Awamu ya Sita, Vitendo vinaongea zaidi kuliko Maneno

Awamu ya Sita, Vitendo vinaongea zaidi kuliko Maneno

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Tunasema tunataka kukuza ajira kwa vijana, tumepata mikopo kwa ajili ya kukuza Teknolojia. Tunasema Teknolojia ndio kila kitu kwa Dunia ya sasa, tunashauri vijana wajifunze na kuwekeza kwenye teknolojia, ni Vema na Haki, yet tunasababisha kitendea kazi muhimu (bundle) kisishikike; hapo tunajenga au tunabomoa.

Internet Bundles
Dunia ya sasa ni (Information at your fingertips), kila information unaweza ukaipata bure mtandaoni. Unaweza ukajifundisha mwenyewe jambo ambalo lingewachukua watu wa karne za nyuma miaka kulifanyia research leo unaweza ukalifanya kwa siku. Ni kama kipindi kile cha Maktaba kila mkoa ili watu wajifunze hii ndio maktaba ya leo. Kama kipindi kile ambapo hatukugeuza Maktaba kama kitega uchumi cha kuongeza pesa ni vema tusigeuze hii Source of Information kama kibubu cha kujichotea Pesa.

Je, Gharama za Bundle ni Kosa la Serikali au Mitandao, nani wa kulaumiwa?
Unaweza kusema watu wa mitandao ni wezi, si kweli, sababu ni Serikali ndio imeamua kutoa bei elekezi kwahiyo hizo bei ni maelekezo ya Serikali, na unapotoa bei elekezi ushindani unapatikana vipi? Kulikuwa na kipindi cha offer za Vifurushi vya Bundle za Bure mida fulani au hata usiku, sasa ukipangia watu bei elekezi na kila mshindani akafuata hizo bei unadhani kuna umuhimu wa mtoa huduma kutoa offer / vifurushi?

Kipi Kifanyike
Ni rahisi sana;
  • Serikali ina kampuni yake TTCL na nyingine ambayo wana share nyingi Airtel, kwanini wasiwekeze huko na kufanya shamba darasa na kushusha bei kama wanavyotaka ili iwe mfano?
  • Pili, Serikali iwaache hao wengine wajivinjari kama wanavyojua bila kuwapangia wala kuwaingilia, ili nguvu ya soko ipange bei hata wakifanya cartel Serikali ina TTCL itabakia bei za chini watu watahamia TTCL.
  • Kwa kutumia kampuni yao hawashindwi kuweka free surfing kwa mitandao kama Youtube kwa ajili ya watu kujifunza hata masaa ya usiku au zile freeware softwares kuzifanya mtu aweze kuzi-download bure.
Tutakuza Teknolojia kwa kufanya vitendea kazi kuwa gharama rafiki na sio vinginevyo.
 
Ngoja wakamzonge mama ili wazipige hizo za mmarekani.
Maana stupid haiwapunguzii ladha ya hela wanazoiba
 
Hii ni awamu ya kupigiwa soga tu na chereko chereko nyingi ila matendo ni ziro kabisa.

Stupid pumbavu kabisa.
 
Tunasema tunataka kukuza ajira kwa vijana; tumepata mikopo kwa ajili ya kukuza Teknolojia; Tunasema Teknolojia ndio kila kitu kwa Dunia ya Sasa, tunashauri vijana wajifunze na kuwekeza kwenye teknolojia - Ni Vema na Haki; Yet tunasababisha Kitendea Kazi Muhimu (Bundle) kisishikike...; Hapo tunajenga au tunabomoa

Internet Bundles
Dunia ya sasa ni (Information at your fingertips); kila information unaweza ukaipata bure mtandaoni; unaweza ukajifundisha mwenyewe jambo ambalo lingewachukua watu wa karne za nyuma miaka kulifanyia research leo unaweza ukalifanya kwa siku. Ni kama kipindi kile cha Maktaba kila mkoa ili watu wajifunze hii ndio maktaba ya leo; kama kipindi kile ambapo hatukugeuza Maktaba kama kitega uchumi cha kuongeza Pesa ni Vema tusigeuze hii Source of Information kama kibubu cha kujichotea Pesa.

