Azizi Ki: Kocha Rulani Mokwena alinifuata na kuniambia wewe ni mchezaji mkubwa sana na una kila sifa. Una nguvu na una umiliki mzuri wa mpira miguuni

Kurunzi

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2009
Posts
9,753
Reaction score
10,747
“Kocha Rulani Mokwena alinifuata na kuniambia wewe ni mchezaji mkubwa sana na una kila sifa. Una nguvu na una umiliki mzuri wa mpira miguuni mwako,akanishauri niongeze uharaka eneo la ushambuliaji ili kuwa bora zaidi."

"Amenisisitiza kufanya hivyo akiamini kuwa pia naweza na nitakuwa bora zaidi kwa kuwa na namba nzuri ya ufungaji na hili nitalifanyia kazi”

©️ Stephane Aziz Ki
 
Aziz Ki aliwaka sana wala siyo siri. Alichoambiwa ni kweli kabisa, ana sekunde fulani chache za kuchelewa kufanya maamuzi ingawa uzuri wake akishayafanya hayo maamuzi mara nyingi yanakuwaga sahihi.

Aliyemshauri aache kupandisha bukta yake alimpa ushauri bora sana. Nadhani ndiye mchezaji bora wa NBC msimu huu.
 
Ko
Aziz Ki aliwaka sana wala siyo siri. Alichoambiwa ni kweli kabisa, ana sekunde fulani chache za kuchelewa kufanya maamuzi ingawa uzuri wake akishayafanya hayo maamuzi mara nyingi yanakuwaga sahihi.

Nadhani ndiye mchezaji bora wa NBC msimu huu.
Kolokwinyo watabisha
 
Mchezaji bora asiyekuwepo nusu fainali ni sawa na debe tupu lisilokuwa na unga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…