X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,605
- 1,843
http://en.wikipedia.org/wiki/Ted_Haggard
http://www.ted-haggard.com/
Mchungaji Ted Haggard (50), baba mwenye ndoa na watoto watano, alikuwa Rais wa shirikisho la Makanisa ya Kiivanjeli.National Association for Evangelicals.(NAE ) nchini Marekani.
NAE inasimamia makanisa yapatayo 45,000 ikiwa na idadi wa wafuasi wasiopungua milioni 30. Haggard alianzisha kanisa lake mnamo mwaka 1985 na aliweza kuwavutia watu wengi ndani na nje hadi kuchaguliwa kuwa Rais wa NAE.
Pia mchungaji Haggard licha ya kuwa mtu aliyekuwa akiheshimika sana, alikuwa ni mmojawapo wa marafiki wa Ikulu ya Marekani na chama cha Republican cha Rais Bush.
Lakini hadhi na mamlaka yote hayo yalifikia kilele siku nne kabla ya uchaguzi wa Marekani baada ya shoga Mike Jones kujitokeza na kulifumua bomu hili la uzinzi na Haggard.
Haggard alimchukiza "mpenzi" wake Jones ambaye kwa mujibu wake, walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi kwa miaka mitatu hadi Augusti mwaka huu. Mike alipoulizwa ni kwanini ameamua kujitokeza wakati huu wa uchanguzi alisema
"Kwanza ninataka kuonyesha kukerwa kwangu na Haggard kwa unafiki wake wa kupiga kampeni ya kuzuia ndoa za watu wa jinsia moja"
Mwanzoni Mchungaji Haggard alikanusha kuwa na uhusiano wa kingono kinyume cha maumbile na Jones. Alisema kuwa alikwenda kwa Jones kufanyiwa Massage. Pia katika wakati huo, alishawishika kununua madawa ya kulevya ambayo baadaye anasema aliyatupa. Alisema "Nilishawishika,nikanunua madawa lakini sikutumia niliyatupa".
Jumapili ya tarehe5 Novemba, Haggard aliandika barua kwa waumini wake kukiri kuwa alikuwa na matatizo ya ngono kwa muda mrefu. Aliongeza kuwa alikuwa muongo na mnafiki kwa muda mrefu.
Baada ya kusomwa waraka huo huko Colorado kwenye kanisa lake lenye washarika wapatao 15,000, kanisa lake rasmi liliamua kumtimua Haggard.
Hii si mara ya kwanza kwa kiongozi wa madhehebu ya kisasa ambayo yanatiliwa shaka na watu wengi kuanguka. Miaka ya themanini walianguka magwiji kama J. Baker na Jimmy Swaggart.
Kimsingi uhuru na urahisi wa kufungua makanisa haya ndicho chanzo cha matapeli wengi kufanikiwa kudanganya watu na kuwaibia kwa jina la Mungu. Hebu fikria unatoa sadaka, askofu au mchungaji wako anazitumia kuhongea mashoga na kununua madawa ya kulevya.
Kazi kwenu huko nyumbani ambako uamsho umekuwa fasheni ya hali ya juu hadi kwenye matelevisheni. Wafuatilieni viongozi wenu mjue wanaishi kimungu au la. Atakayethibitika kuwa kama Haggard mfukuzeni bila kujali kuwa ni mwanzilishi wa kanisa lenu.
http://www.ted-haggard.com/
Mchungaji Ted Haggard (50), baba mwenye ndoa na watoto watano, alikuwa Rais wa shirikisho la Makanisa ya Kiivanjeli.National Association for Evangelicals.(NAE ) nchini Marekani.
NAE inasimamia makanisa yapatayo 45,000 ikiwa na idadi wa wafuasi wasiopungua milioni 30. Haggard alianzisha kanisa lake mnamo mwaka 1985 na aliweza kuwavutia watu wengi ndani na nje hadi kuchaguliwa kuwa Rais wa NAE.
Pia mchungaji Haggard licha ya kuwa mtu aliyekuwa akiheshimika sana, alikuwa ni mmojawapo wa marafiki wa Ikulu ya Marekani na chama cha Republican cha Rais Bush.
Lakini hadhi na mamlaka yote hayo yalifikia kilele siku nne kabla ya uchaguzi wa Marekani baada ya shoga Mike Jones kujitokeza na kulifumua bomu hili la uzinzi na Haggard.
Haggard alimchukiza "mpenzi" wake Jones ambaye kwa mujibu wake, walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi kwa miaka mitatu hadi Augusti mwaka huu. Mike alipoulizwa ni kwanini ameamua kujitokeza wakati huu wa uchanguzi alisema
"Kwanza ninataka kuonyesha kukerwa kwangu na Haggard kwa unafiki wake wa kupiga kampeni ya kuzuia ndoa za watu wa jinsia moja"
Mwanzoni Mchungaji Haggard alikanusha kuwa na uhusiano wa kingono kinyume cha maumbile na Jones. Alisema kuwa alikwenda kwa Jones kufanyiwa Massage. Pia katika wakati huo, alishawishika kununua madawa ya kulevya ambayo baadaye anasema aliyatupa. Alisema "Nilishawishika,nikanunua madawa lakini sikutumia niliyatupa".
Jumapili ya tarehe5 Novemba, Haggard aliandika barua kwa waumini wake kukiri kuwa alikuwa na matatizo ya ngono kwa muda mrefu. Aliongeza kuwa alikuwa muongo na mnafiki kwa muda mrefu.
Baada ya kusomwa waraka huo huko Colorado kwenye kanisa lake lenye washarika wapatao 15,000, kanisa lake rasmi liliamua kumtimua Haggard.
Hii si mara ya kwanza kwa kiongozi wa madhehebu ya kisasa ambayo yanatiliwa shaka na watu wengi kuanguka. Miaka ya themanini walianguka magwiji kama J. Baker na Jimmy Swaggart.
Kimsingi uhuru na urahisi wa kufungua makanisa haya ndicho chanzo cha matapeli wengi kufanikiwa kudanganya watu na kuwaibia kwa jina la Mungu. Hebu fikria unatoa sadaka, askofu au mchungaji wako anazitumia kuhongea mashoga na kununua madawa ya kulevya.
Kazi kwenu huko nyumbani ambako uamsho umekuwa fasheni ya hali ya juu hadi kwenye matelevisheni. Wafuatilieni viongozi wenu mjue wanaishi kimungu au la. Atakayethibitika kuwa kama Haggard mfukuzeni bila kujali kuwa ni mwanzilishi wa kanisa lenu.