Elections 2015 Baada ya Pinda kutangaza nia, Membe afunguka

 
Hawa marais ambao Membe anadai wamekuwa connected na dunia kutokana kuongoza wizara kwa mambo ya nje ndio wanaotuchafulia nchi, mfano mzuri ni JK ameshindwa kupunguza umaskini, uchumi wa Tz umezidi kuporomoka, saraf ya Tz ndo ivyo tena, ajira imekuwa kama ndoto lakini ukimtathmini JK na safari za nje tokea amekuwa rais utagundua ni rais wa kwanza ulimwenguni anayeongoza kupanda ndege kwenda huko duniani lakini wananchi wake njaa na umaskini umekithiri hata mlo 1 kwa siku ni shida kwa watanzania walio wengi.

Ni bora kabisa mara hii kupata rais asiye na harufu za mambo ya nje kama Membe ni yale yale tu. Na ukweli ni kwamba huyu Membe inavyoonekana tayari wanataka kurithishana urais na JK labda kuna makato huko watakuwa wanapeyana sasa hii pia haikubaliki.
 

Hawa marais ambao Membe anadai wamekuwa connected na dunia kutokana kuongoza wizara kwa mambo ya nje ndio wanaotuchafulia nchi, mfano mzuri ni JK ameshindwa kupunguza umaskini, uchumi wa Tz umezidi kuporomoka, saraf ya Tz ndo ivyo tena, ajira imekuwa kama ndoto lakini ukimtathmini JK na safari za nje tokea amekuwa rais utagundua ni rais wa kwanza ulimwenguni anayeongoza kupanda ndege kwenda huko duniani lakini wananchi wake njaa na umaskini umekithiri hata mlo 1 kwa siku ni shida kwa watanzania walio wengi.

Ni bora kabisa mara hii kupata rais asiye na harufu za mambo ya nje kama Membe ni yale yale tu. Na ukweli ni kwamba huyu Membe inavyoonekana tayari wanataka kurithishana urais na JK labda kuna makato huko watakuwa wanapeyana sasa hii pia haikubaliki.
 
Kwa ccm hakuna wakumfikia E.L. Hao wengine wasindikizaji
 
[/QUOTE]
Nimekukubali sana,Membe hawezi kulingana hata kidogo kwa sifa nzuri alizonazo PINDA, Pinda anauwezo mkubwa sana kumzidi hyo Membe na ndio maana JK anamkubali sana PINDA zaidi ya MEMBE
 
Katika uongozi wa sasa, aina ya kiongozi wa kumrithi JK naona bado sijaona anayefaa coz we will need someone who can do a real transformation of how we work.. JK tried but we need someone to take it to the next level..Sasa kwa Membe bado sana!!!


Yes mkuu, LIKE EVERY OTHER CANDIDATE, WE EXPECT MORE THAN POLITICS FROM HIM. WE EXPECT A COMPLETE ROAD-MAP OF HOW WE GONNA REACH THE NEXT LEVEL FROM ALL CANDIDATES!
THE WORLD IS CHANGING EXPONENTIALLY AND SO MUST OUR NATIONAL LEADERSHIP!

 
Huyu nayee mropokaji tu!!

Kuna mtu humu kasema eti "...jamaa yupo poa sana" 2005 vijana woooooote walimshobokea JK! Matokeo yake ni setbacks and disappointments tu!!!
 
Hivi wahariri wa mwananchi (kwenye picha wanaonekana wanne inawezekana walikuwa zaidi) hawakuwa na kazi nyingine wagawane majukumu maswali yao wampe mmoja akamhoji? Na huo muda kulikuwa hakuna kazi wizarani hadi waziri anatumia ofisi kuongelea mambo yenye maudhui ya kichama?
 
MAELEZO YA MGOMBEA WA BAVICHA TAIFA FRANCIS BONIFACE MARWA

UTANGULIZI

Ndugu zangu watanzania, awali ya yote niwashukuru sana, ninyi nyote mtakaobahatika kukutana na huu ujumbe wangu mahususi ndani ya mitandao hii ya Kijamii, magazetini ama kupitia chombo kingine chochote kile cha habari ambacho nitaweza kumudu gharama zake ili kuifanikisha azma hii ya kuwafikishieni ujumbe wangu, juu ya nini hasa kimenisukuma kuingia katika kinyang'anyiro hiki cha kuiwania nafasi ya "Mratibu wa Hamasa" BAVICHA ngazi ya Taifa.

