Baada ya picha za vyoo vya Shule ya Kamama (Uyui - Tabora) kuziweka hapa JF, nimeona wanajenga vyoo vipya

Baada ya picha za vyoo vya Shule ya Kamama (Uyui - Tabora) kuziweka hapa JF, nimeona wanajenga vyoo vipya

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
photo_2024-08-25_10-31-43.jpg

Ujenzi ukiendelea
Wiki mbili iliyopita niliandika kuhusu Shule ya Kamama iliyopo Kata ya Goweko, Kijiji cha Kamama, Wilayani Uyui kuwa ni hatarishi hasa Vyoo na madarasa, hatua zimeanza kuchukuliwa.

Kama hukuona andiko langu la awali, lipo hapa ~ Hali ilivyo Shule ya Msingi Kamama (Tabora) inasikitisha, vyoo ni chakavu na vichafu, madarasa ndio usiseme

Nimepita mitaa hiyo na kushuhudia ujenzi wa Vyoo ukiendelea kwa kasi eneo hilo la Shule hiyo, nilipouliza mmoja wa mafundi wanaoshiriki ujenzi huo akaniambia kuwa mipango iliyopo ni kujenga hadi madarasa ambayo nayo yanaonekana kuwa chakavu.
photo_2024-08-25_10-31-43 (2).jpg

photo_2024-08-25_10-31-43 (3).jpg
Kama hilo ni kweli basi nitoe pongezi kwa uongozi unaohusika wa suala hilo, hiki ndicho Wananchi tunachokitaka, nimezungumza kwa faida ya Jamii na Serikali imen/ chukua hatua.

Kiukweli vile vyoo ambavyo bado havijabomolewa ni tishio kwa watumiaji, ni chakavu sana kama ilivyo madarasa.

Tusisubiri majanga yatokee kisha ndio tuanze kusema ningejua ningefanya hivi au vile.

================ =================

MAJIBU YA VIONGOZI
Jamii Forums ilipowasiliana na Mkuu wa Wilaya ya Uyui, Zakaria Mwansasu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha kwa nyakati tofauti na kuwauliza kuhusu shule hiyo na kuhusu hoja ya Mdau, haya ndio yalikuwa majibu yao:

DC WA UYUI, Zakaria Mwansasu :
Utaratibu wa kuripoti jambo unakuwaje? Huyu Mwananchi aliyeripoti kwenu si anaijua Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na ya Mkoa zilipo, Mwananchi anatakiwa abalansi huku na huku kisha ndio aandike taarifa yake, nakushukuru (akakata simu).

MKUU WA MKOA, Paul Chacha:
Ungekuwa wewe ungejibuje? Mimi sijui sijaona hiyo taarifa unayoniuliza, wala sina taarifa kuhusu Shule ya Msingi Kamama, sina taarifa unataka nikuambiaje, mimi sijui unachokisema na siwezi kukujibu chochote.

VYOO VYA AWALI
WhatsApp Image 2024-07-30 at 13.58.40_0e19a03d.jpg

WhatsApp Image 2024-07-30 at 14.02.26_d599236a.jpg

Pia soma:
~
Miundombinu ya Shule ya Msingi Kamama yaboreshwa, Vyoo na madarasa vyajengwa
 
Viongozi wanatakiwa kuwa makini na kauli zao hasa wanapotakiwa kutoa ufafanuzi wa mambo yenye maslahi kwa umma. Sio kwa hayo majibu
 
View attachment 3078667
Ujenzi ukiendelea
Wiki mbili iliyopita niliandika kuhusu Shule ya Kamama ilikiendevyopo Kata ya Goweko, Kijiji cha Kamama, Wilayani Uyui kuwa ni hatarishi hasa Vyoo na madarasa, Uhatula zimeanza kuchukuliwa.

Kama hukuona andiko langu la awali, lipo hapa Hali ilivyo Shule ya Msingi Kamama (Tabora) inasikitisha, vyoo ni chakavu na vichafu, madarasa ndio usiseme

Nimepita mitaa hiyo na kushuhudia ujenzi wa Vyoo ukiendelea kwa kasi eneo hilo la Shule hiyo, nilipouliza mmoja wa mafundi wanaoshiriki ujenzi huo akaniambia kuwa mipango iliyopo ni kujenga hadi madarasa ambayo nayo yanaonekana kuwa chakavu.
Kama hilo ni kweli basi nitoe pbongezi kwa uongozi unaohusika wa suala hilo, hiki ndicho Wananchi tunachokitaka, nimezungumza kwa faida ya Jamii na Serikali imen/ chukua hatua.

