Azam FC mabingwa wa Kombe la Mapinduzi 2018 waifunga URA kwa penalti 4-3

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Azam FC imeibuka mshindi wa Kombe la Mapinduzi Cup 2018, baada ya kuifunga URA ya Uganda kwa mikwaju ya penalti 4-3 baada ya timu hizo kumaliza dakika 90 za mchezo bila kufungana. Azam inashinda kombe hili kwa mara ya pili mfululizo.

Mlinda mlango wa Azam FC, Razak Abalora amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa fainali hiyo ya Mapinduzi Cup kati ya Azam FC na URA FC, Razak amefanikiwa kuokoa mikwaju miwili ya penati.
 
Azam FC imeibuka mshindi wa Kombe la Mapinduzi 2018, baada ya kuifunga URA ya Uganda kwa penalti 4-3. Azam inashinda kombe hili kwa mara ya pili mfululizo.
[emoji122] [emoji122] [emoji122] [emoji122] hongera zao!
 
Heko Azam Kwa ubingwa mfupa uliomshinda Simba , Yanga akajidai anauweza kumbe hamna kitu mbwembwe tu
 
Kipa Razak wa Azam ni hodari sana. Nimeamini kuwa kipa wa Yanga bonge la shati, amejaa golini magoli yanapita tu.

U.R.A kuna Chirwa kibao, lakini Rostand kashindwa kuwa msaada.
 
Haya tena Azam FC.. Njoo kwenye VPL sasa
 
Hongera Lamba Lamba kwa kututoa kimasomaso [emoji120] [emoji120] [emoji122] [emoji122]
 
Halafu nawadharau sana wote mliokuwa mnaiangalia hiyo Fainali ya Mapinduzi kwani mnaonyesha kabisa kwamba Wote hamjui Mpira na hamna cha kufanya. Hivi Wewe una akili zako kamili utaacha kweli kwenda Kutongoza Mademu au Kubeti au Kumbaioloji Mkeo na ukakesha kuangalia Fainali ya ' Litimu ' libovu kabisa la Azam FC? Kwanza nasikia Referee kawaonea mno URA Kipindi cha Kwanza na naweza kusema kwamba Bingwa ni URA kutoka nchini Uganda sema tu Marefarii watakuwa walitishwa au walihongwa ili wafanye kila wawezalo Azam FC iwe Bingwa. Hakuna Timu ninazozichukia Tanzania kama Yanga na Azam na hivi karibuni nijiandaa pia kuanza kuichukia Timu ya Singida United.
 
Pole mkuu kwa denial
 
Kila MTU anastarehe yake Mkuu !!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…