Natambua macho yote ya watanzania ndani ya mipaka ya Taifa letu, yameelekezwa kwenye chaguzi za Chama chetu zinazoendelea Nchini kote hivi sasa, ama wapo wanaozitakia mema, na wapo wanaozitakia shari, ili kesho wapate jambo la kuupotoshea umma, kupitia majukwaani, na vijiwe vyao vya kahawa, uji, Draft na Pool table.

Kutokana na hayo yote, na mengine mengi zaidi, ndio sababu wengi wetu hususani sisi vijana, tumechukua maamuzi magumu ya kuomba nafasi za uongozi ndani ya Taasisi hii pendwa kuliko zote Nchini, ili tupate fursa za kuitetea na kuilinda kama mboni ya Jicho.

Baraza letu la Vijana (BAVICHA), ni moyo wa Chama hiki, na hii ndio sababu, upo ulazima wa kuijenga na kuiimarisha BAVICHA na iwe imara, yenye misimamo isiyoyumbishwa na dola, tena yenye maamuzi magumu kwa maslahi ya Chama na wazalendo wa Taifa hili kwa ujumla wao, ambao ndio walipa kodi.

NIMEFANYA NINI NDANI YA CHAMA

Nimeichukua rasmi Kadi ya Chama mwaka 2001 huko kwetu Serengeti Mara, mwishoni mwa mwaka 2009 kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa nikiwa Shuleni Kidato cha Pili, nikachaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa Chama ndani ya Kata yangu. Baada ya kukabidhiwa majukumu hayo ya kuibeba dhamana ya Chama, licha ya kwamba nilikuwa Shuleni, nilijituma kadri ya uwezo wangu kukijenga na kukieneza Chama ndani na nje ya kata yetu, kupitia michezo ya Shule za Sekondari, kwa kukutana na watu Sokoni, minadani na hata pia kupitia Vikundi rika vya Maendeleo huko vijijini, ambavyo huko kwetu Mara tunaviita "Saiga".

Uchaguzi ulipotangazwa rasmi, tukawaandaa wagombea wetu, na tukaingia msituni kupambana, baada ya uchaguzi, tukashinda wenyeviti wawili wa vitongoji kati ya watatu waliopo kijijini kwetu, cha kushangaza, CCM wakashinda nafasi moja ya kitongoji, ila wakamtangaza Mwenyekiti wa Kijiji kigumashi, jambo lililonikera sana, haijawahi kunitokea.

Baada ya uchaguzi huo wa Serikali za mitaa, ikafata zamu ya uchaguzi wa Serikali Kuu, madiwani, wabunge na Rais. Hapa sasa, ilikuwa ni patashika nguo kuchanika, kwa kuwa walitunyang'anya nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji kwa mabavu, ikabidi tuwaandae vijana wenzetu kuhusu namna ya kukabilisna na uchaguzi Mkuu uliokuwa mbele yetu ili kuhakikisha kwamba Diwani wetu wa CHADEMA anashinda nafasi hiyo.

Licha ya kwamba ilikuwa ndio mara yetu ya kwanza kuwasimamisha wagombea wa CHADEMA ndani ya Kata yetu na Jimboni kwetu tangu Nchi ipate uhuru, lakini nadhibitisha hili hadharani kwamba, Kata yetu ya Nyansurura ambayo mimi ndiye Kiongozi wa Chama mwenye dhamana ya Uenezi, ni miongoni mwa Kata 6 pekee zinazoongozwa na CHADEMA kati ya Kata 28 za Jimbo la Serengeti huko Mkoani Mara.

Jimboni kwetu (Serengeti) nako pamoja na kwamba ndio uliokuwa mwanzo wa kumsimamisha mgombea wa CHADEMA kwa nafasi ya Ubunge, nilikuwa miongoni mwa vijana walioshiriki kikamilifu katika kumpambania mgombea wetu, mpaka hatua ya mwisho. Nafarijika sana kutamka kuwa, pamoja na masahibu mengi tuliyokumbana nayo katika kipindi chote cha uchaguzi, tulifanikiwa kupata kura 19,700 ambazo ni sawa na 41% ya kura zote, ili hali mgombea wa CCM akatangazwa kigumashi kwa 54% ya kura zote, huku mwenzetu wa CUF akipata 5% ya kura zote.

