Baada ya kuhudumia mtoto nimegundua sio damu yangu. Nimuoe huyu mwanamke nilee mtoto asiye wangu au nimuache?

We jamaa yaani unauliza uoe huyo mwanamke au lah!!!?...yaani wewe mwenyewe umekosa jibu!??..mbona majibu yako wazi...ulishafanya makosa ya kiufundi toka awali,halafu unataka ufanye kosa lingine kubwa...

Aisee kuna watu mna mioyo!
 
Tatizo Baba wa Mtoto OG yupo,na anamtambua Mtoto wake,kutakua na mvutano hapo na watamchanganya Mtoto asijuwe Baba ni yupi kati yao!!!
 
Tatizo Baba wa Mtoto OG yupo,na anamtambua Mtoto wake,kutakua na mvutano hapo na watamchanganya Mtoto asijuwe Baba ni yupi kati yao!!!
Baba OG hakumkataa mtoto? Sasa huyu mama alibambika au? Hapo kuna mtihani. Wakae chini wazazi waangalie namna ya kumlea mtoto. .
 
Pole nyingi sana kwake, kwa kifupi tu aachane na huyo Mwanamke atafute Mpenzi mwingine Wanawake wapo wengi sana.
 
Hapo hupendwi kibaya zaidi kaona wew ni wakukuchuna ndo maana akakupa na mtoto anaejua sio wako umuhudumie baba wa mtoto ni wakula raha tu

Kheri kuvunja uchumba kuliko hiyo ndoa unayotaka kuingia itakugharimu Sana..
 
Huyo jamaa usiyekua na mawasiliano naye wala kutomfahamu uliona amempost wapi huyo mtoto?
 
Sasa atakuwaje mtoto wake wakati baba halisi yupo na anamtunza na kumpost juu. Angekuwa baba yake hayupo hapo sawa. Usimpotoshe huyo kijana. Hapo inabidi aachane tu na huyo binti kwa kuwa ameshadanganywa na pia aligeuzwa kitega uchumi kwa kubebeshwa majukumu ya kulea na kuhudumia mtoto asiye wake. Binti hampendi jamaa na ndio maana amemdanganya na asingegundua mwenyewe angadanganywa milele

Ushauri wangu kwa mtoa mada aachane na huyo binti muongo na Mungu atampa mwanamwali asiye na makando kando wafunge ndoa. Kuhusu huyo mtoto si damu yake na ukute hata hilo jina la mama yake alilotoa analijua yeye tu na pia ni kama kumpa mtoto wa mtaani jina la mama yako maana alitamfanya kuwa wa kwako.

Unachunwa na kahaba halafu unataka kulioa kabisa baada ya kugundua kuwa ni liongo, tapeli na dangaji
 
Mambo kama hayo yanapotokea kwa wanandoa huwa ni vigumu kuachana kwa kuwa mara nyingi huwa tayari wana watoto wngine. Kwa huyu ambaye ilikuwa ni matarajio tu sioni shida iko wapi - muache tu tafuta mwingine ile usifanye haraka sana , Tuliza kwanza kichwa chako endelea na mishe mishe zako kwanza.
Ukiona akili yako imeshatulia then tafuta mwingine. Kuhusu mtoto, huyu hana hatia yoyote, hajui lkilichotokea, msaidie kadri utakavyoombwa kumsaidia. Kuna siku huyu mtoto akishakua anaweza kuuliza chanzo cha jina lake (au walimwengu watamweleza kisa chote), kama utakuwa unaendelea kumsaidia basi anaweza kuwa msaada kawako baadae.
Inwezekana pia huyo baba wa mtoto wasioane - walikuwa wanafanya kama wengi wafanyavyo wakiwa vyuoni na wakadanganyana mengi. Yote ni mitihani.
Ikifikia hatua anataka mrudiane muoane - pima sababu za kurudiana, jipime na wewe mwenyewe - inawezekana umeshafanya hivyo kwa wengine pia!
Mwanangu, maisha ni mtihani lakini kwa sasa - muache tu na tuliza akili usikurupuke, yajayo......!
 
