Baada ya kushuhudia show ya Saida Karoli

Hakuna bampa hapo, ni uelewa kichwa maji tu. Watanzania maana yake ni wananchi kwa ujumla
Miongoni mwa watanzania kuna MAKABILA na hilo linapelekea UKABILA na LIPO tu,lipo maofisini lipo mitaani lopo mashuleni,kuna makabila bado yanaamini katika UKABILA iwe kwa connections au jambo lolote hata kwa wenye elimu ya levo ya Lipumber
 
Watoto wanne kila mtoto na baba yake? ? Nampa hongera ni mwanamke wa shoka.
 
Miongoni mwa watanzania kuna MAKABILA na hilo linapelekea UKABILA na LIPO tu,lipo maofisini lipo mitaani lopo mashuleni,kuna makabila bado yanaamini katika UKABILA iwe kwa connections au jambo lolote hata kwa wenye elimu ya levo ya Lipumber


Don't drag me away from my point. Aliyemsainisha Saida Karori kwenye mikataba ya ulaghai ni Felician Muta, ni muhaya. Sasa uliposema hata wahaya nao ni watanzania naona kama unachangaya madesa tu.
 
Sijaongelea muziki wake hapo
Watanzania tunashindwa kutoboa kwa unafiki na woga wakusema kweli, mimi ni mtanzania na siyo mhaya na sikubali kulalamikiwa kwa kumdhulumu saida, tunajua wazi waliomzulumu ni wahaya wenzake waliojidai kumbela kumbe wanataka awabebe, huyu mama aliwahi kujaza Nakavubo stadium, wakina Fred Rwegasira wale wakihaya wakawa wao ndio kama baba na mama zake, na yeye kwa ushamba hakujua hili akawaegemea, sasa naamini ameshituka japo Ruge nae mhaya na huyo Tumsiime siji mhaya sijui mganda tumuombee mungu tu. Ila abaki kwenye category hiyo ya local/cultural mambo ya kulama uzungu aachane nayo kabisa, mambo ya mingao na viatu virefu no no no
 
Hakuwa na elimu wala uwezo wa kujua mambo, hata alipojaza uwanja wakimpa milioni 2 anaona sawa tu, anatakiwa kuwa na manager mwenye nia ya dhati kabisa kumsaidia huyu mama
 
Kwanza mnachotakiwa kujua ni kuwa Saida hakuwa Bench ila alikuwa hasikiki tu,kwa wale wa mikoa ya Mwanza na kanda ya ziwa kote watakuwa mashaidi wa hili kuwa alikuwa anafanya kazi yake ya muziki kama kawa na shoo alikuwa anafanya.Sasa kinachotokea leo hii ni kupewa tena airtime kama zamani.
 
Uko sahihi. Pia kuna mtu anaitwa Felicien Muta (FM). Huyu ndo alimuibua na kumzamisha Saida. Taifa alikua kila akipafomu inatapika. Hakuna show ya Saida iliyododa. Chezea Halidi na Philimoni [emoji38]

FM alimpangishia sinza na Saida alipotapisha Taifa mara ya kwanza FM alimnunulia Chaser mayai enzi hizo. Malipo ya show zote hatimiliki na kila pembe ya muziki wa Saida ispokua kipaji alimiliki FM.

FM ndie alikua na lebo inaitwa FM music studio. Alikua anagonga kopi za kanda za bolingo ile mbaya. Rangi za kanda zake bluu na njano. Ndio hiyo studio alikua anarekodia nyimbo za saida.

FM Music Band ilikua ya Muta. Kuna magwiji humo ambao baadae walijiondoa wakilalama kuzulimiwa. Walijiita FM Academia. Sasa wakijulikana zaidi kama Wazee wa Ngwasuma. Kina Nyoshi.

Hiyo historia kidogo. Na ni sahihi kusema Saida alidhulimiwa na Wahaya wenzie. Specifically Muta na Rwega.

Na sasa amepata kiki tena. Na wanaomuibua ni haohao wa kwao. Nadhani Ruge na Gire. Uzuri wote wako njema.

Kila la heri Saida mpya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…