Licha ya kwamba mpaka leo hii sikuwahi kukata au kukatishwa tamaa na mtu yeyote yule, lakini nimeendelea kuwa mwaminifu, mtiifu, mwadilifu, mjukumikaji katika shughuli zote za kichama popote pale zinapotokea ndani ya mipaka ya Nchi yetu, na hata wakati mwingine nimeendelea kuwa msiri sana kwenye mambo muhimu na nyeti ya Chama chetu, tena mambo yanayohitaji vikao maalumu vya Chama ili kuyazungumza, ili kuilinda heshima na hadhi ya Chama chetu, maana ninaamini kuwa wasakatonge watabana sana ila mwisho wao utakapofika wataachia.

Nje ya Jimbo na Katani kwetu, nimekuwa miongoni mwa vijana wenye nia na moyo wa dhati katika kukipigania Chama masaa 24. Ninaendelea kushiriki harakati zote za kukijenga na kukieneza Chama hiki, kila ninapokutana na harakati hizi ndani ya Nchi yetu.

Ninaendelea kushiriki Mikutano mbalimbali ya kukijenga Chama, nimekuwa nikishiriki katika midahalo, matamasha na makongamano mbalimbali yaliyofanyika Nchini kwa ajili ya kutoa elimu kwa watanzania, juu ya mchakato wa Katiba mpya unaoendelea Nchini hivi sasa, mchakato ambao Chama changu ni miongoni mwa Taasisi zinazoitetea Rasmu ya Tume ya Jaji Warioba, yenye maoni ya wananchi yaliyokusanywa kwa mujibu wa Sheria.

Nitaendelea kukitetea, kukijenga na kukilinda Chama hiki kama Mboni ya Jicho, popote nitakapokuwa, iwe ndani au nje ya mipaka ya Nchi yetu.

NITAFANYA NINI NDANI YA BAVICHA TAIFA NA CHAMA KWA UJUMLA

Sote tunatambua kuwa, CHADEMA bila Mabaraza haya ya BAVICHA, BAWACHA na WAZEE tena yaliyo imara, ni sawa na Bunge la Katiba bila Tundu Lissu, Halima Mdee na Jussa Ladhu wa Zanzibar.

Kwa kushirikiana na Viongozi wenzangu wa Baraza na Chama kwa ujumla, tutakwenda kuangalia namna bora ya kukitafutia wigo mpana kitengo hiki cha hamasa Nchini, ili huduma iweze kuwafikia walengwa kwa haraka na wepesi zaidi, tofauti na ilivyo sasa kwa mfano kwamba, mtu wa Uhamasishaji aliyeko Makao Makuu ya BAVICHA Taifa, ndiye atakayefika Songea, Pemba, Mwanza, Tabora, Lindi au Tarime, ndipo huduma ya hamasa iwafikie wananchi wa eneo hilo husika.

Hapa namaanisha nini, namaanisha kwamba, kwenye kitengo hiki cha hamasa ndani ya BAVICHA Taifa, tutafanya ugatuaji wa madaraka kutoka Makao Makuu ya Baraza na kukasimisha mamlaka hayo katika ngazi zote za uongozi wa Chama, kuanzia Taifa, Kanda, Mikoani, ndani ya Wilaya/Majimbo, Kata/Shehia, Matawi na Misingi.

Utaratibu huu mpya nitakaokwenda kuuanzisha,utafanikiwa kwa kutoa elimu kwa watu maalumu watakaoteuliwa na wataalamu wa mafunzo ya Chama kwa kushirikiana na Baraza, ili kusudi, baada ya wao kupata mafunzo hayo kutoka kwa wataalamu wa mafunzo wa Makao Makuu ya Chama, nao watapelekwa kwenye Kanda.

Baada ya watu wa Kanda kupata mafunzo hayo ya Uhamasishaji, nao watapelekwa Mikoani, ili kusaidia kutoa elimu kwa watu wa Wilaya/Majimbo, nao watu hawa wataipeleka elimu hii ya hamasa kwa watu wa Kata zao, na hawa wa Kata watakwenda kutoa elimu ngazi ya Matawi na hawa wa Matawi nao, watatusaidia kuipeleka elimu hii ya hamasa kwa watu wa ngazi ya msingi.

Ndugu zangu watanzania, yapo mengi naamini kwa kushirikiana nanyi, naamini nitayafanya, ila kikubwa zaidi, natambua ni uaminifu, uwazi, uwajibikaji, uadilifu, heshima na utii wa kanuni na taratibu za Chama chetu, zilizoainishwa katika Katiba yetu ya Chama.

Nihitimishe kwa kuwatakia kila la kheri ninyi nyote mnaoendelea na chaguzi za ndani ya Chama, sio tu kwa wale wa ngazi za Wilaya/Majimbo, hata pia ninyi wa chaguzi za ngazi za Mikoa.

