Azam tunapenda muwe mnatuonesha matukio ya kimichezo ya live mbali na soka k.v. Marathoni na Jogging

Azam tunapenda muwe mnatuonesha matukio ya kimichezo ya live mbali na soka k.v. Marathoni na Jogging

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Nikiangalia televisheni za wenzetu za michezo hasa za super sport wenzetu huonyesha Marathon mbalimbali kwenye miji lakini hapa kwetu Azam kupitia chaneli zake imekuwa ikijikita zaidi kwenye soka na kidogo siku za karibuni wamekuwa wakituonyesha masumbwi.

USHAURI WANGU KWENU
Hizi jogging na Marathon zinazofanyika kwenye miji mbalimbali hapa kwetu Tanzania nashauri muwaze kuzirusha live ili kuhamasisha michezo miongoni mwa jamii zetu. Aidha nawaza mnaweza kuwasiliana na waratibu wa matukio haya ili kupata sponsors na hii ikawa fursa mpya ya biashara lakini yenye manufaa kwa jamii yetu.

Aidha wekeni utaratibu wa kutuonyesha live matukio kama mbio za magari zinazofanyika kila mara huko Arusha Kilimanjaro, Mwanza, Iringa na kwingineko. Pia tumekuwa na michezo ya mbio za Baiskeli kule Mwanza tunaomba muyaweke kwenye programu ya kutuonyesha live itafaa sana. Hizi ni fursa zitumieni mtupe raha.
------
Kwani hii dunia ni yetu?
 
Umetusahau sisi wacheza pooltable mkuu. Mashindano ya pooltable, dart tukumbukwee piaa
 
Kwanini bongo hamna mashindano ya tennis na kuogelea?
 
Nashangaa. Sisi wengine kuogelea ndio michezo yetu.
 
Nje ya mada. Hivi ligi daraja la kwanza hairushwi?
 
Hata hiyo boxing ni msimu tu. Upepo ukipita hutaiona tena.
Na kuongezea hata mprira watangazaji hata kama timu hamuipendi onyesheni professional yenu siyo hiki mnachofanya kushabikia badala ya kutangaza. Mbaya zaidi hata matukio mtu wa kuchanganya picha inapotokea kurudia tukio labda ni adhabu ,inaonyesha kabisa kuna upendeleo fulani kwani kuna timu ambayo huwa ikichezewa rafu hamuonyeshi marudio ila ngoja yenyewe icheze rafu mnarudia kila upande na kamera zenu.Mwisho kabisa hizi bei mlizotangaza hakuna mapunguzo yoyote mmeongeza kinyemela maana unapunguza bei huku unapunguza vipindi huu ni ujanja ujanja
 
Back
Top Bottom