Baada ya tamko lingine la Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania; Je, ni wakati muafaka kwa Serikali kutathimini upya mahusiano yake na taifa hilo?

Baada ya tamko lingine la Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania; Je, ni wakati muafaka kwa Serikali kutathimini upya mahusiano yake na taifa hilo?

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
Tarehe 11/06/2020 Ubalozi wa Marekani umetoa tamko lingine linaloelezea ongezeko la maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 nchini Tanzania, na kuwashauri raia wake kukaa ndani na kuachana na mizunguko isiyo ya lazima. Taarifa hii inafuatia tahadhari mbali mbali ambazo imekuwa ikizitoa tangu ugonjwa huu kufika nchini Tanzania ambazo zilipelekea kaimu balozi wa Marekani nchini Tanzania kuitwa na serikali ya Tanzania na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje. Serikali ya Tanzania ilieleza kusikitishwa na namna Ubalozi wa Marekani umekuwa ukitoa taarifa ya hali ya maambukizi ya ugonjwa huo zisizo sahihi zinazoweza kuzua taharuki kwa Watanzania na wageni kutoka nje ya nchi. Pia serikali ilimtaka kaimu balozi wa Marekani kutoa taarifa zilizothibitishwa na kuwa hakuna kizuizi serikalini kwa mabalozi kupata "taarifa sahihi na zenye ukweli."

Baada ya taarifa hiyo kwa mara mbili mfululizo Ubalozi wa Marekani umeendelea kutoa taarifa zinazokinzana na kauli ya serikali, Rais amehakikishia wananchi wake kuwa ugonjwa umepungua sana na kuwasifu watu wengi anaokutana nao kwa kutokuvaa barakoa, ikiwa ni kielelezo kuwa hali ya hatari ya maambukizi imepungua na inaelekea kuisha Tanzania. Wakati huo huo ubalozi wa Marekani umekuwa ukielezea kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huo hatari na kuwasihi raia wake kusalia ndani ama kuondoka nchini Tanzania mara moja pale usafiri wa ndege utakapopatikana.

Vile vile Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umesema kuwa wakati wowote mlipuko utakapozidi hospitali zetu zitazidiwa na hivyo kuna uwezekano wa Raia wake kukosa huduma kutoka vituo vya afya, lakini Waziri wa Afya amenukuliwa akiwa Dodoma na kusema kuwa hakuna hata mgonjwa mmoja kwenye vituo vingi vya afya walivyokuwa wametenga kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa hao, na kusisitiza yeye mweyewe hajavaa barakoa kwa sababu hali ni shwari. Kuongezea hilo alisema kuwa kuna zaidi ya mikoa 15 ambayo haina wagonjwa wa Corona.

Tumekuwa tukiambiwa na Rais kuwa ugonjwa huu ni vita na mabeberu wamekuwa wakitufanyia hujuma bila kuambiwa hasa mabeberu ni akina nani, lakini kutokana na mkinzano huu inaonekana kabisa wale mabeberu wanaweza kuwa ni nchi ya Marekani. Kama hizi taarifa ubalozi wa Marekani unazotoa kwa kukaidi ushauri wa serikali yetu, je kuna haja gani ya kuendelea kuwabembeleza? Tumekuwa tukiaminishwa kuwa sisi ni nchi tajiri na tuna uwezo wa kusimama wenyewe bila kuyumbishwa na msimamo wa mabeberu, kwa nini serikali isiangalie upya mahusiano na taifa la Marekani? Ikumbukwe nchi ipo katika hatua za kujaribu kunusuru sekta ya utalii na matamko kama haya yanarudisha nyuma juhudi za serikali na wizara yake husika, kwa kupunguza imani kutoka kwa watalii.

