Sielewi kwa nini mmeihusisha AZAM na sasa SIMBA kwa issue ya huyo dogo wakati hamna kiongozi hata mshabiki wa timu hizo aliyeonyesha kuwa anamtaka sana. Inawezekana ni kweli ndiyo timu zinazomtaka ila bila uthibitisho wowote, huku ni kujionyesha tu kuwa hamjiamini na mna wasiwasi na washindani wenu.
Nakumbuka zilipoanza fununu kuwa amepata timu nje, mashabiki wengi wa Yanga walionekana kupata ahueni, wakidai, afadhali aende nje maana kwenda AZAM ni kurudi nyuma, hahah.