Baada ya kutimuliwa kwenye Ligi kuu NBA Hasheem Thabeet atimuliwa ligi ya chini G league[emoji28]

Mkuu usichukue uzi wa tweet na kujenga hoja kwamba "wamarekani" wanamchamba. Inawezekana vile vile kuna uzi wa tweet wa "wamarekani" wakimsifia!!!

We ungetueleza kwanza ligi ya chini anayocheza sasa ni ipi? kaingia lini? katimuliwa lini? na sababu zilizotolewa kumtimua ni zipi?
Hapa utakuwa umetuelimisha vizuri tujue kinachoendelea!!! We labda mjuzi wa haya mambo tuelimishe na sie basi!!!
 
Mtoa mada hamna kitu , kaishia English course
 
Tunafurahia sana wenzetu wasipofanikiwa, wakitukanwa kwenye mitandao, wakiandikwa kwa mabaya hata tusiyoyafahamu, wakioneshwa hawawezi, wakitumbuliwa na hayo yote mabaya. Binadamu tuna chuki kubwa dhidi ya wenzetu. Hebu jifikirie, ungekuwa wewe ungejisikiaje? Halafu hebu fikiri zaidi, je, itakusaidia nini ukifurahia mabaya yakimtokea mtu mwingine? Do you gain anything? Itakupa mkate wa siku? Tusiwe sadists. Leo kwake, kesho kwako,
 
Na ww punguza unafik wa mitandaoni, utafikir huyo hashim alishawah kukupa buku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
What a pity!
Apambane aende hata uchina huko akatafute maisha Mengine, au akomae zaidi lakini umri umeamza kwenda.

Kwa mara nyingine tena tumepungukiwa uwakilishi kwenye mataifa ya wenzetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Basi nyuzi kama hizi wabongo wanachangia meno yote nje
Wanafurahi kinoma yani unakuta mtu hajala siku nne , anadaiwa kodi , anamkwepa mwenye nyumba wake, ada ya shule ya wanawe.hajamaliza kulipa, ila akisikia mtanzania mwenzie amefeli maisha anafurahi kinyama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hali tata...!!!!
ni kumpa moyo tu sasa kwa atakachofanya baada....ila tunae "samagoal" walao!!!!
 
Wanafurahi kinoma yani unakuta mtu hajala siku nne , anadaiwa kodi , anamkwepa mwenye nyumba wake, ada ya shule ya wanawe.hajamaliza kulipa, ila akisikia mtanzania mwenzie amefeli maisha anafurahi kinyama

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa iyo mambo mabaya hatutakiwi kuongelea? Nyie ndo mtu akipost picha wanafunzi wapo foleni ya maji mnawateka yaani mnapenda kupongezwa tuu. Mbona alipoingia NBA pia tulimpongeza? Kwaiyo wewe ukinya njiani unataka sisi tupige kimya tu ufanye yako, jifunzeni kubalance maisha kuna mazuri na mabaya yote tutayaongelea ndo tulivyoumbwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hasheem Thabeet pole sana. Inaweza isiwe kwenye NBA lakini unaweza jaribu bahati yako sehemu nyingine. Cha muhimu ni kutokata tamaa. Kama MTanzania hii habari si nzuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…