"Tumepata athari ya kifedha baada ya mchezo (dhidi ya Simba Sc) kusogezwa mbele, kwa sababu mchezo kama ungechezwa tarehe 6 kama ilivyopangwa basi tarehe 7 tungerudi na hivyo watu wangepumzika na kusingekuwa na haja ya watu kukaa kambini kuwahudumia."
"Lakini wametuongezea siku moja mbele ambayo sisi haikuwepo kwenye ratiba, hivyo muda wa maandalizi na kukaa kambini umeongezeka, na hivyo tumepata hasara kutokana na kuwahudumia watu siku hiyo wakiwa kambini," amesema Zakazakazi Afisa habari wa klabu ya Azam FC