Ahsanteni sana!!!

Francis Boniface Marwa, Mgombea wa nafasi ya Mratibu wa Hamasa BAVICHA Taifa 2014. 0785881009/0767881009 01/09/2014. *****************

Aluta Continueeee........
 
Kama kati ya kura 2011 alipata kura 1455 na akashika nafasi ya 6 je walioshika nafasi za 1-5 kila mmoja alipata kura ngapi?

hata me hapo sijaelewa na vile hesabu zinanipiga chenga ndo basi tena
 
Membe ni dhaifu sana kuliko wagombea wote ccm. Anabebwa na familia za wakubwa...anatoa rushwa aliwapeleka baadhi ya viongozi Wa vyio vikuu china, safari ile iliratibiwa na jamaa ambaye alishakuwa kiongozi TAH..SO. Huyu bwana aligombea ubunge akanguka chino pu! Nasikia 2015 anautaka ubunge,lakini nafasi hakubaliki kwenye like jumbo hata kidogo. Haya nayajua vizuri Kwa sababu shughuli za nyingi ziko kwenye maeneo Yale.

Niseme pia Mh.Pinda kutoa kwake machozi hazarani siyo udhaifu. Barani Africa kunaKeneth Kaunda alikuwa na hisia kali,alipotembelea vijijini na kuona umasikini watu wake walionao aliangua kilio. Machozi ya karibu yanadhirisha kiwango cha hisia ya mtu,pamoja na upendo wa kiongozi kwa watu wake.

Pinda ni makini na hili kundi la Mh.Membe linamuogopa sana.Hivi majuzi ulifanyika kikao cha diaspora,walipo sikia kuwa Pinda yupo pale katika harakati zake za kuelekea ofisi kuu ya nchi 2015,waliamua kukimbia mwaliko ule.
 
mimi namjua,anaitwa joka la mdimu,..halili ndimu lakini ukichuma lazime likugonge!


Nyabhingi bwana🙂...Kumbe bado unakumbuka yale maneno ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo Mchinga Ndg. Mundhiri Mundhiri.

Lakini baadae kilichotoea Joka la Mdimu likamshikisha adabu kwa kumtengenezea zinga la kiunzi/zengwe la kufa mtu. Inasemekana Joka la Mdimu lilijenga mkakati wa kumtafuta na hatimaye kupandikiza mpinzani chipukizi wa kumgaraza Mundhiri tu kwenye kura za maoni ile 2010.
Na matokeo yake ubunge wa jimbo Mchinga ukawa historia kwa Mundhiri. Na mpaka leo unaambiwa Mundhiri na Joka la mdimu ni uhasama wa ule wa 'bifu' la kufa mtu kwani ni watu ambao hawatazamani macho kwa macho wala kukutana kwenye hadhara moja huko kwao Lindi, huku Mundhiri akiwa ni majeruhi kwani mdomo ulimponza.
 
Mkuu Sikumbuki kama Bara wameshawahi kutoa rais wa Zanzibar
Hata mimi sikumbuki lini Mzanzibar aliwahi kuwa rais wa Tanganyika. Bali ninachokifahamu sheria isiyoandikwa kuwa urais wa Tanzania ni kupokezana kati ya mtanganyika na Mzanzibar. Hivyo basi huu ni wakati wa Mzanzibar kuwa rais wa Tanzania.
 
Katika uongozi wa sasa, aina ya kiongozi wa kumrithi JK naona bado sijaona anayefaa coz we will need someone who can do a real transformation of how we work.. JK tried but we need someone to take it to the next level..Sasa kwa Membe bado sana!!!


Hapo kwenye nyekundu; huyo Jakaya wako unaesema he tried, my foot what did he try to accomplish? The dude has had no vision during his tenure and only succeeded to log in millions of astronomical miles in the process ballooning our external debt!!! In a sane country the dude could be impeached for abuse of office.
 
Tunataka kiongozi mwadirifu hatutaki watu wanaogombea sababu gesi imepatikana .........

Kama kweli tunataka kiongozi mwadilifu basi sio ndani ya ccm cause huko hayupo hata 1, kwangu mimi nataka kiongozi kwanza kweli awe mwadilifu na mchapa kazi wa kweli na visionary leader na awe mtu mwenye msimamo wa mambo mbalimbali, pia awe mtu wa ku-take action kwa wazembe! Ndani ya ccm mtu wa hivyo sijamuona bado.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…