macho_mdiliko
Platinum Member
- Mar 10, 2008
- 25,191
- 48,765
Yanatengenezwa mazingira ya 'dharura' hapo...Hivi ni lini kutakuwa na umeme wa uhakika Tanzania??Maana watumiaji ni proportion chache tu ya raia wote,ile kuwakidhi hao tu nalo limekuwa shida.Where is da vision mr president?Ngeleja?Rashid(if u r stil there)?
Huwa inauma sana Mkuu.Mkuu tulishaambiwa kwamba Kikwete katika awamu yake ya kwanza katimiza yale yote yaliyokuwemo ndani ya ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005. Nadhani asilimia kubwa ya yaliyokuwemo kwenye ilani hiyo ni kuwakingia kifua mafisadi wote kuanzia Mkapa, Rostam, Karamagi, Iddrisa Rashid, Mzee wa Vijisenti na wengineo wengi. Ingekuwa nchi nyingi uchaguzi wa mwaka huu CCM ingekiona cha mtema kuni kilimchotoa kanga manyoya kwa kuwadharau kabisa wapiga kura, lakni kwa nchi yetu watashinda tena kwa kishindi kikubwa na kurudi tena madarakani kiulaini kabisa. Mungu inusuru nchi yetu.
Pamoja na kuwa na mito yote inayotuzunguka na rasilimali nyingi tulizonazo bado hata hatuwezi tukaumiza vichwa japo kidogo tu tuone tutajikwamua vipi na tatizo la nishati.Inabidi tufike mahala tukalitendea taifa letu haki ambapo ni pamoja na kuondoa kero kama hizi na hata tukafikiria kuwa mzee mwanakijiji kule aliko na wazee wenzake waache kukata magogo kwa ajili ya mkaa kwa kuwasambazia umeme vijiji.Sasa unafikiri zile generator 'zetu' tutazipeleka wapi???
Mimi niko Mbeya umeme ulikatikatika saa 1:00 jioni mkoa mzima wa Mbeya, nikajua sasa hapa ngoja tusubiri isije ikawa kama alivyosema Askofu KKB kuwa ataombea umeme usiwake,Habari zinazotiririka sasa hivi zinadokeza kuwa umeme umekatika katika maeneo mbalimbali ya nchi na hadi hivi sasa bado chanzo hakijajulikana lakini siwezi kushangaa kutasababisha kununuliwa kwa haraka kwa mitambo ya Dowans (kitu ambacho hakitaondoa tatizolenyewe)..
Mikoa ambayo inaripoti kukatika kwa umeme ni maeneo kadha ya Jiji la Dar, Mwanza, Moro, Tanga, Arusha.. tunaendelea kufuatiliia..
Sasa unafikiri zile generator 'zetu' tutazipeleka wapi???
Mimi niko Mbeya umeme ulikatikatika saa 1:00 jioni mkoa mzima wa Mbeya, nikajua sasa hapa ngoja tusubiri isije ikawa kama alivyosema Askofu KKB kuwa ataombea umeme usiwake,
Kama umeme umekatika Mbeya maana yake hata Iringa itakuwa hivyo.
Mbona nilisikia alishakubali Tanesco wapitishe nyaya karibu na kanisa lake..au alibadili mawazo?
Hakukubali.... ila imebidi asalimu amri..... nguvu ya dola...na nasikia akasema atapitisha maombi ili usiwake...
Tungependa hawa CCM watueleze said:[/FONT]
Uchaguzi umekaribia kina R.Aziz na EL hawana uhakika wa kurudi Bungeni kwani wamebanwa majimboni mwao sasa wanataka kutumia muda huu kumalizia mambo yao kama vile kuuza hii mitambo mapema ili hata wasiporudi basi Serikali ijayo isiizuie au kuitaifisha hii mitambo iliyokwishajifia.
Mwaka wa 2010 hakuna umeme! Hii kweli ni ari mpya na nguvu mpya ya kumaliza nchi.
Upepo tunao, kwanini wasitumie wind turbine generators. Halafu mnadai eti mna viongozi na wana taaluma. lol.
Wapige simu siemens ujerumani watawasaidia hawa. Kama hawana number wanipigie simu, nitawasaidia.
uwe unaongea mambo ya maana na wewe .sio unakuwa na chuki za kipumbavu na watu.Umeme ukatike unamhusisha Lowassa na Rostam...umaskini wa mawazo kitu kibaya sana
mikoa mbalimbali imeanza kuripoti kurudi kwa umeme.. nadhani hali itakuwa imetengemaa
Habari zilizothibitishwa na Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Ngeleja zinasema kuwa tatizo la umeme lililoikumba nchi muda mfupi ulipita linatokana na matatizo ya kiufndi kwenye gridi ya taifa na juhudi zinaendelea wakati huu kuhakikisha kuwa hali inatengemaa kabla ya kupambazuka.
Akizungumza nami muda mfupi uliopita Waziri Ngeleja amesema kuwa matatizo kama haya huwa yanaweza kutokea na kwa vile ni ya kiufundi zaidi basi yanahitaji umakini wa hali ya juu kuyatatua na amewahakikishia wananchi kuwa juhudi zote zinafanywa ili kurejesha hali katika hali ya kawaida.
.......
MM Naomba Number ya NgelejaHabari zilizothibitishwa na Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Ngeleja zinasema kuwa tatizo la umeme lililoikumba nchi muda mfupi uliopita linatokana na matatizo ya kiufndi kwenye gridi ya taifa na juhudi zinaendelea wakati huu kuhakikisha kuwa hali inatengemaa kabla ya kupambazuka.
Akizungumza nami muda mfupi uliopita Waziri Ngeleja amesema kuwa matatizo kama haya huwa yanaweza kutokea na kwa vile ni ya kiufundi zaidi basi yanahitaji umakini wa hali ya juu kuyatatua na amewahakikishia wananchi kuwa juhudi zote zinafanywa ili kurejesha hali katika hali ya kawaida.
"Siyo tatizo la sehemu sehemu tu, ni tatizo la system nzima ya gridi yetu na mafundi wetu wako kazini sasa hivi kurejesha hali katika hali ya kawaida" amesema Bw. Ngeleja.
Wakati huo huo nilitumia muda huo kumpa pongezi kwa jinsi alivyosimamia suala la Kakobe na Nguzo za umeme na hatimaye kuifanya serikali ichukue msimamo badala ya kuyumbishwa kirahisi. Nilimhakikishia kuwa Watanzania wanataka kuona serikali yao inachukua maamuzi badala ya vikao visivyoisha hasa kwenye mambo ambayo uamuzi unahitajika haraka.