kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Awanu ya sita ni awamu ya Katiba, ni ushahidi tosha kuwa kutii na kuheshimu Katiba ya nchi kunalipa sana. Taifa limevuka salama baada ya kifo cha Mh. Rais Magufuli kwakuwa Katiba yetu haikupepesa macho juu ya Rais ajae baada ya Rais aliyeko kubata bahati mbaya. Katiba yetu ndiyo Nyangumi wetu aliyetuvusha kutoka kwenye maji marefu yaliyojaa papa wengi kwenda nchi kavu.
Hivyo ni wito wangu kwa viongozi wote wa Awamu ya Sita kuwa waendelee kuiheshimu Katiba kwa 100% kuliko awamu zote zilizopita. Viongozi wa awamu ya 6 waitekeleze Katiba mstari kwa mstari, kifungu kwa kifungu na ukurasa kwa ukurasa, na ikiwezekana waiboresha sana kuliko ilivyo sasa ili kuondoa maeneo yote kwenye Katiba yasiyotutakia mema kama taifa.
Itakuwa sio sawa kama Katiba tunayoapa kuilinda inaruhusu uhuru wa vyama vya siasa, uhuru wa habari, uhuru wa kujumuika, uhuru wa kuchagua na kuchaguliwa, uhuru wa kupiga kura na kupigiwa kura, na uhuru wa kuishi lakini kuna kiongozi au mtendaji kwa utashi wake na sababu zake anaamua kuzuia na kuuminya uhuru huo. Kufanya hivyo ni kukosea sana, maana inaonekana unachagua kuheshimu zile sehemu tamu kwako za Katiba na kuchukia sehemu chungu kwako za katiba.
Awamu hii ya 6 lazima ifanye mengi sana kuhusu Katiba yetu hii.
Hivyo ni wito wangu kwa viongozi wote wa Awamu ya Sita kuwa waendelee kuiheshimu Katiba kwa 100% kuliko awamu zote zilizopita. Viongozi wa awamu ya 6 waitekeleze Katiba mstari kwa mstari, kifungu kwa kifungu na ukurasa kwa ukurasa, na ikiwezekana waiboresha sana kuliko ilivyo sasa ili kuondoa maeneo yote kwenye Katiba yasiyotutakia mema kama taifa.
Itakuwa sio sawa kama Katiba tunayoapa kuilinda inaruhusu uhuru wa vyama vya siasa, uhuru wa habari, uhuru wa kujumuika, uhuru wa kuchagua na kuchaguliwa, uhuru wa kupiga kura na kupigiwa kura, na uhuru wa kuishi lakini kuna kiongozi au mtendaji kwa utashi wake na sababu zake anaamua kuzuia na kuuminya uhuru huo. Kufanya hivyo ni kukosea sana, maana inaonekana unachagua kuheshimu zile sehemu tamu kwako za Katiba na kuchukia sehemu chungu kwako za katiba.
Awamu hii ya 6 lazima ifanye mengi sana kuhusu Katiba yetu hii.