1. Mchumba hasomeshwi
2. Usitafute sifa ukweni, issue ya kuingilia majukumu ya ada ni kutakaa kujionesha wewe unaweza tunza mtoto wao na imekucost sasa.

Hizi nyuzi mkuu hukuzionq kweli au zimefunguliwa too late.
Hao mabinti ndio sababu za wadada wengi kupigwa shaba hivi karibuni.

Pia mkuu ina maana hata mashangazi walishindwa kutambua damu yao kweli, mkiambiwa mtoto akijifungua apelekwe kwa familia ya baba wacheki kama ni damu yao hatusikiii.

Pole sana jomba, hio hesabu ni irrecoverable debt, piga moyo konde ulifanya accounting for non profit organizations [emoji28]
 
Sasa ushauri utamfikia vipi huyo mwenye hicho kisa?
 
Wewe anonymous wa Kigoma wewe!

Utaoa "hata bure" mwanamke asiyekupenda, laghai na saliti?

Wanaume "kabila yako" mnatuangusha sana wanaume ujue, ningelikuwa ni kaka yako ningelikuzindua akili zako kwa fimbo!

Kwa tafsiri isiyo rasmi:"ndoa ni mkataba halali wa hiari wa kuishi pamoja kati ya bibi na bwana wapendanao" period

Kama kati yenu mmoja wapo upendo haupo, ndoa hapo haipo pia.

Mwanamke laghai, kakusaliti bado unawaza kuishi naye eti kisa ba'mkwe anakupenda, nyie vijana nyie, mnakwama wapi!

Kaa naye mbali huyo ibilisi, muda, hisia na mali alizokupotezea vinatosha.

Wewe bado ni mdogo, hajakuingiza chaka ukapotea mazima, geuka ujipange upya, aangukaye husimama tena.

Haya makosa yanayojirudia kwa wanaume kusomesha ama kulea wachumba kabla ya ndoa yanawagharimu wengi, lakini hamsikii kama sikio la kufa.

Ifike sehemu sasa, tuheshimu kufuata mila na tamaduni zetu zinazoongoza njia sahihi za kutafuta mchumba na kufunga ndoa.

Haya mambo ya utamaduni wa kizungu, kumuita mwanamke "mchumba" huku unamlala na hadi kuzaa naye kabla ya ndoa ni uzinzi kama ulivyo uzinzi mwingine na ni laana.

Umri wako "umeiva" tafuta msichana fresh, asiye na makando kando na kashifa za kimapenzi, mwenye haiba ya uaminifu na mcha Mungu ili uoe utulie na Mungu atakubariki.

Achana na hilo gume gume lisilokutakia mema wala kuuthamini upendo wako kwake pamoja na kujitoa kwako kwa hali na mali.

Sasa siyo uende tena kwa huyo hawara yako akakuweke kwenye kinena ukaanze kulia kipindi ukifanya mapenzi na kututukanisha wana Jf wote washauri!

Utasikia ukiambiwa: "kama unanipenda, nitukanie wana Jf wote walio kushauri kuniacha".

Kwa kuwa bado unamfia, nawe utasikika ukigugumia huku ukisimamia ukucha: "kum... kum...zenu wana jf mlionishauri nim... nimmmmm'iiiii, chozi!

Isee, tukikugundua!
 
Sikutaka akose chochote, hata wazazi wake walipopungukiwa kwenye ada, mimi niliongezea pale wazee walipopungukiwa[emoji848][emoji2827]
 
Kwa bahati nzuri alijifungua mwezi wa kwanza baada ya kuhitimu chuo! [emoji1541]
Hapo ndipo penye kiini cha tatizo
 
Angalia ustaarabu wako kaka sio muaminifu huyo mwanamke
 
Tumbi au?
Siyo Uhazili kweli!

Wamepabadili jina wanapaita "Chuo cha utumishi wa umma".

Maana chuo hicho kuanzia wakufunzi wake maadili sifuri kabisa.

Kuna rafiki yangu mjeshi mmoja sasaiv ni marehemu, alisomesha mwanamke akaajiriwa pale.

Kifupi, waliishi pamoja "kotaz" za chuoni pale na mwisho wa siku yule mjeshi alifurushwa na huyo mwanamke kwa kutupiwa vibegi vyake nje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…