AZAM HD CUP kuendelea leo...

Mphamvu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
10,702
Reaction score
3,319
Michuano ya Kombe la Shirikisho (AzamHD Federation Cup) inatarajiwa kuendelea leo katika viwanja vinne tofauti nchini, ambapo kila timu inahitaji kupata ushindi ili kusonga mbele katika mzunguko wa pili utakaochezwa mwezi Disemba mwaka huu.



Jijini Mbeya wenyeji Mbeya Warriors watakuwa wenyeji wa Wenda FC mchezo utakaochezwa uwanja wa Sokoine jijini humo, huku katika uwanja wa Majimaji mjini Songera timu ya Mighty Elephant watakua wenyeji wa African Wanderes.

Kariakoo ya Lindi watawakaribisha Changanyikeni FC katika uwanja wa Ilulu, huku timu ya Sabasaba ya mjini Morogoro wakiwakaribisha jirani zao Mkamba Rangers katika uwanja wa Jamhuri.

Michuano hiyo itaendelea kesho Jumatano kwa michezo miwili, Polisi Morogoro watawakaribisha Green Warriors uwanja wa Jamhuri mjini humo, huku timu ya Mshikamano FC wakiwa wenyeji wa Cosmopolitan katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Katika michezo iliyochezwa jana, Abajalo ilibuka na ushindi wa mabao 5 ? 1 dhidi ya Transit Camp, huku Pamba FC ya jijini Mwanza ikiibuka na ushindi wa bao 1- 10 dhidi ya Bulyankulu FC ya mkoani Shinyanga.

Chanzo; Shirikisho la Soka Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…