Je Gharama za Bundle ni Kosa la Serikali au Mitandao; Nani wa Kulaumiwa
Unaweza kusema watu wa mitandao ni wezi; Si kweli, sababu ni Serikali ndio imeamua kutoa bei elekezi kwahio hizo bei ni maelekezo ya Serikali; na unapotoa bei elekezi ushindani unapatikana vipi ? Kulikuwa na kipindi cha offer za Vifurushi vya Bundle za Bure mida fulani au hata usiku; sasa ukipangia watu bei elekezi na kila mshindani akafuata hizo bei unadhani kuna umuhimu wa mtoa huduma kutoa offer / vifurushi ?

Kipi Kifanyike
Ni rahisi sana....
  • Serikali ina kampuni yake TTCL na nyingine ambayo wana Share nyingi Airtel; Kwanini wasiwekeze huko na kufanya shamba darasa na kushusha bei kama wanavyotaka ili iwe mfano ?
  • Pili Serikali iwaache hao wengine wajivinjari kama wanavyojua bila kuwapangia wala kuwaingilia ili nguvu ya soko ipange bei hata wakifanya cartel Serikali ina TTCL itabakia bei za chini watu watahamia TTCL
  • Kwa kutumia kampuni yao hawashindwi kuweka free surfing kwa mitandao kama Youtube kwa ajili ya watu kujifunza hata masaa ya usiku au zile freeware softwares kuzifanya mtu aweze kuzi-download bure.....
Tutakuza Teknolojia kwa kufanya vitendea kazi kuwa gharama rafiki na sio vinginevyo....
Of course kiwango Cha propaganda na vitisho hakuna
 
Of course kiwango Cha propaganda na vitisho hakuna
Mkuu hata umesoma nilichoandika... In Summary ninachosema ni kwamba tunasema tunataka kukuza teknolojia wakati ni sisi ndio tunasababisha bei ya Bundle kuwa kubwa wala sio mitandao ya Simu kama wengi wanavyofikiri
 
Mkuu hata umesoma nilichoandika... In Summary ninachosema ni kwamba tunasema tunataka kukuza teknolojia wakati ni sisi ndio tunasababisha bei ya Bundle kuwa kubwa wala sio mitandao ya Simu kama wengi wanavyofikiri
Huyo ni mlamba asali ametoka kurina huko mambo ya maana kama haya wala hawezi kuchangia
 
Kwenye Makala moja ya Citizen mwaka huu ambapo wanasema huenda tukalipia Internet bei ya chini hapo baadae

Kwenye Makala hio nape amekuwa qouted kwamba Awamu ya Sita inafanya mambo kadhaa ili bei zishuke moja ya hayo mambo ni:-
  • the government seeks to remove excise duty, which telecommunication operators say gobbles up at least 40 percent of their revenues.
  • We are proposing to abolish the 17 percent excise duty on ICT-related services. This duty is usually charged to discourage the use of products such as alcohol and cigarettes, but since ICT is a human right, we shall remove this duty,” Mr Nnauye reaffirmed.

  • government intends to reduce the so-called “right of way” levies charged by the Tanzania National Roads Agency (Tanroads) and Rural and Urban Roads Agency (Tarura) when an institution want to have the right to use a road reserve for its undertaking.
    “For instance, when TTCL wants to lay down its fibre optic cables, it has to pay $1000 per kilometre to the said institution depending on jurisdiction, yet Tanesco pays only $5, and water authorities pay $20 per kilometre, but in Rwanda it is zero tariff, although Kenya and Uganda charge $30 and $50, respectively,” he explained. According to Mr Nnauye, the ministry is proposing zero tariff,

Vilevile wamekuwa wakijinasibu kwamba Bei ya MB Tanzania ni ndogo kuliko nchi nyingi zingine wanasahau kwamba watanzania walikuwa hawanunui kwa njia ya MB bali vifurushi ambavyo kwao ndio vilikuwa cheaper ukizingatia income zinatofautiana kwahio huwezi kulinganisha nchi moja na nyingine...

Bali swali langu kubwa kwa ndugu Waziri hata hizo kodi wakiziondoa bei itakuwa ndogo kiasi gani sababu kwa maneno yao hata sasa Bei kwa MB ni ndogo; vilevile jambo la Pili hizi Kodi hazijaanza jana kwanini kuna mpando wa Ghafla wa Bundle na hakuna pa kukimbilia sababu mitandao yote ni kama bei zinafanana ?

Kwanini wasijikite kwenye Kampuni yao na kushusha bei kuliko kuchokonoa na kuwapangia watu mwisho wake wanaharibu ?
 
