Aveva na "genge" lako.. Jipimeni Mapema

Hahahahaha eti mchezaji anaecheza namba zote hizi ngonjera wasipokuwa makini msimu ujao simba itafuata mkondo wa timu za Tanga
 
Karibu tena sembo najua nitaendelea kupata updates za simba nw
 
Hata Mimi nasikia kua "Mfanyabiashara" Mo anaitaka Simba.. Tunatakiwa tutafakari sana kabla ya kumkabidhi timu huyu "Mfanyabiashara".
Alishindwa kuihudumia Mbagala Market ataiweza Simba?
 

Mbagala market aliitelekezea wapi huyu Mo?
 
Mbagala market aliitelekezea wapi huyu Mo?
Hili ndilo hata Mimi linanipa ukakasi.. Kama alishindwa vidogo.. Ataweza vikubwa kweli?
Tunatakiwa tuwe makini sana katika hili.
 
Mbagala market aliitelekezea wapi huyu Mo?
.....acheni kushadadia mambo yaliyopita wakati sasa hivi Simba inafanya vibaya,hao mbagala market huwezi kuwaweka kundi moja na Simba,muacheni mwenye pesa achukue timu awekeze hadhi ya Simba irudi,habari ya kuhukumu kabla hajafanya chochote ni ujinga tu!,vinginevyo endeleeni kuuliza maswali yenu ya kitoto Simba iendelee kugeuzwa paka!
 
Kumbe tupo wengi tulioshtukia huu mchezo wa viongozi wa simba kucheza na akili zetu kutumia magazeti. Kwanza walishatudanganya sana kuanzia miaka hiyo mara aucho halid, mavugo, mshambuliaji na kipa wa gor mahia (majina yamenitoka) n.k. tukaishia kuona wakina nserekuma na papa ndaw. Kamati ya ufundi inasema ina listi wachezaji 33 wanataka kuwasajili hivi kila mwaka simba inaundwa upya? Kamati makini ya ufundi ingekuwa na listi ya wachezaji wasiozidi 10 saba wa ndani na 3 wa nje kwani timu inaanza kuundwa na wachezaji waliopo unaendelea kuwapunguza taratibu kila mwaka then ndani ya miaka 3 unapata timu imara. Inaelekea hata hawajui mapungufu ya simba nini? Halafu unaanza kuajiri kocha au unaanza kusajili wachezaji? Je wachezaji unaosajili wasipoendana na mfumo wa kocha alumiwe nani mbele ya safari?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…