Uchaguzi 2020 Baada ya kumsikiliza Tundu Lissu akiwa kwenye mkutano wa ACT-Wazalendo, nimejiridhisha ni mgombea dhaifu zaidi awamu hii

Nashauri vyombo vya dola viendelee kumpuuza kabisa, kuchukua hatua dhidi yake nikimpa kick, siku hazigandi kwani tarehe 28/10/2020 ni keshokutwa tu hapo.
Vyombo vya dola havimpuuzi, viliandikiwa barua na Amsterdam advocates.
 
Umemaliza, ana hasira mbaya sana itakayomgharimu zaidi ya kile alichopata vilevile ana umimi so hafai kuwa kiongozi.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app

..hana hasira.

..jingine ni kwamba hana uoga.

..pia amesema ndani siku 100 za utawala wake ataanzisha tume ya MARIDHIANO na suala la kulipa kisasi haliko kabisa ktk ajenda zake.
 
Kitendo tu cha kumuandikia uzi kinaonesha jinsi TL alivyo na nguvu
 
Kwenye Yeye kuwa na 'Hasira' nakubaliana nawe japo hata bado hajafikia 25% ya 'Hasira' zangu, ila Yeye kuwa 'Mmimi' nakukatalia na umekosea.

..TL ameahidi kuwa akipewa ridhaa ya kuongoza ataanzisha tume ya MARIDHIANO ya kitaifa ili kuondoa uwezekano wa watu kulipiziana visasi na kuliingiza taifa ktk machafuko.

..wengi walitegemea kuwa TL atakuwa MUOGA baada ya tukio lile. Sasa huu ujasiri anaounyesha baadhi wanautafsiri kama hasira au kutaka kulipa kisasi kitu ambacho siyo kweli.
 
Lisu yupo empty kabisa,na hajakaa kiuongozi zaid ya ulalamishi tu na kubadili ukweli kua uongo.
 
Lumumba wanaweweseka Sana,Lissu kawashika pazuri!
 
Tundu Lissu anaweza akawa na Hoja, ila 'Kisaikolojia' anaonekana 99.9% ya atakayokuwa akiongea katika 'Kampeni' ni Shambulizi lake si Masuala.
Kwa sasa Tanzania inachokosa kuliko vyote ni uhuru wa mawazo. Na mawazo ndiyo huleta ubunifu.

Jamii ya watu waliokosa uhuru wa mawazo haiwezi kugundua kitu.

Angalia nchi kama China yenye watu zaidi ya bilioni moja, hakuna kitu wanachogundua. Siku zote wamekuwa watu wa kuiga. Inazidiwa kwa ugunduzi na nchi kama Sweden, Netherlands, Singapore, Israel, UK, Germany, n.k. Nchi yenye watu zaidi ya bilioni moja inahangaika na kutafuta wawekezaji kutoka kwa nchi kama Netherlands na Singapore, zenye watu kila moja, wasiofika 20 milioni.

Wataalam wa Human science wanaeleza kuwa kuna mahusiano ya karibu sana kati ugunduzi na uhuru wa fikra.

Tundu Lisu ni mhanga wa kukataa kufungiwa kufikiri na kunena. Anaenda kwa watu kutetea uhuru wao wa kufikiri na kutenda huku yeye mwenyewe akiwa shahidi wa namna utawala wetu unavyotaka kuwafanya watu kuwa mateka wa kufikiri.

Acha tu alielezee hilo shambulio. Jambo baya sana au zuri sana, ni sahihi kunenwa mara nyingi. Usishangae wala kukereheka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umemaliza, ana hasira mbaya sana itakayomgharimu zaidi ya kile alichopata vilevile ana umimi so hafai kuwa kiongozi.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Mwenye umimi mbaya kabisa ni yule anayeweza kuamua kumwua binadamu mwingine kwa sababu tu kampinga. Aheri mwenye umimi wa maneno maana atajibiwa kuliko mwenye umimi wa kuamua kuwaondoa wote wasiotaka kuukubali umimi wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitu muhimu ni kwamba watanzania washampuuza Lissu kitambo sana.
Sema baadhi ya wanaCCM, hasa wale wenye upeo mdogo, siyo Watanzania wote.

Wapo Watanzania wengi wanaozingatia mambo muhimu yote anayozungumza Tundu Lisu. Pia wapo wanaCCM wenye akili kama Mh. Anna Makinda alitamka wazi juu ya mchango wa pekee wa Tundu Lisu Bungeni. Na alisema kwamba kuna mambo yalitarajiwa yasemwe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali lakini hakuyasema, bali ni Lisu aliyekuwa akiwafumbua macho.

Ukiwa na akili ndogo huwezi kumwelewa Tundu Lisu.

Mzee Warioba aliwahi kusema 'kama itatokea Tundu Lisu akawa Rais, watu wajiandae kuishi kwa kufuata sheria, jambo ambalo ni jema'

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Toa hoja jombaa


Hoja zimetulia alaf unadai za kuungaunga?

Ni ukweli mtupu Lissu hafai na yupo kuvuruga amani yetu kwa maslahi ya mabeberuu
 
Hahaaaa
Bora wasirushe habari zake tu maana kila analoongea ni jaziba na uchochezi mtupuuu
 
Ushabiki na masifu vyote vinawaondolea uwezo wa kufikiri. Uzi aliotunga ni kiwango cha mtoto wa chekechea.
 
Yaani mpaka kufikia Oktoba tutakua tumesikia neno Risasi zaidi ya Mara elfu kwa siku.
 
Umesikika Naibu W. Ulifanikiwa kupenya kwenye kura za maoni kule Songwe?
Hahahaa, Hawa ni watu wasiojulikana wanahangaika kweli na lissu.hawalali.kwa hakika lisu ni kidume wa taifa.kitendo Cha lissu kuingia ulingoni imekuwa balaa.
 
Hata sijakuelewa
Magufuli for another 5 years anatosha.
 
LISSU NI GAME CHANGER!! Siasa za Tz tangu tarehe 27 July Lissu kurejea nchini zimebadilika Sana.Namna ya watu kuwaza na kufikiri,pia kutenda imebadilika Sana.NAFIKIRI HATA MIKAKATI YA WATU WEMA NA WABAYA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU NAYO IMEBADILIKA SANA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…