Hili swala wanaloliita uchumi WA digitali huwa linanishangaza, data inatakiwa iwe nafuu bila hivyo ni ngumu Sana Kwa vitu vingi kwenda mfano mzuri filamu za kitanzania zinakumbana na ugumu kunufaika Kwa kiwango kikubwa na intaneti ndio maana app kama swahiliflix au kipaji app zimekufa. Sasa uchumi WA digitali na ubunifu unaujengaje kimtindo huu.

Ripoti ya National Security Commission on Artificial Intelligence ya USA inaisisitizia serikali kufanya kila namna kuhakikisha intaneti inakuwa cheap maana data ndio msingi WA AI technology na kumbuka USA data ni cheap. Mwaka 2013 Vodacom ulikuwa unapata unlimited Kwa shilingi 200 usiku

Serikali haipaswi kuchochea monopolistic behaviour na iache intervention isiyo na msingi
 
Hili swala wanaloliita uchumi WA digitali huwa linanishangaza, data inatakiwa iwe nafuu bila hivyo ni ngumu Sana Kwa vitu vingi kwenda mfano mzuri filamu za kitanzania zinakumbana na ugumu kunufaika Kwa kiwango kikubwa na intaneti ndio maana app kama swahiliflix au kipaji app zimekufa. Sasa uchumi WA digitali na ubunifu unaujengaje kimtindo huu.
Achana na kuwa rahisi tu, nina uhakika kama Serikali isingekuwa na uroho wa Tozo wangewaachia hawa jamaa hawashindwi kuingia mikataba na hawa wenye filamu watu wakawa wana-stream bure pesa za matangazo wakagawana na wenye kazi zao..., ila wao ndio wanaharibu mbaya zaidi mwananchi hajui mbaya ni nani analaumu mwingine...., Kweli Kikulacho Kingouoni Mwako.......
Ripoti ya National Security Commission on Artificial Intelligence ya USA inaisisitizia serikali kufanya kila namna kuhakikisha intaneti inakuwa cheap maana data ndio msingi WA AI technology na kumbuka USA data ni cheap. Mwaka 2013 Vodacom ulikuwa unapata unlimited Kwa shilingi 200 usiku

Serikali haipaswi kuchochea monopolistic behaviour na iache intervention isiyo na msingi
Naama achana na miambili kuna hata vifurushi vilikuwa vya bure kuanzia usiku wa manane mpaka saa 12 asubuhi, ila wao wameamua ku-fix ambapo hapajavunjika badala yake wamevunja kila kitu....

Narudia tena kama wao ni Thinktanks wa nchi kwanini wasijaribu kuifanya TTCL kama shamba Darasa kweli nyumbani kunoge ili turudi ?!! (Ila haaa, Hapana nyumani wameharibu na huku kwa majirani tulipokumbilia nako wanabomoa)..... Ila siwalaumu until the day ambapo mwananchi atafuatilia nini ni nini na kipi ni kipi tutaendelea na hizi ngonjera....
 
Kwanini internet itegemee kampuni za simu?
Lazima tutafute gharama nafuu ya internet kivingine...free WiFi community village mbona nchi nyingi Sana wanafanya??
 
Kwanini internet itegemee kampuni za simu?
Lazima tutafute gharama nafuu ya internet kivingine...free WiFi community village mbona nchi nyingi Sana wanafanya??
Tatizo sio Makapuni ya Simu; Hilo lingekuwa Tatizo kipindi fulani watu walikuwa wanapata Bundle Bure Usiku let alone kulipia kitu - Sababu ya Ushindani; TCRA na Serikali ikalikoroga kwa kuleta bei Elekezi hivyo bila ushindani kila mtu anacheza mule mule - Kwanini mmoja atoe ndogo ili avutie wateja wakati kuna limit ya bei mmepangiwa kwamba hii ndio nzuri ?

Kwahio hata ikija Internet yenye gharama nafuu haitakuwa nafuu sababu serikali itataka ipate kodi kutokana na bei fulani elekezi (kumyonya mwananchi) Refer wanavyotaka kuchaji whatsapp calls, refer skype ilivyokuja Bongo ilikatazwa; refer kuna mtu alikuwa anatoa international calls kwa bei rahisi akafunguliwa Kesi kwamba ameikosesha Serikali mapato - Yaani angechaji bei kubwa mapato ni makubwa per unit (In short it has always been the case muharibifu ni serikali ila watu hawajui wanapeleka lawama pengine)

 
Back
Top Bottom