Baada ya Kufanyiwa LEEP, ameingia Hedhi,ila Damu inatoka nyingi sana.

Mkuu upo sahihi kabisa.Baada ya hii Operesheni nimejifunza kitu aiseee na ningependa na wengine wawe na mtizamo wako.Kama ishu siyo ya Emergency ni vizuri kufanya consultancy nyingi Kwa kadili inavyowezekana. Nilisikitika sana baada ya kuona Specialist mwingine akisema kuwa Mgonjwa hakutakiwa kufanyiwa hii Operesheni.Na vipimo alivyokuwa anafanyiwa Wala havikuwa necessary maana Kipimo cha kwanza kilishatoa majibu hasi hivyo hakukuwa na haja ya kung'ang'ania vipimo vya Aina hiyo.Badala yake ilibidi kupima vipimo vingine ili kujua tiba ya kutoa.Nimejifunza kitu aiseee
 

Wote tunajifunza kupitia makosa au mambo tunayokabiliana nayo maishani. Naamini atakaa sawa, na hakutakua na madhara makubwa kidonda kikipona vizuri. Mgonjwa anaendeleaje? Ni maombi yetu apone upesi
 
Wote tunajifunza kupitia makosa au mambo tunayokabiliana nayo maishani. Naamini atakaa sawa, na hakutakua na madhara makubwa kidonda kikipona vizuri. Mgonjwa anaendeleaje? Ni maombi yetu apone upesi
Mgonjwa anaendelea vizuri ile damu haitoki imekata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…