Auawa na Wanafamilia akidai Tsh. 6500/-

Auawa na Wanafamilia akidai Tsh. 6500/-

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1685203669832.png

MKAZI wa Mtaa wa Nyakabungo, Nyamagana mkoani Mwanza, Peter Domini, ameuawa kwa kushambuliwa na kupigwa na kitu chenye ncha kali wakati alipokwenda kwa jirani yake kudai Sh. 6,500.

MKAZI wa Mtaa wa Nyakabungo, Nyamagana mkoani Mwanza, Peter Domini, ameuawa kwa kushambuliwa na kupigwa na kitu chenye ncha kali wakati alipokwenda kwa jirani yake kudai Sh. 6,500.

Imeelezwa kuwa Domini alikwenda nyumbani kwa jirani yake, Julius Gaini, kufuatilia deni lake juzi majira ya saa 2:00 usiku. Baada ya kufika, aliwakuta watu watatu na kuzuka ugomvi uliowafanya watu hao kuanza kumshambulia na kusababisha kifo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Wilbroad Mutafungwa, jana alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Mutafungwa alisema baada ya taarifa hizo kufika katika Jeshi la Polisi, waliwakamata watu watatu ambao ni Julias Gaini (59),Judith John (48) na Rhoda Julius (49) wote wakazi wa Mtaa wa Nyakabungo kwa tuhuma za mauaji hayo.

“Upelelezi wa tukio hilo bado unaendelea na utakapokamilika, watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka dhidi yao. Kadhalika, niwatake watu kuacha kujichukulia sheria mkononi maana jeshi letu limejipanga kudhibiti vitendo vyote vya uhalifu,” alisema.

Katika hatua nyingine, Kamanda Mutafungwa alisema jeshi hilo linawashikilia waganga wa kienyeji 34 kwa tuhuma za kujihusisha na ramli chonganishi wakati wakitoa huduma za uganga kwa wateja wao hali ambayo imekuwa ikisababisha migogoro na mauaji katika jamii mkoani hapa.

Alisema waganga hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika wilaya za Misungwi, Ilemela, Nyamagana, Kwimba, Sengerema na Magu huku wakikutwa na vielelezo mbalimbali zikiwamo nyara za serikali.

"Tumewakamata kutokana na oparesheni iliyoanza Mei 17 hadi 24, mwaka huu, wakifanya shughuli ya uganga bila kusajiliwa huku wakitumia nyara za serikali bila kibali. Hawa watu hawafuati sheria na ndiyo chanzo cha matukio mbalimbali yasiyofaa pamoja na mauaji ya mara kwa mara," alisema Mutafungwa.

Aidha, Kamanda Mutafungwa alisema oparesheni hiyo ni endelevu huku akiwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano katika kuwafichua waganga ambao wanaleta visa vya uchonganishi ndani ya jamii kupitia ramli chonganishi na kwamba watu waliokamatwa watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

NIPASHE
 
Hebu fikiria mtu anauwawa kwa haki yake
Unadaiwa Lipa
Mimi niliacha kukopa zamani sana kwa sababu watu hawalipi na wanapokuja kukopa wana sura za huruma na sababu genuine kabisa

Mpe sasa, akikupa mgongo ndio mwisho wa kuiona ile sura ya huruma mbwa hao
 
IMEANDIKWA!
[emoji116][emoji116]
Joshua bin sira.31:31
31Usimkaripie jirani yako penye karamu ya mvinyo, wala usimdhihaki anapocheka; wala usimwambie neno la shutumu, wala usimsumbue kwa kutaka alipe deni.
 
View attachment 2637026
MKAZI wa Mtaa wa Nyakabungo, Nyamagana mkoani Mwanza, Peter Domini, ameuawa kwa kushambuliwa na kupigwa na kitu chenye ncha kali wakati alipokwenda kwa jirani yake kudai Sh. 6,500.

MKAZI wa Mtaa wa Nyakabungo, Nyamagana mkoani Mwanza, Peter Domini, ameuawa kwa kushambuliwa na kupigwa na kitu chenye ncha kali wakati alipokwenda kwa jirani yake kudai Sh. 6,500.

Imeelezwa kuwa Domini alikwenda nyumbani kwa jirani yake, Julius Gaini, kufuatilia deni lake juzi majira ya saa 2:00 usiku. Baada ya kufika, aliwakuta watu watatu na kuzuka ugomvi uliowafanya watu hao kuanza kumshambulia na kusababisha kifo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Wilbroad Mutafungwa, jana alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Mutafungwa alisema baada ya taarifa hizo kufika katika Jeshi la Polisi, waliwakamata watu watatu ambao ni Julias Gaini (59),Judith John (48) na Rhoda Julius (49) wote wakazi wa Mtaa wa Nyakabungo kwa tuhuma za mauaji hayo.

“Upelelezi wa tukio hilo bado unaendelea na utakapokamilika, watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka dhidi yao. Kadhalika, niwatake watu kuacha kujichukulia sheria mkononi maana jeshi letu limejipanga kudhibiti vitendo vyote vya uhalifu,” alisema.

Katika hatua nyingine, Kamanda Mutafungwa alisema jeshi hilo linawashikilia waganga wa kienyeji 34 kwa tuhuma za kujihusisha na ramli chonganishi wakati wakitoa huduma za uganga kwa wateja wao hali ambayo imekuwa ikisababisha migogoro na mauaji katika jamii mkoani hapa.

Alisema waganga hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika wilaya za Misungwi, Ilemela, Nyamagana, Kwimba, Sengerema na Magu huku wakikutwa na vielelezo mbalimbali zikiwamo nyara za serikali.

"Tumewakamata kutokana na oparesheni iliyoanza Mei 17 hadi 24, mwaka huu, wakifanya shughuli ya uganga bila kusajiliwa huku wakitumia nyara za serikali bila kibali. Hawa watu hawafuati sheria na ndiyo chanzo cha matukio mbalimbali yasiyofaa pamoja na mauaji ya mara kwa mara," alisema Mutafungwa.

Aidha, Kamanda Mutafungwa alisema oparesheni hiyo ni endelevu huku akiwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano katika kuwafichua waganga ambao wanaleta visa vya uchonganishi ndani ya jamii kupitia ramli chonganishi na kwamba watu waliokamatwa watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

NIPASHE
Alienda kudai 6500 kwa staili gani? tuanzie hapo
 
Mwanza ,Musoma , Kenya, kuuwa kwao nisawa tu geita poa tu hata huku kwetu Raha tu Kwa wameru kuua sawa tu , kitu kidogo hata sisi warusha , wachagga sawa tu kwao nikawaida
 
Hii ni ugonjwa wa akili unaozidi kuiandama Tanzania na Dunia Kwa ujumla
 
Afu utasikia watu wanasimama jukwaani, thithi ni matajili kweri kweri
 
Leo sio Geita ni Mwanza. Ila kuna kitu fulani kinatembea kwenye damu ya jamii ya hiyo mikoa, huwezi sikia eti Mzaramo kamuua mtu kisa 6500
 
Back
Top Bottom