#COVID19 Baada ya mtu kupata chanjo ya Covid-19 miongoni mwa mambo ya kuzingatia ni kutopata kilevi cha aina yoyote kwa saa 72 (siku tatu)

Chanjachanja hata hatujui tunadhibiti nn?

mpukutiko upo palepale.....

bora yuleee alituambia tufunge Na kuswali.....

tumrudie Mola wetu.....

#kufa tutakufa tuu....#
 
Dah yaani juzi tulichoma asubuhi jioni tukaenda club kujipongeza.. Na tuligida ulabu hasa
Mkuu hizi ni porojo za ''wanasayansi wa Bongolala. Sehemu nyingine zote duniani hakuna masharti kama haya. Nasisitiza, chanjo haiingiliani na chakula aua dawa. Hii ni kwa mujibu wa WHO na pia watengezeaji wa chanjo zote zilizopitishwa na WHO.
Should we eat or drink differently the day or two after getting vaccinated?

The effectiveness of the vaccine is not dependent on any food or drink before or after taking the vaccine
 
Naomba kuuliza,je kama MTU anatumia dawa,yaan yupo katika dozi YA MALARIA,NA PIA ANATUMIA DAWA ZA PRESHA..ANAPASWA KUCHANJWA?
 
Jamani nina swali ukichanjwa unapewa kithibitisho chochote kinachoonyesha umepata chanjo,
 
je sie ambao hatuchanji tunaruhusiwa kula bia baada ya muda gani
 
Hakika inashangaza sana kuona serikali imeruhusu chanjo kabla ya tahadhari za chanjo kutangazwa.

Kama watalaamu wetu wa afya haya waliyajua kwanini tahadhari zake hazikutolewa mapema kabla ya zoezi la chanjo kuanza?

Tunaiomba serikali pamoja na madhara atakayoyapata atakayechanja serikali kutohusika lakini ni wajibu wa serikali kutoa tahadhari kabla ya mtu kuchanja.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…