AUGUST ni Mwezi wa SENSA! Mwezi wa kutambulika

AUGUST ni Mwezi wa SENSA! Mwezi wa kutambulika

kevylameck

Member
Joined
Nov 3, 2013
Posts
18
Reaction score
19
3AA2BFFF-D71C-44FC-8E4E-F9D18EA31337.jpeg

Baadae mwezi huu,Jumanne ya August 23 kutafanyika tukio kubwa, la kihistoria na lililobeba mustakabali wa maendeleo yetu.

Baada ya miaka 10 kupita,Sensa ya watu na makazi ya mwaka huu itakuwa ya sita kufanyika nchini baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Sensa nyingine kulingana na Sheria ya Takwimu Sura 351 kifungu kidogo cha 6(2)(a) zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988, 2002 na August 2012.

Sensa ni zoezi la kupata idadi ya watu wote nchini, kwa umri na jinsi, mahali wanapoishi, viwango vyao vya elimu, hali ya ajira, hali ya vizazi na vifo, hali ya makazi na taarifa nyingine nyingi muhimu.

Zoezi la sensa hufanyika kwa kutumia karani wa sensa kwenye eneo la kijiografia ili kuhesabu kaya na watu wote waliolala kwenye kaya husika usiku wa kuamkia siku ya sensa pamoja na kuchukua taarifa zao kulingana na maswali yaliyopo kwenye dodoso.

Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wetu, anasema takwimu sahihi kuhusiana na watu ambazo zimechambuliwa na kuainishwa kwa makundi, ukubwa na mtawanyiko wa watu na makazi ni muhimu katika kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo

Takwimu na taarifa zitakazokusanywa zitatumika baadae kupanga na kutunga sera za kiuchumi, kijamii na mazingira na pia kutathmini ubora wa hali ya maisha ya watanzania kwa ujumla.

Kulingana na Katibu wa Umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Kenani Kihongosi, anasema serikali inatambua kuwa ni vigumu kupata maendeleo endelevu bila kuwa na takwimu sahihi na za kuaminika kuhusu watu wake pamoja na makazi yao.

Katika Kampeni zake, Kenani Kihongosi anasema ni wajibu wa kila Mtanzania kujiandaa na kushiriki na kutimiza wajibu wake kufanikisha zoezi hilo la kitaifa.

Karibu August! Karibu mwezi wa kuhesabiwa! Mimi nimejiandaa na nipo tayari kuhesabiwa. Wewe je?

#Ushirikiwakonimuhimu
#Sensakwamaendeleo
#Sensainaharakishamaendeleo
 
Msimu wa Sensa huwa nakumbuka kitabu pendwa aka Ngoswe Penzi kitovu cha uzembee. Muzeee ngengemkeni mitomingii
 
TUJIKUMBUSHE 😊SENSA NA NGOSWE, "Penzi kitovu cha uzembe"

KISA CHA NGONSWE NA SENSA

👇🏽👇🏽👇🏽👇🏽👇🏽
MITOMINGI; nadhani sasa mgeni amekwisha kumaliza kula hebu nenda kaondoe vyombo

MAMA_MAZOEA; Basi fanya haraka (Mazoea anatoka, anaenda kwa Ngoswe alipo).

MAZOEA; Hodi! Hodi!

NGOSWE; Karibu

MAZOEA; (Akiingia). Ahsante. Nimekuja kuchukua vyombo.

NGOSWE; Vyombo! Kaa basi mbona unasimama kama vile hakuna viti.

MAZOEA; Nimeambiwa nifanye haraka.

NGOSWE; Mmm! Haya ngoja ninawe basi (Ngoswe ananawa kwa taratibu jicho likiwa usoni mwa Mazoea ambaye anatazama kando). Hivo mzima wee?

MAZOEA; Bee?

NGOSWE; Salama?

MAZOEA; Salama tu.

NGOSWE; Sasa ndio umekataa kukaa?

MAZOEA; (Ajidai hakusikia) Si umekwisha maliza?

NGOSWE; Bado kidogo.

MAZOEA; Basi nitakuja chukua baadaye. (Ataka kutoka)

NGOSWE; Basi nenda navyo. (Mazoea anarudi kuinama kuvichukua. (Ngoswe kwa sauti ndogo). Hivyo waitwa nani?

MAZOEA; Mie?

NGOSWE; Ndio wewe hapo kisura.

MAZOEA; (anatabasamu huku akiondoka). Mazoea!i

Story ni tamu ila tulishaambiwa ya Ngoswe tumuachie Ngoswe
! ! !


JIANDAE KUHESABIWA
 
Back
Top Bottom