Kiukweli vile vyoo ambavyo bado havijabomolewa ni tishio kwa watumiaji, ni chakavu sana kama ilivyo madarasa.

Tusisubiri majanga yatokee kisha ndio tuanze kusema ningejua ningefanya hivi au vile.


================ =================

MAJIBU YA VIONGOZI
Jamii Forums ilipowasiliana na Mkuu wa Wilaya ya Uyui, Zakaria Mwansasu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha kwa nyakati tofauti na kuwauliza kuhusu shule hiyo na kuhusu hoja ya Mdau, haya ndio yalikuwa majibu yao:

DC WA UYUI, Zakaria Mwansasu :
Utaratibu wa kuripoti jambo unakuwaje? Huyu Mwananchi aliyeripoti kwenu si anaijua Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na ya Mkoa zilipo, Mwananchi anatakiwa abalansi huku na huku kisha ndio aandike taarifa yake, nakushukuru (akakata simu).

MKUU WA MKOA, Paul Chacha:
Ungekuwa wewe ungejibuje? Mimi sijui sijaona hiyo taarifa unayoniuliza, wala sina taarifa kuhusu Shule ya Msingi Kamama, sina taarifa unataka nikuambiaje, mimi sijui unachokisema na siwezi kukujibu chochote.

VYOO VYA AWALI
Mungu akubariki sana ndugu BigTall kwa kuliweka wazi hili mpaka hatua zikachukuliwa.
Kongole sana sana.
Sote tukiendeleza hili la kuweka wazi mambo ya hovyo yaliyopo mitaani, naamini kabisa kelele zetu hazitaenda bure kama ilivyotokea kwa hili ulilolipazia sauti na kuliweka hadharani hapa Jamii Forums.
Akhsante sana na ubarikiwe.
 
Hongera Sana umewasema, na kuwapa pongezi kwa kuchukua hatua, swali la kujiuliza hiyo bajeti ya ukarabati wa vyoo na madarasa ghafla ghafla hivyo imetoka wapi? usikute pesa ipo muda mrefu ila kuna wajinga waliikalia
 
"Nashukuru kwa taarifa na nampongeza huyo mwananchi kwa uzalendo mkubwa aliouonyesha, japo sijapata taarifa yake, lakin kesho mimi pamoja na timu yangu/ timu yangu itafika eneo la tukio na nakuhakikishia ujenzi utaanza mara moja ..asante sana"
Viongozi wanafeli wap?
 
Nchi ngumu hii 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣

Bajeti hii ilikuwepo kwa mtazamo wangu.

Sijui Nyie Wahenga Mnasemaje ______________
 
huwa najiuliza tu, wale wakaguzi wa shule ambao hufika shule zote pengine ndani ya miaka miwili; haya mambo hawayaoni, hadi yatoke kwenye TV au mitandao ya kijamii
Nafikiri ipo haja ya kuwataka report zao ziambatanishe picha kadhaa kwa kila shule kwa weledi kabisa.
 
Vyoo vyote vya shule ya msingi na sekondari VINA NUKAAA.na walimu hawajali.wanashindwa hata kujenga tiles vyooni.,wanashindwa hata kuweka vyoo vya sink chooni,wanashindwa kuweka hata vifaa vya usafi chooni.
 
"Nashukuru kwa taarifa na nampongeza huyo mwananchi kwa uzalendo mkubwa aliouonyesha, japo sijapata taarifa yake, lakin kesho mimi pamoja na timu yangu/ timu yangu itafika eneo la tukio na nakuhakikishia ujenzi utaanza mara moja ..asante sana"
Viongozi wanafeli wap?
Hawana weledi wa kiuongozi, Tanzania ili uteuliwe ni kuwa kada wa CCM basi, weledi hawana
 
Vyoo vyote vya shule ya msingi na sekondari VINA NUKAAA.na walimu hawajali.wanashindwa hata kujenga tiles vyooni.,wanashindwa hata kuweka vyoo vya sink chooni,wanashindwa kuweka hata vifaa vya usafi chooni.
unaendana na jina lako
 
Mimi huwa najiuliza tu, wale wanaoitwa wakaguzi wa shule ambao hufika shule zote pengine ndani ya miaka miwili; haya mambo hawayaoni?
Wadhibiti Ubora wa Shule ni mpango wa upigaji tu, hata uendeshaji wake unategemea michango Toka shuleni
 
Ntamani sana Maxence Melo haya majibu yangekuwa yanawekwa hadharani ili wahusika wawajibishwe hata na wananchi wenyewe
 
Back
Top Bottom