Baada ya kulemewa sana na madeni, sasa uwanja wa Real Madrid ni ukumbi wa harusi

KING MIDAS

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2010
Posts
8,589
Reaction score
16,936
⚪⚪ Real Madrid C.F. wameanza kuandaa harusi katika uwanja wao wa Bernabeu kama njia mojawapo ya kukusanya fedha ya kulipa mikopo ya mabilioni ya fedha waliyokopa kwa ajili ya kufadhili ukarabati wa uwanja huo.

•Kwa mujibu wa Mundo Deportivo Klabu ya RealMadrid sasa ina deni kubwa zaidi kuliko klabu yoyote nyingine barani Ulaya.

•Uwanja wa Bernabeu sasa una ubora wa hali ya juu, ukiwa na miundombinu ya kisasa kama vile paa linalofunguka na kufungwa, mfumo bora wa sauti na mwanga, pamoja na viti vya kisasa kwa ajili ya mashabiki.

 
Hadi ugali na samaki upo ndani ya Bernabeu mkuu?
 
Ni pesa yako tu hata Wembley ukitaka kufanya harusi yako unaweza kukodi. Wembley wanatumia sana kwa boxing,concert za muziki etc. Btw hivyo viwanja vya Ulaya unavyoviona vyote vina private boxes, lounge na halls za ukubwa tofauti humo humo ndani ambazo huwa zinakodishwa kwa matukio mbalimbali zikiwemo harusi.
 
Huo Ugali kuku na chips samaki vinahusiana vipi na Real Madrid kuelemewa na madeni? Halafu umeleta taarifa kichawi chawi sana. Uchawi hauna faida.
Fan wa barca huyo. Pale barca kuanzia coach Xavi hadi mashabiki wanawachukia sana Real Madrid kwakuwa wale wana wanaishi kinyamwezi sana na mambo yao yanaenda wakati wao wanaishi kimakonde kama wapo huko ntwara kwenye samaki nchanga na si moja wala mbili inayokaa.
 
Nashindwa kuacha kushangaa kwamba mtoa mada alikuwa hajui kuwa hayo matukio mara kadhaa na kwa viwanja vingi vya football hufanyikia humo.

Wakati mwingine hata kumbi za mikutano na michezo inayochukua mashaabiki wachache pia hupatikana humo.
 
Nashindwa kuacha kushangaa kwamba mtoa mada alikuwa hajui kuwa hayo matukio mara kadhaa na kwa viwanja vingi vya football hufanyikia humo.

Wakati mwingine hata kumbi za mikutano na michezo inayochukua mashaabiki wachache pia hupatikana humo.
Wengi hawajui kuwa hivyo viwanja vikoje ndani, mpaka ufike au ufanye utafiti.
 
Madrid ama Barcelona? Barca inadaiwa kila sehemu wanauza karibia vitu vyao vyote. Deni la Madrid ni cha Mtoto kwa Barca.
 
Mkuu huo Uwanja una maeneo ya kukodi iwe hotels,Bar mpaka maeneo ya Bank yapo hapo sio swala la madeni na pia taarifa ya Ugali na Samaki umechapia...ukiweza kwenda ukauona huo Uwanja sidhani kama kuna siku utakuja kuandika kama ulivyoandika..
 
Kwa hiyo na ugali wanapika kwa maharusi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…