Augustine Lyatonga Mrema BADO ni Mwanachama Hai wa CCM

YES. Nakumbuka Mwalimu siku moja alikuwa akizungumza na waandishi wa habari 1995 akasema ili kuwepo na upinzani wa kweli lazima mtu atoke ndani ya CCM. Hivyo akamshauri Mrema ahamie NCCR baada ya kuzungumza na kina Marando. Kwenye uchaguzi mkuu wa 1995 Mrema akatangaza lengo lake la kugombea urais kupitia NCCR. Mwalimu akamwita akamwambia akagombee ubunge aachane na urais Mrema akamkatalia tena akazungumza hadharani akasema ''Nyerere huyo huyo aliyeniambia niondoke CCM niende upinzani ni Nyerere huyo huyo anayeniambia nisigombee urais nigombee ubunge.'' Sasa hapa utajua wazi kuwa Mrema amewekwa kama mvurugaji wa upinzani. Ndo maana anawashawishi wenzake waungane na wakishaungana ikikaribia uchaguzi anawavuruga wote wanagombana mara CCM inashinda. Huyu ni ndumila kuwili hafai kabisa.
 


Mh! afadhali umeliona hili. Kuna watu humu ndani wanajiona kama ndo wana haki ya kuanzisha thread. Yani kuna watu hata akianzisha thread isiyokuwa na maana(mf kushabikia ulevi, uzinzi n.k) utaona wachangiaji weeeengi sana. Tunakubali kuwa kuna watu wamejiunga na jf zamani, na labda waliwahi kutoa michango muhimu ktk mada mbalimbali, lakini tabia ya kuwakebehi new/junior/less popular members nimekuwa nikiiona kwa chini chini, na inakatisha tamaa. Najua kweli kuna watu wengine wanajiunga humu au wanabadilisha username ili kupromote hisia/misimamo yao au hata vyama vyao, naomba watu hao tuwajibu kwa hoja na si kuwaprovoke eti wametumwa kwani kwa kufanya hivyo tunawaumiza wale wasiokuwa na lengo baya!

Hii ni observation yangu binafsi, i stand to be corrected!
 
Kama Lyatonga anaendelea kulipia fee ya kila mwaka ya kadi yake tangu atoke CCM, hapo tunaweza kusema ni mwanachama hai. Vinginevyo mmmmmmmmmmh.
 
Aisee kama mnasema mzee Mrema ni CCM eenhe basi nyie wote hamju...hamjui kweli..Mzee Mrema ni Mpinzani wa Kwe.....Wakweli..Kama Mnabisha eeenhe Nyie piteni morogoro road eenhe Ukipita pale Kagera Karibu na Mwembechai Mtaona Ofisi ya.....Yake kweli.....Huyu Mzee eeenhe aiseee ni Mpambana........Mpambanaji Kweli...na yuko tayari kufa kwa ajili ya Maslai ya watanzani.......Watanzania kweliii...
Mpaka hapo nimemaliza utetezi wangu kwa Mzee Mre....Mrema Kweliii....Na mwenye Wivu Na ajinyo.....ajinyonge Kweli....
 
nimekuja kugundua kuna watu huma wanajiona wapo deep sana kifikra na kimtizamo wa mambo kiasi cha kuona wengine hawafai, huyu mchokonozi kaleta alichokipata kutoka kwenye vyanzo vyake, cha msingi angeombwa ushahidi, ila sio mnaojifanya wajuzi wa mambo kuanza kutoa kashfa za kishamba...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…