Avamiwa na Siafu baada ya kukataa kumuoa bintie mganga

Avamiwa na Siafu baada ya kukataa kumuoa bintie mganga

SheriaE

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2018
Posts
606
Reaction score
447
KENYA: Avamiwa na Siafu baada ya kukataa kuoa binti ya mganga

Kijana aliyekodi nyumba ya kifahari ya mganga eneo la Kiritiri kaunti ya Embu nchini Kenya alilazimika kuhama alipovamiwa na siafu baada ya kukataa kuoa binti wa mpiga ramli huyo. Inaaminika kuwa tangu alipohamia katika nyumba hiyo, mpiga ramli huyo amekuwa akimshawishi amuoe binti yake, kwa ahadi kuwa kama akifanya hivyo, atampa jumba lake hilo la kifahari.

Hata hivyo, kijana huyo alimwambia mganga kwamba hawezi kumuoa bintiye kwa kuwa hampendi. Inaelekea hilo lilimuudhi mganga huyo kwani siku moja kijana alipokuwa amelala usiku alivamiwa na siafu, na hivyo kumbidi kuhama nyumba hiyo.

Source: CRI Kiswahili
 
Kenya kwa uchawi hawajambo juzijuzi makamu wao wa rais ameenda kwa waganga kufanyiwa zindiko
 
Sumbawanga na Nigeria imehamia Kenya siku hizi
 
hongera sana waganga wetu naona kazi inaendeleaaa mazeee....ongezeni juhudi pia kwa haka kaugonjwaaa!!
 
Picha za hilo jumba la kifahari la mganga tafadhali, video za siafu zikimng'ata huyo mpangaji!
Halafu ikipatikana picha ya mganga na bintiye itapendeza...
 
Picha za hilo jumba la kifahari la mganga tafadhali, video za siafu zikimng'ata huyo mpangaji!
Halafu ikipatikana picha ya mganga na bintiye itapendeza...
CRI Kiswahili wameripoti.
 
Back
Top Bottom