Baada ya kuitembelea stendi ya Magufuli iliyotajwa na CAG kuwa itasababisha foleni

Japo mimi siyo mhandisi ila ushauri wangu wangeiga kidogo modernity ya stand ya Dodoma pia kivuko kwenda stand ndogo wangeweka subway.
Wanaweka daraja la juu kwenda kituo cha daladala mbezi, sio mbaya! Subways zina gharama zaidi kwa mazingira yetu...
 
Cc;@kangi lugola
Asome akiwa anamtaja Magufuli kwa sauti
 
Pamoja na uzuri na ubora wa kituo hiki lkn jambo la msingi ifahamike kuwa ni miongoni mwa chanzo kikubwa cha mapato ya Serikali hivyo mamlaka husika zinapaswa zikitunze na kukiboresha zaidi.
endapo mazingira yataboredhwa zaidi basi mapato ya serikali yataongezeka mara dufu.
abiria wa kigeni wanao fika maeneo hayo wanatamani kufanya manunuzi ktk maeneo hayo, hoteli za kisasa n.k.
mamlaka zinapaswa zidhibiti upigaji kama ilivyo jitokeza ktk soko la kkoo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanaoharibu hii nchi ni
1. Uvccm
2. Maafsa wanaokula rushwa
3.........
4.......
Malzia mwenyewe
 
Kweli kabisa mkuu, yaani mtoto wa Dada ndo anashika mfuko mkuu halafu tuseme huyo mtu alikuwa na nia njema na hela zetu?
 
stend sio shida! shida ni watu wanavuka kwenda stend ndogo ya daladala wanasababisha foleni

badala ya kujenga flyover ya magari wamejenga daraja la wavuka miguu! shida
Na asubuhi wakati wa kutoka magari unakuta msululu wa maroli yaani yanasimamishwa then ndio mabasi yatoke ilitakiwa kubuniwa njia ya juu pale ikaunganishwa ma Morogoro road
 
ili kuendelea kulinda legacy yake, tuletee na picha za traffic lights za chato pia
 
Kikwete hakujenga airport Msoga..
Hapa tungejua kama lile mansion pale Msoga limejengwa kwa ile pesa iliyosemwa na BBC kuwa ilikopwa mwaka wa mwisho ila haikuingia serikalini ambayo kimsingi ni sawa na bajeti ya Stieglers.

Inawezekana hawakujenga hizo port(Sina hakika ile inayotakiwa kule Bagamoyo kama haina mkono wa mmoja wao), ila kuna mabiashara mengi tunasikia kuwa ni yao kwa majina ama ya waarabu au wafanyabiashara wengine, achilia mbali tunayosikia kuwa ni ma-tycoon wa mambo haramu kabisaaa.

Ni bora miradi inayofanyika na kukamilika hata kama kuna upigaji, kuliko miradi inayokufa ilhali pesa yote imetoka na hakuna yeyote wa kufanya lolote.
 
E

Point yangu haikua kumtetea hata mmoja ubadhirifu uliotokea kipindi cha Kikwete ni mkubwa hakuna asiyelijua hilo mfano Meremeta, Kagoda, IPTL,Dowans n.k

Je wananchi tuliwezaje kuyajua hayo? Jibu ni moja uhuru wa vyombo vya habari ulikua mkubwa japo sio kwa 100% ( kila kitu kutajwa)

Je ukija utawala wa Jiwe Unaziamini vipi takwimu na report za utawala ule ! Wasoma report wangeweza kutaja mambo hasi zama zile? Huoni tumesomewa report ya CAG juu ya hasara shirika la ndege ! Ila miezi michache iliyopita si ndio tuliambiwa watalii wamejaa hadi ndege zimefurika booking??

Ukweli ni kuwa tutayajua mengi tu yaliyotumia nguvu kuyaficha
 
Mkuu, mimi pia simtetei mtu, najaribu kushangaa hii jamhuri ya watumia mtandao ambao kimsingi haiwezi kuwa hata asilimia 40 ya waTz wote kutaka kuamua ukweli wa TZ yote.

Uhuru wa habari si hoja ya msingi, kama kweli nchi ilisimama kimaendeleo kwa kuminywa uhuru huo katika hiyo miaka 5, tuoneshe maendeleo yaliyopo ambayo yanafanana na miaka 55 ya taifa huru hili, zingatia nchi kama Singapore, Thailand na pengine China tuliokuwa nao sawa wakati huo.

Tumekaa tunajaribu hata kufananisha TZ na Rwanda, ila hatutaki kupitia kwenye tanuru ili kuendelea.

China waliendelea, ila gharama ya maendeleo hayo sio hii mnayotaka ninyi. USA waliendelea ila sio kwa demokrasia, ukoloni na utumwa ulihusika ili mataifa ya ulaya kuendelea.

Hatuko kwenye level ya kutapata maendeleo kwa siasa, demokrasia na kubembelezana
 
Hahaaaa mzee jama kafa na alishazikwa huamini!??/duuu aisee msukuma umechelewa wewe!!
Govi linakuwasha kalitoe ndugu !!!
Kila kitu maguuu maguuu maguuu maguuu mfate alipo
 
CAG Assad?
 

Tulikuwa tunaaminishwa IPTL,Dowans na Meremeta ni Mr Nywele nyeupe kwa miaka kumi, mwisho wa siku kilichotokea πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡ tukashindwa kuamini. Tatizo waliopo madarakani hatuwaamini, ila wanaotaka kuingia ndio hawaaminiki kabisa.
 
Sikuwahi kuunga mkono nywele nyeupe kupokelewa CHADEMA hivyo hivyo sijawahi na sitowahi kuamini mtu aliyewahi kuwa mtendaji wa shughuli za kila siku serikalini (PM ) akawe mpinzani "halisi" never in a million years kwa Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…