Baada Ya Mo Dewj Kunyimwa Simba, Msimu Huu wa Simba Utakuwa mbaya kuliko yote

Mbona haja nyimwa timu maana uongozi Leo umeandika barua ya kumkaribisha ktk kikao atakacho elekeza mikakati yake tarehe 15/8 tembelea blog ya Millard ayo utaiona
 
Simba imekuwa kama kikundi cha wahuni au kikundi cha ushangiliaji, Timu kama hii ambayo ikifungwa wanapigana au wanapiga mawe magari ya viongozi wao, Timu ambayo wachezaji wanakaa wanadai malimbikizo ya mishahara, timu ambayo wachezaji wanapanda daladala na boda boda kwenda uwanjani kucheza mechi ya ligi, Timu ambayo wachezaji wanashindana kushiriki michezo ya ndondo cup....Simba mbumbumbu fc inatakiwa ishushwe daraja au ifutwe kabisa kwa kushusha hadhi ya Ligi kuu Tanzania.
 
Tatizo mnashinda tu JF ndio maana mnaandika upumbavu sasa mtoa maada hapo umeandika nini?alafu unajiita shabiki wa simba au kwenye mkutano juzi haukwenda???

Ifike mahali unapo toa taarifa kama hii uwe na uhakika nayo basi Japo kwa aslimia 5% tu,ila pole maana lengo lako halija kamilika
 
hiyo ni offer yake sasa kama na wewe unajeuri weka mzingo mezani mfano bil 30...
Simba wemeashikwa pabaya sana..... Hivi thamani ya Simba ni 20b!!!??? Nani aliyefanya huyo UTHAMINISHAJI!!!??? Kitu cha pili hizi bilioni 20 hzipewi timu moja kwa moja ni uwekezaji wa HATI FUNGANI ambapo faida yake ni almost 3.7 bilioni kwa mwaka ambapo ndio Simba itapata , kwa wakati huohuo Mo akiwa ndio muwekezaji mkubwa 51% hiyo faida ya 3.7 bilions na yeye anapata 51% ya 3.7 bilions hivyo atapata kama 1.9 bilions na Simba 1.8 billions ....

Huyu jamaa ni "KICHWA " ..... KAWATAJIA TU BEI HAJAWACHAMBULIA MGAWANYO WA MAPATO NA MATUMIZI KWA UWEKEZAJI WAKE..... TAYARI SIMBA WANATAFUTANA..... kamoshi kama ka ileeee YANGA ACADEMIA ,YANGA ASILI NA YANGA KAMPUNI kananukia Simba.... Mo kanunua mashabiki wampigie debe .... Na kuna matajiri wengine nao wananunua mashabiki wa kumpinga Mo..... Acha muvi iendeleee

.
 
Sasa Simba ikipata 1.8 Bil na Mo akapata 1.9 tatizo liko wapi? kwa kwasasa tunapata nini? halafu haiuzwi nakama inauzwa 100-51 basi thamani ya Simba ni bil 40 kasoro na siyo 20 kama unavyotaka kutuaminisha ukikumbwe tar 15.8 ndiyo wanaanza majadiliano na kamati tendaji ya Simba na hapo ndiyo wataanza kuzungumziabmasirahi ya pande zote na pengine kiwango kikaongezeka...
..Acha watu wawekeze na Mimi nitanunua...
 
Hizo assets zipo miaka mingap sasa? Brand ya simba ipo miaka mingap sasa? Jengo lina umri gan na lina hali gani? Linaisaidia klabu kwa asilimia ngapi?wanachama wangap wa Simba watakaoweza nunu hisa za kufikisha bil 5 ?tuzungumze kiuhalisia.