Kama serikali ikiendelea kukaa kimya na kuacha ubalozi ufanye unachotaka, tunahatarisha sekta ya utalii na hata wananchi wanaweza kupata taharuki, kwa maana inawezekana taarifa hizi zinaukweli ndani yake, ni wakati muafaka ubalozi wa Marekani kuomba msamaha kwa kutoa taarifa potofu, ama serikali iutake ubalozi kufungashsa virago na kutuachia nchi yetu yenye amani na afya tele. Na kama serikali ikishindwa kukemea matamko haya basi ijitokeze hadharani na kueleza kwa nini inashindwa kukemea uovu huo unaofanywa na mabeberu, pengine taarifa zao ni za ukweli.


EaO8a15WoAEmrEL.jpeg
 
Mtanzania yeyote mwenye akili timamu hawawezi kufuata ngonjera za serikali kuhusu corona. Ukitaka kupoteza maisha kwa Corona fuata uzushi wa "corona imepungua sana".
 
Cannabis,
Yatafuata makubwa. Unajua viongozi wetu ni wajinga mno na wanajiletea mwisho wao wenyewe kwa ujinga wao. Tusubiri tutaona kitu muda si muda.
 
Mtanzania yeyote mwenye akili timamu hawawezi kufuata ngonjera za serikali kuhusu corona. Ukitaka kupoteza maisha kwa Corona fuata uzushi wa "corona imepungua sana".
Bila bila, Corona inawezaje kupungua?
 
Yatafuata makubwa. Unajua viongozi wetu ni wajinga mno na wanajiletea mwisho wao wenyewe kwa ujinga wao. Tusubiri tutaona kitu muda si muda.
fazili, usitishe watu wala hao US hawna muelekeo huo
 
Si wawaondoe raia wao wote wanashindwa nini mpka muda huu wanakua kama CHADEMA MANENO MEEEENGI
 
Gusa ubalozi wa United States of America,or anything connected or owned by them halafu uone kitakachofuata!

Unaongea as if problem in USA

Problem ni nyie msiojua kupambana na covid-19,Kenya na Uganda imewakataa na upumbavu wenu

Haya kata uhusiano na Kenya,Uganda,Zambia,Rwanda,etc and then malizia na USA!

Mnakunya nyie,hamuwezi kua na thinking ushuzi namna hii!
 
fazili, usitishe watu wala hao US hawna muelekeo huo
Sitishi mtu yalishatokea kwa bashite kufungiwa kuingia USA nani alifikiri hata kama USA wanamfuatilia? Wazungu ni tofauti katika utendaji wao, wanafuata kanuni. Wanafuatilia mambo kwa umakini na wanapanga nini cha kufanya. Siwezi kuwatisha watu kwa kuwaambia kuwa mtu asishangae tutakapoona ubalozi unafunga ofisi zake na jiwe anapigwa ban na hata kuanza kufanyiwa ya Saadam na Ghadafi.
 
Sitishi mtu yalishatokea kwa bashite kufungiwa kuingia USA nani alifikiri hata kama USA wanamfuatilia? Wazungu ni tofauti katika utendaji wao, wanafuata kanuni. Wanafuatilia mambo kwa umakini na wanapanga nini cha kufanya. Siwezi kuwatisha watu kwa kuwaambia kuwa mtu asishangae tutakapoona ubalozi unafunga ofisi zake na jiwe anapigwa ban na hata kuanza kufanyiwa ya Saadam na Ghadafi.
Kwa sabau ya corona?
 
Sitishi mtu yalishatokea kwa bashite kufungiwa kuingia USA nani alifikiri hata kama USA wanamfuatilia? Wazungu ni tofauti katika utendaji wao, wanafuata kanuni. Wanafuatilia mambo kwa umakini na wanapanga nini cha kufanya. Siwezi kuwatisha watu kwa kuwaambia kuwa mtu asishangae tutakapoona ubalozi unafunga ofisi zake na jiwe anapigwa ban na hata kuanza kufanyiwa ya Saadam na Ghadafi.
Ban akati jamaa hana hata mpango wa kwenda huko.
 
