Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, mchana imemtangaza, Aristica Cioaba, kuwa kocha mkuu wa kikosi hicho.
Aristica Cioaba (45) anakuja Azam FC kurithi mikoba ya Mhispania Zeben Hernandez, aliyesitishiwa mkataba pamoja na bechi lake zima la ufundi
Kocha huyo kutoka nchini Romania amesaini mkataba wa mwanzo wa miezi sita na Azam FC, atasaidiana na makocha Wazawahttps://www.jamiiforums.com/mobile-gallery/2aedb0a9a6e0f653cb230743dab9504c.jpg[/IMG
Aristica ametokea Aduana stars ya Ghana walikotoka wachezaji Yakub Mohamed na Mohamed Yahya waliojiunga na Azam mwezi Desemba mwaka jana.
Unasema MCHANA HUU, afu uzi ndio kwanza una dk 20 tu. Btw bravo Azam, taarifa iliotoka inasema kocha hajapata vibali vya kufanyia kazi bado, so ataanza kazi ktk VPL, huko zenji na yeye ni mtazamaji kama Mimi.