Australia kuitambua Palestina kama taifa huru

Biblia ilishaweka wazi mgogoro wa Israel na Palestina ndo unatupeleka kwenye vita ya Halimaghedonia - Israel vs UN army ikiongozwa na Rusia na USA ambapo mpaka nyuklia zitatumika, mdogo mdogo nchi za Ulaya, Amerika zinaanza kuona Israel ni nchi korofi na hatari kwa usalama wa dunia, jaribio la mwisho ni USA kuikimbia Israel baada ya kumdharirisha kiongozi wa kidini ambaye ataende Israel na kukiuka taratibu zao za Ibada na kutaka aabudiwe yeye kama Yesu Kristo na wakati atakuwa ni Yesu take( nabii wa uongo)
 

1. Kwa hIyo unadhani ungeweza ikawa umefunuliwa kuwa mtumwa was kudumu tu hapa duniani na kuwa hIyo ingekuwa sawa pia?

2. Labda hapa niulize wewe umefunuliwa kuwa nani ndugu?

3. Hapa nitambue wamasai wanaamini ng'ombe wote duniani ni wa kwao. Hii ni hata kama wangekuwa china, marekani nk huko; au watusi wenye kuamini wao ndiyo wanapaswa kuwa viongozi kokote duniani hata china Huko.

4. Hapo #3, huoni Kila MTU akija na Imani yake hakutakalika duniani hapa?

6. Vipi kuhusu ya usawa wa binadamu, je yako na maana yoyote Ile kwako?

Nimechangia hoja yako kwa mtazamo wangu wa kiimani, nawe pia hubanwi kuona mantiki yoyote ile ndani ya maudhui yake. Ni vyema ukakipuuzia kile nilichokichangia kama unaridhika kuwa hakina maana.

1. Kuchangia mada kwa mtazamo wako hakuna maana tusiweke maoni yetu kwenye maoni yako. Au hakuwezi kuwa na maana unachoona ndiyo iwe hicho hicho tu na tena kutingishwa tukaiona misingi ya Hoja zako?

2. Hoja zako SI ni lazima tuzipime Kwa vigezo vyote vilivyopo; wakisema dhahabu hujaribiwa Kwa moto? Au?

3. Au nasema uongo Ndugu yangu?
 

1. Hapo kwenye kufungamanishwa mgogoro wa Wadai ardhi na masuala ya dini ni Tatizo kubwa la msingi.

2. Unatambua Israel wakristo ni 1.6% na wala mwisraeli si kuwa yuko vitani kumpigania Yesu? Wala mpalestina kumpigania Muhammad?

3. Baada ya kuyasema hayo tukumbuke kuzitunza posts hizi kukumbushana pale huu upepo ukishapita kwani tayari unaelekea kwema:

Israel's Gaza withdrawal hints at what comes next

4. Hivi yakiisha salama na kukawepo muafaka wa kudumu, utauweka wapi uso wako?
 
Mkuu hakuna haja ya kuwa na malumbano ambayo hayawezi kukusaidia wewe wala mimi. Kwa jinsi ambavyo naona unazijenga hoja zako natambua kuwa u muelewa ila unasumbuliwa na tatizo la kuchagua upande ambao unahisi unaonewa.

Hii ni kawaida ya ubinadamu, "prejudice & bigotry" ni sehemu yake. Kwa hiyo kwa vyovyote vile huwezi kukubaliana na kile ambacho Israel inakifanya dhidi ya Hamas kama "retaliation". Je! Shambulizi la Hamas la October 2023 dhidi ya Israeli na uchukuaji wa mateka wewe unalichukuliaje!?

Je! Israeli haikuwa na haki ya kuchukua hatua na kujilinda dhidi ya wanamgambo wa Hamas ambao wanajificha katika makazi ya raia wema na maeneo mengine yenye huduma za kijamii kama vile vituo vya afya na nyumba za ibada!?

Mimi jinsi nilivyo na pia kile nichokifanya katika kuendesha maisha yangu ndiyo maana halisi ya wito wangu kwa Mungu wangu. Ni vile kama wewe ulivyokuwa katika maisha yako, na kile ambacho unakiamini kuwa ni mungu wako, kwa kuwa mimi wala sikijui, na pia wala sihitaji hata kukijua.
 
Mkuu hakuna haja ya kuwa na malumbano ambayo hayawezi kukusaidia wewe wala mimi. Kwa jinsi ambavyo naona unazijenga hoja zako natambua kuwa u muelewa ila unasumbuliwa na tatizo la kuchagua upande ambao unahisi unaonewa.

1. Mkuu ipo Tofauti baina ya malumbano na majafiliano.

2. Hoja hupingwa Kwa hoja na kama binadamu kazinya bongo zetu ni kufanya uchbuzi wa haki kama ilivyo kazi ya miguu kutembea au kukimbia.

3. Wakati malumbano hayana tija ila majafiliano yana faida kubwa kwa afya ya akili.

4. Nikweli kwamba ni naamimi kuwa uonevu wowote haukubaliki na hata Mungu haukubali. Ndiyo maana hata Mungu hatawaacha salama waonevu wowote.


1. Oct 7 ilikuwa ni mwendelezo wa mapambano ya wapalestina katika mzozo wa vita ulioanzia 1947 huko.



2. Oct 7 wapalestina hawakuvamia maeneo ya waisraeli bali waliingia kwenye maeneo yao yanayokaliwa na adui.



3. "Right of retaliation" kwenye maeneo au vitu vya wizi, Israel anaipata wapi? Hii ni sawa na mwizi kupambana na wanao mwandama kwenye eneo la tukio.

Je! Israeli haikuwa na haki ya kuchukua hatua na kujilinda dhidi ya wanamgambo wa Hamas ambao wanajificha katika makazi ya raia wema na maeneo mengine yenye huduma za kijamii kama vile vituo vya afya na nyumba za ibada!?

1. Israel kama mvamizi, hana haki ya kupambana na aliowavamia kwenye maeneo yao.

2. Kumbe tofauti ya harakati hizi za ukombozi wa Palestina na vita vya Maji maji au Mau mau au vita vya kupigania uhuru kokote ni nini?

Kama Maji Maji au Mau Mau ilikuwa halali, iweje lawama kwa wapalestina?


1. Hapa ndipo unapopaswa kutambua hata sisi kama Palestina walipo, tumepita kwenye ukoloni na utumwa labda kama huu huu au hata mbaya zaidi.

2. Uko hapa Leo ulipo au nilipo jwa sababu kuna watu (kina Kinjekitile, mkwawa, nk) waliojitolea maisha yao kutupigania na hapa tulipo twala matunda kwa raha zetu.

3. Hudhani wapalestina Hawa nao wanayo haki ya kujitoa kupigania haki ya taifa lao ili angalau wajukuu wa wajukuu zao waje kuishi kwa amani kama wewe na mimi hata kama itawagharimu wao leo?

4. Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kutaka vita isiyokuwa na sababu. Lakini vipi akija mtu kukutoa makazini kwako, wewe au wanao? Utampisha Kwa sababu labda kuwa Mungu alimpangia yeye kuja kukutoa na kukufanya wewe mtwana wake?

5. Wadhani maazimio yote haya ni kwa kuionea Israel?

 
Safi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…