Baada ya kushindwa hoja sasa wanajaribu kuhamisha mjadala kwa kuwabambikia kesi za ajabu ajabu wakosoaji

Baada ya kushindwa hoja sasa wanajaribu kuhamisha mjadala kwa kuwabambikia kesi za ajabu ajabu wakosoaji

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Inawezekana ndivyo mabingwa wa siasa ndani ya chama wamemshauri hivyo. Kuwa ili watu waache kujadili ule mkataba wa ajabu kabisa uliosainiwa na serikali basi watu fulani fulani wakamatwe na kupewa kesi za nzito nzito.

Kwamba mjadala utahamia kwenye kesi hizo za jinai badala ya mkataba. Mambo yakipoa basi watu wataomba kurudi mezani kwenye maridhiano.

Dear Mama naniliu, hauna mtaji wa kutosha kuwa na maadui ndani ya chama na nje ya chama. Badala ya kuongeza maadui ni vema ungefanya jitihada za kuongeza marafiki wa kweli, ndani na nje ya chama.

Sio kila anayekushauri namna ya kupambana na 'wapinzani' wako ana nia njema na wewe. Na sio kila anayekupinga ana chuki binafsi na wewe.
 
Back
Top Bottom