KERO Baa ya Ellis (Morogoro) imerejea tabia ya kupiga kelele usiku kucha, Serikali ichunguze kinachofanyika usiku

KERO Baa ya Ellis (Morogoro) imerejea tabia ya kupiga kelele usiku kucha, Serikali ichunguze kinachofanyika usiku

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Wapangaji wa Shirika la Nyumba zilizopo karibu na Manispaa ya Morogoro tunalalamika bar maarufu ya Ellis iliyopo karibu na Ofisi za Manispaa ya Morogoro, inapiga kupiga mziki mkubwa hadi asubuhi hali ambayo ni kero kubwa kwetu.

Sisi Wapangaji baadhi ni Viongozi na Watumishi wa Umma tuliwasilisha malalamiko yetu kwa kwa NEMC, siku za nyuma na yalifanyiwa kazi lakini kwa sasa changamoto hiyo imerejea tena, tunaomba Serikali kuingilia kati.

Inawezekana kuna mkubwa yupo nyuma ya hiyo bar na ndio maana wahusika wamekuwa wakivunja Sheria mara kwa mara na hakuna hatua zinazo chukuliwa ikizingatiwa kuwa jirani na ofisi za umma.

Nyakati za usiku kuna wakina dada wanaojiuza lakini pia wapo wanaume mashoga ambao hapo ndio kama eneo lao maarufu la kukutana na wateja wao.

Ushauri.
Ni vizuri biashara zinazoendelea hapo zikafuatiliwa kwa ukaribu kwakuwa eneo hilo lipo karibu na ofisi za umma haitapendeza kuona biashara ya ngono zikifanyika katika eneo hilo.

Pia Manispaa ya Morogoro ni vizuri ikaweka taa zenye mwanga mkali katika eneo lote la uzio ili kuondoa giza katika eneo hilo kuzuia kuwepo kwa biashara yoyote.

Ufafanuzi wa NEMC ~ NEMC: Tunachunguza madai ya Baa ya Ellis kuwa imekuwa kero kwa majirani kutokana na kelele za muziki
 
Acha roho mbaya.
Acha kupangia watu maisha.
We ingia chumbani kwako
Lala ya nje yasikuumize.

Watu wasile bia ati wakuache ulale
 
Niko hapa Terminal pub, ndiyo nataka nitoke hapa nielekee hapo Elis
 
Umesema baadhi yenu ni viongozi na watumishi hivyo ni wazi mnazijua vizuri sana sheria za nchi, mpelekeni mahakamani mara moja huyo mmiliki. Hii nchi tatizo kubwa ni kuchekeana na kuchukuliana poa wakati sheria na mahakama zipo.
 
Elii's bar ya hovyo sana nadhani mamlaka za manispaa ya huo mji wenu wa kijinga watakuwa mashoga, hio sehemu inapaswa kuwa ni mgahawa na sio club ya usiku.

Huku Dodoma hakuna ujinga wa namna.

Morogoro ndio makao makuu ya mashoga
 
Back
Top Bottom