Azam Media kuwazidi kete DStv?

Ila sio kuzidi investment ya DSTV katika tasnia ya habari hasa za michezo.
wale wame invest million of dollars na sio madafu ya Tsh. aliyoweka AZAM TV.

Mkuu, najizuia kukutafutia jina. Awali ya yote ukiwa nchi yoyote hapa africa (Lesotho, Camerron, Congo, Kenya, Uganda nk) ukikuta wananchi wa huko wanaangalia AZAMTV ni hakika wewe kama Mtanzania itakupa furaha kuliko kukuta wanaangalia kina DS--------TV. Labda tuuuuuu kama Utanzania wako umekaribia "expiry date".

Pili NANI aliwapa DS------TV mamlaka ya kuonyesha EPL kwa Sub-Saharan Africa? Hii ni nchi ipi? Huu ni mwendelezo wa Berlin Conference na ukoloni mamboleo. Zinduka!!!!! Huu ugawaji wa HAKI-ulizihusisha nchi zilizopo eneo linaloitwa Sub-Sharan Africa? Mababu zao kina DS......TV waligawa na kujitwalia maeneo yetu kama njugu bila kujali nani wapo wapi! Sisi ndio tumewalisha raslimali zetu tangu enzi na enzi.

Ushabiki naouona kwa baadhi yetu na mahaba kwa wanyonyaji hawa hauna tofauti na wale machifu waliopewa kioo cha kujitazama na kurudisha fadhila kwa kugawa maeneo ya ardhi.

Ipo mipira mingi tuu Azamtv na sijaona kama ina-standard ya chini kuliko ya EPL. Kisha jiulize iliwachukua DS/TV muda gani hadi kushusha BEI tena kwa kuwalenga wa TZ? Nani kawafanya washuke bei? Kwani hawataki faida? Wema wa ghafla hivi unatoka wapi?
 
Mie natumia Azam na nawapongeza kwa hatua hiyo ila kazi bado in kubwa,nawashauri waoneshe ligi fulani kati ya zile 3 kubwa za Ulaya walau watuoneshe hata moja alafu kwa Africa waoneshe na ile ya Ghana na ama Congo DRC walau zina mvuto

Ni kweli. Ila kazi ni ndefu kwa sababu kwa sasa lazima wazinasue nchi moja baada ya zingine kutoka kwenye mikataba waliyoingia na warusha TV wengine. Ila kwa kasi waliyonayo dhidi ya umri wao, napata hisia kuwa kwa mara ya kwanza DSTV wamepata washindani makini. Kina Ds/TV, na wengine wote wanajua vizuri sana kitisho hiki na ndio maana ya hii haraka ya kushusha bei zao. Mbele ya safari usishangae hiyo EPL kuiangalia kwa bei ya kutupa.
 
DSTV wapo mbali kidogo ila taratibu wakikimbizwa watakutwa tu...
 
azam kuonesha mpira sio lazima ampiku dstv anaweza tu kuchukua hata asilimia 20% ya haki hio akawa anaonesha mechi 2 kwa wiki kama kipindi kile cha dstv na gtv sport.
 
hivi nyinyi mliochangia mada hii nani mwenye dstv nyumbani kwake au mnaisikia tu kwa kuonyesha mipira azamtv kwachanel hamfiki dstv hata kwa ncha ya ukucha
 
hivi nyinyi mliochangia mada hii nani mwenye dstv nyumbani kwake au mnaisikia tu kwa kuonyesha mipira azamtv kwachanel hamfiki dstv hata kwa ncha ya ukucha

dstv hamiliki ligi ya uingereza bali chama cha mpira cha uingereza fa ndio wenye mamlaka haya.

kama azam ataweza kumzidi dau dstv inawezekana kabisa 100% kuonyesha.

ngoja nikupe mfano hai kabisa ambao umetokea, nchi za kiarabu aliekua na tenda ya kuonyesha ligi ya uingereza ni abudhabi sport kwa muda mrefu, jamaa hawa wa aljazeera wakapanda dau na kushinda wao haki za kuonyesha hivyo wakapokonywa abudhabi wakapewa aljazeera.

dstv hata wawe na chanell elfu 1 za maana, azam akitimiza vigezo vyote kumzidi dstv basi fa watawapa azam epl
 
ana chuki zake nyingine tu huyu hadi anapindisha ukweli. yaani ligi za afrika ziizidi EPL? au tm EPL zinazidiwa na nyingine za ulaya????
 