Kwa sabau ya corona?
Kwani bashite alifungiwa kwenda Marekani kwasababu ya nini? Na wewe bwana unaona corona ni tatizo dogo?... upo kama viongozi wako. Corona inamaanisha kila kitu, uchumi, biashara, na zaidi uhai wa watu. Serikali inapocheza na corona namna hii inamaanisha wageni wanashindwa kufanya biashara na kazi zao. Unaona sasa ubalozi unakuwa kwenye hatari pamoja na mabalozi na wafanyakazi wengine wengi ambao ni raia wa Marekani. Pia hii inaifanya Tz kuwa chimbuko la corona hata pale nchi nyingine zitakuwa zimetokomeza corona. Kwasababu ya corona?...
 
Ban akati jamaa hana hata mpango wa kwenda huko.
Marekani wakitaka kukupiga hawaanzi na makombora, wanaanza na ban kama hizo halafu wanaangalia. Kwa taarifa yenu tu,... hali tayari ni mbaya...japo kwa chini chini na tunakoelekea jiwe asiyesema hakuambiwa...
 
Cannabis,

Mkuu naona unakuza mambo ili kuleta uchochezi kwa maana Tanzania haijawahi kusema hakuna ugonjwa siku zote inasema corona ipo; haijawahi kusema watu wasichue tahadhali siku zote imesema tuchukue tahadhali na hayo ndiyo maneno US inawambia raia wake.
Hakuna nililokuza, hakuna sehemu niliyosema ugonjwa umekwisha ila ubalozi wa Marekani ndio unakuza mambo kwa nini wanasema "The risk of contracting COVID-19 remains high" hii kauli utaona itakavyochukuliwa na wote wanaopingana na hatua ambazo serikali imechukuwa kupambana na hili janga, utaona taarifa kutoka vyombo kama BBC zikianza kumiminika baadaye, hii ni mbaya kwa taswira ya taifa letu. Unajua shida ambazo Wizara ya Maliasili na Utalii wanapitia kujaribu kuleta watalii hapa nchini ?

Kama hali ni mbaya kwa nini viongozi mara nyingi wajisifu na kusifu watu katika mikutano ya hadhara kwa kutokuvaa barakoa ? Huko mtaani kwenu ni watu wangapi wanavaa barakoa ? Ni tahadhari gani hasa zinachukuliwa hivi sasa ? Maisha yanaendelea kama kawaida lakini taarifa hizi za Ubalozi zinakinzana na kauli rasmi kutoka kwa viongozi wakuu wa nchi. Inamaana kama wanachosema ni ukweli, viongozi wetu wameamua kututoa kafara ? Lazima kuwe na uwajibikaji kutokana na kutolewa kwa taarifa kama hii, sio kuikalia kimya. Tanzania ni nchi huru.
 
Sasa kwann wewe ndio unaugua wakati ulitakiwa ufurahie utapata president atakayewekwa na wamarekani?

JPM ukitaka kumkomoa mfanyie ban ya Chato na nchi jirani. Huko USA anaweza asijefika tena. So let then do it.

Wazungu wa wapi makini sana? Ndio maana wako Afghanistan? Na kumuondoa Gaddafi na Saddam. Call it dhulma sio umakini.
Sitishi mtu yalishatokea kwa bashite kufungiwa kuingia USA nani alifikiri hata kama USA wanamfuatilia? Wazungu ni tofauti katika utendaji wao, wanafuata kanuni. Wanafuatilia mambo kwa umakini na wanapanga nini cha kufanya. Siwezi kuwatisha watu kwa kuwaambia kuwa mtu asishangae tutakapoona ubalozi unafunga ofisi zake na jiwe anapigwa ban na hata kuanza kufanyiwa ya Saadam na Ghadafi.
 
Marekani wakitaka kukupiga hawaanzi na makombora, wanaanza na ban kama hizo halafu wanaangalia. Kwa taarifa yenu tu,... hali tayari ni mbaya...japo kwa chini chini na tunakoelekea jiwe asiyesema hakuambiwa...
Hali ni mbaya okay sikupingi,hebu tutanabaishe hali mbaya nyanja gani?
 
Back
Top Bottom