Azam FC waichakaza Al Hilal

Soloma TV Online

Senior Member
Joined
Jun 26, 2023
Posts
104
Reaction score
291
Timu ya soka ya Azam FC yaanza Pre-season vizuri baada ya kuishushia kichapo cha mwizi wa kuku Al Hilal kwa magoli 3 - 0 huku FEI TOTO akirudi kwenye ubora wake baada ya kutoa assist ya goli.
 
Mashabiki wa Yanga ndo wanaongoza kuumia pale wakiondokewa na mchezaji.

Morison alipo ondoka Yanga waliumia sana, ikawa kila kitu anachofanya hata kiwe kizuri lazima wam dis!

Sasa hivi ni feisali, yaani hata afanye nini mashabiki wa Yanga lazima wamponde!

Inabidi mjifunze kuwa hawa wachezaji sio wenu milele, na hamna hatimiliki ya kumiliki mchezaji for the whole life!
 
Hili liko Kwa mashabiki dunia nzima Mkuu. Wachezaji wanaoondoka bila kuacha mahusiano mazuri na mashabiki huzomewa kote duniani na wengine hufikia Hadi kuchoma jezi yake. Luis Figo toka Barcelona kwenda Real Madrid ilibidi hata vyombo vyake apelekewe. Jana kulizuka habari zisizojulikana chanzo juu ya Mkataba wa Chama na kwamba anaondoka Simba Kwa vile si chaguo la Robertinho. Tazama maumivu waliyopata mashabiki wa Simba Kwa Muda mfupi. Jonas Mkude kaachwa na Simba na kapewa Kwa Heri, jezi No.20 ikastaafishwa Kwa heshima yake na akakaribishwa kuagwa siku ya Simba day, lakini tetesi za kutakiwa na baadaye kusajiliwa na hasimu wao huenda zikabadili neema yote aliyoahidiwa. Usishangae Mkude akawa mchezaji anayezomewa na mashabiki wa Simba na kushangiliwa Sana na mashabiki wa Yanga siku ya mechi Kati yao.
 
Itoshe tu kusema Yanga mmezidi.Mna tabia za kikekike Sana. Kwenu Kila mchezaji anaeondoka kama alikuwa muhimu kwenye kikosi chenu lazima mmuwekee vinyongo na visasi visivyo na Maana. Wakati mwingine mnaweka hadi ahadi za kuwaroga. Nakumbuka sakata la Nyionzima , Ajibu ,morison na sasa Feisal . Kwanini nyie tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…