubwa la kiswahili peke yake hatuna vitabu wala material ya kutosha kufundisha kiswahili kwa elimu ya juu. Wataalumu wengi wameandika vitabu kwa kingereza kwasababu ya soko. Lakini vilevile hao China ambao anawasema ndiyo wanalipa mamilioni wamerakani, waingereza na waaustralia kuwafundisha kingereza. Mimi sikubaliani na hii hoja hasa pale ambako watoto wa hao wabunge wanalipa mamilioni kusomesha watoto wao english media.
 
Hata kiswahili chenyewe kinatushinda, kina maneno machache mno, sio ya kufundishia ile ni lugha ya biashara sio academics, sema tu ndo hivo hatuna national"thinking tank"
Watoto wake wanasoma kwenye academy sisi anataka tuzalishe mabaa made sijui?
 
Lugha ya kufundishia ingekua kingereza, na kiswahili liwe somo tu kama ilivyo sekondari basi hata primary ingekua hivo.

Kiswahili kina misamiati michache, tukisema kiwe lugha ya kufundishia mpaka chuo aisee kuna masomo watu watafeli sana kwa kukalili majina mapya.
 
Lugha ya kufundishia ingekua kingereza, na kiswahili liwe somo tu kama ilivyo sekondari basi hata primary ingekua hivo.

Kiswahili kina misamiati michache, tukisema kiwe lugha ya kufundishia mpaka chuo aisee kuna masomo watu watafeli sana kwa kukalili majina mapya.
Mzee unaweza kubishana na Mzalendo Richard Mabala ?😁

 
Back
Top Bottom