macho_mdiliko
Platinum Member
- Mar 10, 2008
- 25,191
- 48,765
Umeandika mengi lakini sijaona point yako:Wewe kweli macho mdiliko kama jina lako linavyosema,
Nimesoma vizuri na kuelewa vizuri, na ndio maana nikatoa ushauri/mtazamo wangu kwa hicho chama, ili hata kama chama kikimpa adhabu Wema basi iwe kisheria, na asiwe na uwezo wa kukata rufaa mahakamani na mahakama kuweza kutengua hukumu kwa kigezo wametoa hukumu bila ya kufata sheria....
Kwanza tambua kitendo cha chama kuomba mamlaka husika kukataa kupokea utetezi wake ni kosa kisheria, tena ni kosa ambalo linapingana na katiba ya nchi. Hakuna mtu/mamlaka ambayo inauwezo wa kukataa ushahidi wa mshtakiwa. Inapaswa ipokeee na itolee maelezo sababu ya kukataa kuutumia katika hukumu itakayo toa (yani mfano wangesema "tumepokea utetezi kuwa Wema alivyokataa kuitikia wito wa kuja kwenye baraza la chama kusikiliza mashtaka yake alisema hakuwa nchini, ila ushahidi unaonesha alikuwepo nchini na amedharau makusudi, hivyo tunakataa utetezi huo).
NB Hio kauli tu inauwezo wa kumsababishia Wema akakata rufaa mahakamani, na mahakama ikatengua adhabu zote alizopewa.
Pili, hata kama chama kilifanya juhudi za kumtafuta na kushindwa kumpata, wanapaswa kutumia kigezo hicho wakimpata ajitetee kwanini hakuitikia wito kwanza, halafu ajitetee kwanini amesambaza video ambayo anajua ni kinyume na sheria za nchi. Halafu ndio watoe hukumu.
Tatu, mimi natamani afungiwe hata maisha asijishughulishe na maswala ya filamu kwasababu amejisahau kua yeye ni kioo cha jamii, na anapaswa kua mfano mzuri kwa mashabiki pamoja na chama cha filamu nchini. Na si kua mfano mbaya kwa mashabiki zake pamoja na chama cha filamu.
Nne, usipende kuropoka mambo ambayo akili yako haina uwezo wa kuchanganua/kuelewa na wala si size ya upeo wako wa kiakili. Uliza kistaarabu uelimishwe
1. Chama kinasema kilimtumie wito akadanganya yupo nje ya nchi. Kama alidharau unataka wampigie magoti? Kwanini hakwenda kujitetea kama ana huo utetezi?
2. Chama kimesema utetezi aliotoa usikubalike kwani hauna mashiko. ie. anasema ni utoto ulimponza na hatarudia tena wakati alishaonywa siku za nyuma na tena ni serial offender aliyepatikana na hatia ya kumiliki msokoto wa bangi!
Ule wakati wa kubembelezana ulishapita na upepo wa Kikwete. Omba Mungu wakati urudi nyuma na hoja yako itakuwa na kazi.