Azamtv mnatutesa wadau wenu tulio nje ya nchi

SPINE

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2017
Posts
1,068
Reaction score
1,150
Imepita muda sasa Azamtv kupitia online app yenu mmeitoa channel ya azamsport, hivi karibuni pia mmeitoa ZBC2. Kwa kweli mnaumiza walio nje ya nchi maana ndio mlikuwa faraja yetu hasa kwa wapenzi wa ligi ya nyumbani hata mechi za kimataifa kwa klabu zetu pendwa na timu yetu ya taifa.

Kuna kipindi nilisikia kuwa hamkuwa na kibali cha kurusha hizo channel nje ya nchi, mkasema mtashughulikia lakini kimya mpaka leo. Nadhani mnatakiwa kuongeza jitihada maana mlifika level ya juu kuliko ving'amuzi vingi Tanzania kwa kupatikana duniani bila chenga .
 
Binafsi wameniboa ,kabla ya kutaka watu walipie walitakiwa wahakikishe uhakika matangazo yao kutokatika au kupotea inapotekea mchezo muhimu
 
Bora mkuu umeanzisha thd kuhusu hii issue,huenda ikapatiwa ufumbuzi,nami pia nilikua naitegemea sana Azam app kuona baadhi ya mechi za ligi ya bongo.
 
Binafsi wameniboa ,kabla ya kutaka watu walipie walitakiwa wahakikishe uhakika matangazo yao kutokatika au kupotea inapotekea mchezo muhimu
Hiyo issue ya kukatika mawasiliano kwenye mechi muhimu nahisi ni mbinu ya kibiashara😅
 
azam tv siku hiz wanazingua sana

Sent usingJamii Forums mobile app
 
Gomgolamboto ndiyo nje ya Nchi?
Wewe bado unaishi kwenye fikra za kuamini mtu kua nje ya nchi ni jambo kubwa sana na ni ajabu? dunia ilishabadilika,kama umekata tamaa na kuona mtu kua nje ni kama miujiza utakua unajiongopea mwenyewe tu,njoo tutengeneze dollars huku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…