QUOTE="bigmind, post: 17044337, member: 336342"]Umasikini kitu kibaya sana, hiyo hiyo sinpesa ya kununua assets tu za simba[emoji15] [emoji15] [emoji15] lile jengo pale katikati ya jijji kariakooo unajua lina thamani gani? Fikiria pia brand ya simba nimkubwa sana hiyo pesa ndilogo shida ni kwamba uendeshaji wakw ni wa kipuuzi kuna wapiga peaa tu basi!

Mkakati uwe hivi wauze hisa kwa wanachama then waajiri kampuni ya kuiendesha simba kibiashara ibaki kugawa faida ikitokea hivyo.[/QUOTE]
 
[/QUOTE]
kuna wakati ilikuwa ni dampo tu...acha mabadiliko yaje...
 
Hebu uwe unashughulisha akili yako. Mwandishi hajasema amenyimwa ametoa angalizo nini kitatokea kama akinyimwa. Na ndo.maana ya baada ni kama kutabiri.
Kwa nini hampendi kwenda shule mkajifunze?yaani ninyi watu mnaamini ukijua kusoma na kuandika basi...?hujifunzi kufikiri na kutafsir? Au ndo muda mwing akili inashughulika na viloba?


 
Km thamani ya majengo ya simba unambiwa ni bilioni 3 uoni bilioni 20 n nyingi kwa simba, Mo ndo kajichaganya 20b n nyingi sana kwa simba
 
Km thamani ya majengo ya simba unambiwa ni bilioni 3 uoni bilioni 20 n nyingi kwa simba, Mo ndo kajichaganya 20b n nyingi sana kwa simba
Jina la Simba thamani yake ni kubwa kuliko majengo...
 
Ugumu wa Mo kupewa timu ya Simba,hausababishwa na wanachama wa Simba Sc bali unasababishwa na baadhi ya viongozi wakiongozwa na Evance Aveva.Ila wakiendelea kuweka ugumu,mwaka huu Simba Sc itafanya vibaya kuliko misimu mingine
 
Mashabiki wa simba nao wamekuwa ng'ombe sijui? kila unaekutana nae moo moo moo kuna haja ya kuwajengea zizi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nani kaukdanganya kuwa jina la Simba ni kubwa kwa hali iliyopo sasa?ukubwa wake nini kama pesa hamna? unadhan wachezaji watakuja kucheza simba kwa sababu ya jina? watu WANATAKA PESA SASA BAKI NA JINA LA SIMBA.uone misimu ijayo inakuaje. unaiona azam?ilikuwa na jina gani? sasa inafanyaje? ninyi washabiki mtabaki kusema klabu kongwe miaka yote wakati hamna linalofnyika la maana. mnataka muendelee kukaa pale kunywa kahawa miaka na miaka jengo linachakaa, simba haina kiwanja, haina hostel...na bado unasimama mbele ya wanaume unasema simba ni jina kubwa lenyewe tu lina thamani.

Jina la Simba thamani yake ni kubwa kuliko majengo...
 
Ungesoma ukaelewa ....
1) Aliyesema hiyo 20b ni hisa za 51% ni kwa uthaminishaji UPI!!!??.....
2) Umesoma mapato na matumizi ya Simba misimu hata mitatu iliyopita!!!??
3) Unajua Simba wanaingiza ngapi bila kuuzwa kwa hizo hisa!!!?? Kwa sasa .....
4) Anaposema wanachama wapewe hisa wanapewa kwa mtindo gani!!???
5) Simba ni kampuni au timu ya wanachama, katiba yake inasemaje!!??? Imebadilishwa lini!!???
6) Mchakato wa utengenezaji wa hisa na uuzwaji wa hisa unaufahamu!!???

Mnovosema Mo apewe timu .... Sio kirahisi hivyo kuna vitu vingi sana vya kuangaliwa kwa jicho la pili na la tatu..... Na ni mchakato mrefu sio wa kukurupuka kama mnavyotaka..... Ni jambo jema ila mkikurupuka ndio anguko la simba ..... Mnahitaji kutuliza kichwa kwelikweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…