niulize swali wadau. iv azam tv wana network gani kubwa hapa afrika hadi mdiriki kufikir kuwa wanaweza kuipiku dstv? wako south, nigeria, ghana, angola nk? wanaweza lakn miaka mingi ijayo na kama dstv watalala ucngiz. ivi mnafikir kama FA wanalipwa $20m na dstv kuonesha epl kwn sabsahara afrika, basi azam wakipeleka $25m basi fasta FA watawapa tender azam? kuna vigezo vingi siyo bei tu wadau. hii ni kama tenda ya ujenzi au nyngnezo. all in all azam wanajitahd ukilinganisha na wengine wa hapa tz lakn msiwape kichwa sana kuliko uwezo wao. nawapa big up azam tv lakn wakaze buti
 

Sijaelewa mkuu, kwani tenda ya kuonesha EPL mpaka ipewe kampuni moja tu? DSTV si wanaweza kuendelea kuonesha na Azam na wenyewe wakapewa haki ya kuonesha:what:
 
Sijaelewa mkuu, kwani tenda ya kuonesha EPL mpaka ipewe kampuni moja tu? DSTV si wanaweza kuendelea kuonesha na Azam na wenyewe wakapewa haki ya kuonesha:what:

Shukran sana kwa swali lako. Ndio maana nimeuliza; ALIYEJIMEGEA NCHI INAYOITWA SUB SAHARAN AFRICA NI NANI? Hiyo nchi ni ipi na makao yake makuu ni wapi?
 
Sijaelewa mkuu, kwani tenda ya kuonesha EPL mpaka ipewe kampuni moja tu? DSTV si wanaweza kuendelea kuonesha na Azam na wenyewe wakapewa haki ya kuonesha:what:

yap inapewa kampuni moja na kama zitapewa kampuni mbili basi wanagawana mechi, kila kampuni itaonesha mechi zake na hawaruhusiwi kuonyesha zote kwa pamoja. sababu za kufanya hivyo wanazo wenyewe FA si jukumu langu kuwajibia.
 

nakubaliana na wewe 100% azam hana coverage ya kupewa hii tenda, lakini tujiulize swali je gtv alikua na coverage kumshinda dstv? jibu ni hapana hakuwa na coverage kubwa kumshinda dstv na watu walilazimika kununua madish 2 ili waone epl yote. kivipi gtv walifanikiwa? jamaa walifanikiwa sababu walikuwa wanatoza hela ndogo.

imagine azam anaonesha epl kwa charge hii hii ya 12,000 au akaongeza ikawa 15,000 hadi 20,000 unafikiri nchi kama kenya, uganda, nigeria watashindwa kununua azam tv kwa bei ndogo hivyo? coverage itapatikana ndani ya miezi tu. mabanda yote ya tv watainunua.
 

Naapa kuthibitisha sentensi yako ya mwisho ni kweli tena ni kweli tupu.
au ni mwanangu tuekwenda kuangalia soka mbali na nyumbani kwa sababu ya family democracy
 

Kwenye biashara watu wanaojua hawahangaiki na jinsi unavyoanza, wanacheki mipangilio yako ya mbele, dstv.
kwa sasa dstv wanaweza wasitishwe sana na azam ila kibiashara pengine wakichungulia miaka kadhaa mbele na trend ya azam wanaona kitisho halisi. Hiyo ndio market control strategy
 
Nadhani kunakitu hakijawa sahihi hapa. Watu hawataki kufanya utafiti kabla hawajaleta taarifa ambazo hazina ukweli wa kitaalamu.
Miaka 8 iliopita pale Nigeria kuna local tv yaitwa Htv ....hii ndio ilipata exclusive rights za kurusha epl kwa miaka mitatu kwa Nigeria tu. Dstv walihangaika sana maana soko la Naiga ni kubwa na middle class ni wengi. Hata hivyo Htv walititiniwa tena na multichoice.
Hivyo basi Azam anaweza in tye coming years kupata hii kitu atleast kwa Tz. Tusubiri.
BTW yule CEO wa azam ndo mastermind na ndiye alikuwa market strategist wa GTV.
 
idoyo, kama kuna wakati mtu ametumia intellect kumjibu mwingine huu ni mfano mzuri sana. Ilishaniboa alivyomnanga mtoa mada. He was rude to say the least. Strangely mtoa mada alionyesha uungwana mkubwa na hakumrudishia insults. Ur Congrats.

cc mtu chake,
 
Last edited by a moderator:
....ahsante mkuu....ujue watu wengine ni kuwaacha tu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…