Azam FC yaangukia pua Mkwakwani

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
Michezo miwili ya ligi kuu soka Tanzania bara imemalizika katika viwanja viwili tofauti.

Mchezo wa kwanza ambao ulipigwa saa 8 mchana, uliochezwa kati ya Kagera sugar dhidi ya Gwambina umemalizika kwa sare ya bao 1-1. Goli la Kagera sugar lilifungwa na Yusuph Mhilu dakika ya 6, baadaye Mashack Abraham kuisawazishia timu yake dakika ya 90+1

Kwa upande mwingine Azam fc amelazimishwa kichapo cha bao 2-1 na wagosi wa kaya Coastal union mchezo uliochezwa katika Dimba la mkwakwani huko Tanga. Magoli ya Coastal union yamefungwa na Haji Ugando dakika ya 9 na Hamad Rajab dakika ya 54, huku goli pekee la Azam likifungwa na Daniel Amoah dakika ya 36.
 
Hivi wale viongozi wa Azam waliosema Azam walistahili kuifunga Simba leo wanasemaje na yule Idd Nado aliyebahatisha goli akadai anawajulia mabeki wa Simba vp mabeki wa Coastal au wa Coastal ni mabeki bora kuliko wa Simba.
 
Huu ni ushamba katika soka ushabiki mandazi.
 
Azam ni sawa na Irene uwoya ,,anawabania wakubwa anampa dogo janja...sijui zaka zakazi atasema nn Tena..
 
Matokeo ya mpira yapo hivyo,uzaniae sie kumbe ndie.mpira una matokeo matatu.
 
Yule kipa wao mpya alidaka? Siku ile aliwakazia sana mikia!
 
Azam fc kakutana na mgonjwa wa kisukari mwaume wa Dar akatoa nao droo ila kaenda Tanga kakutana na wanaume wanaojua mapenzi kakojozwa
 
Kesho Timu ya Wananchi inajiongezea point zake tatu muhimu kwa vibonde Mbeya City. Wale washirikina wakirudi, wanakuta manyoya tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…