Baada ya Rostam kulinunua Raia Mwema na kumkabidhi Saed Kubenea limekosa mvuto

Fisadi mzoefu kama rostam aziz akinunua gazeti sio kufanya biashara bali ni kulizima kwa mwelekeo wake usioompendeza au ili kulitimia kutetea wapigaji na sera zao.
 
Hii nchi wachambuzi nguli wa mambo ya siasa nyuma yao huwa kuna sponsor na huwa wanaenda na upepo wa sponsor.

Waandishi wachache wakongwe ndio wamebakia na misimamo tena kile kizazi cha Ulimwengu. Wengine wengi kuna remote nyuma yao. Hiyo remote ikiguswa na serikali matusi yanaanza, wakiwa salama wanageuka praise team.
 
Alieuza Raia Mwema Bw. Generali Ulimwengu hapo mwanzo alikua akimiliki Gazeti la Rai.

Rostam alilinunua pia hili gazeti akamkabidhi Bw. Bashe alisimamie.
 
Mbona anasakama media za mzee ulimwengu!?..Rai na watoto wake alinunua,Leo kanunua na raia mwema!?
 
Biashara ya magazeti ni kama imejifia tu .. kidogo Mwananchi wanajiyutumua, Hawa wengine wanaishi Kwa kijungunjiko
 
Hv kweli, mwanaume mwenzio kwa pesa zake za jasho, anaanzisha kampuni, harafu anakuweka wewe Uwe mkurugenzi, mhariri mkuu,! Hujachangia chochote kwenye kampuni, hujashindana kwenye usaili, unapewa tu kwa kuteuliwa!! Seriously, hii unakuwa kama mke,mama wa nyumbani,kila atakachosema boss wako, utafanya tu! Huna utashi,
Alipolinunua gazeti LA Rai, mkurugenzi mkuu alikuwa Hussein Bashe.
 
Hivi ulimwengu ulivyo mambo mengi kwenye mitandao ya jamii wanapata hela kweli na magazeti yao?
 
Alieuza Raia Mwema Bw. Generali Ulimwengu hapo mwanzo alikua akimiliki Gazeti la Rai.

Rostam alilinunua pia hili gazeti akamkabidhi Bw. Bashe alisimamie.
Hivi gazeti la Rai bado lipo huku duniani kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…