Azam FC mabingwa wapya Kombe la ASFC baada ya kuichapa Lipuli FC 1-0 Uwanja wa Ilulu, Lindi

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Klabu ya Azam FC imetwaa Kombe la Shirikisho la Azam Sports Federation Cup, baada ya kuichapa Lipuli FC bao 1- 0 katika mchezo wa Fainali ulifanyika leo Juni 1, 2019 kwenye Uwanja wa Ilulu mkoani Lindi.

Iliwachukua Azam FC, hadi dakika 65' kipindi cha pili kupata bao lililowekwa kimiani na Obrey Chirwa.

Azam FC, imeweka rekodi ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Azam Sports Federation Cup kwa mara ya kwanza kihistoria ya klabu hiyo, hivyo kukata tiketi ya kuiwakilisha Tanzania Kimataifa kwa kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho la Afrika, (CAF CONFEDERATION CUP) msimu wa 2019/2020.

 
Simba SC kuwakilisha nchi Kimataifa Kombe la Mabingwa Afrika CCL

Azam FC kuwakilisha nchi Kimataifa Kombe la Shirikisho

Klabu moja wao wanawakilisha nchi Kimataifa kwa kuongoza ligi na kuongoza kusajili, halafu baadaye wanalalamika.
 
Vipi Mabingwa wa kihistoria wao wanawakilisha nini?
 
Makelele FC ktk ubora wetu kujiandaa tena kwa hamsa hamsa hadi tujilaumu kwanini tunabebwa badala ya kucheza mpira halali vpl [emoji16]
Simba SC kuwakilisha nchi Kimataifa Kombe la Mabingwa Afrika CCL

Azam FC kuwakilisha nchi Kimataifa Kombe la Shirikisho

Klabu moja wao wanawakilisha nchi Kimataifa kwa kuongoza ligi na kuongoza kusajili, halafu baadaye wanalalamika.
 
Nimeuona mpira ni kama waamuzi wamewabeba fulani hivi Azam.....lipuli offside 5 Azam offside 0..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…