Baada ya vuta nikuvute ya kujaribu kuacha fegi, hatimae kwa sasa nimejinasua kabisa kwenye kifungo cha uraibu wa sigara, ni miezi 6+ siijui fegi

Baada ya vuta nikuvute ya kujaribu kuacha fegi, hatimae kwa sasa nimejinasua kabisa kwenye kifungo cha uraibu wa sigara, ni miezi 6+ siijui fegi

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
7e98077e37.jpg

Nimeanza kuvuta fegi since 2012, fegi ilikuwa daily mara 3 asubuhi, mchana, sometomes jioni na usiku, kila siku, ni mara chache mno niliruka.

Nilikuwa mvutaji wa siri sana, nilikuwa naenda kuvutia maeneo ambayo sijulikani na kweli niliweza kuitunza siri hii mpaka nimeacha hakuna anaejua kasoro wife tu aliewahi kunihisi, ila kuna nyakati tofauti tofauti unakuta ile nataka nianze kuvuta mtu naemjua anapita hio njia na tunasalimiana fresh huku nimeficha mzigo, na nikiona hivyo huo mtaa sirudii tena kuvuta, nahama kabisaa!

addiction ilikuwa sugu, nilikuwa na kigari changu, ikifika usiku naenda sehem flan napaki nafungua dirisha navuta, aisee asikuambie mtubuhitaji ndio mama wa ubunifu, kipindi cha mvua nilinununua kopo la maji makubwa nikanywa kidogo nikamwaga, nikalikata lile kopo mkono uwe unaingia pamoja na fegi ili hata mvua ikipiga isizime fegi.

kila baada ya kuvuta nilinunua pipi kali na kupiga mswaki, nilipulizia ka perfume, nilikiwa, nimetumia hela sana kununua hizi perfume na pipi.

basi mwezi wa 10 mwaka jana baada ya attempts kama 3 za nyuma kujaribu kuacha na kurudi, niliamua tu kwamba siitaki sigara, na mda huo nilikuwa navuta sababu ya mazoea tu, nilikuwa sipati kabisa ile buzz.

Mambo yalionifanya niache nilianza kufatilia sana documentaries za cancer vile naona watu wanahangaika na hadi wengine wanatolewa makoo, Pia nikawa naona nifanye sababu ya watoto wangu walau nijitunze tunze, lakini pia nilikiwa sipati kabisa vistimu hata kidogo muda huo, yani ilikuwa navuta basi tu ni mazoea.

Kwa wale mtaofananisha Bangi na sigara, jibu fupi ni kwambaunaweza kuacha bangi kirahisi na wengi wameweza lakini sigara ni ishu nyingine aisee, ile nicotine ya sigara ikiizoea mwili ni mtihani.

As of now nina miezi 7 sasa and i am so happy.
 
Hongera mkuu jitahidi usirudi maana ukirudi addiction yake inakuwa mara mbili yke
 
Hamia kwenye bangi... Thanks me later
Ni rahisi mno kuacha bangi kuliko sigara, nicotine ya sigara ni mziki mwingine ule.

Alafu bangi umri ukienda unakuta ile circle ya watumiaji inapungua, ni kilevi ambacho unakuwa free zaidi kukitumia kwenye 20's ila zaidi ya hapo ule uhuru, kampani, kununua, n.k. inaanza kuwa ngumu, unajikuta umeacha tu wengi hapa wanhamiaga kwenye pombe.
 
Endelea kumwomba mungu kuna wenzio waliacha zaidi ya miez 28+ na wakarudia tena...na imekua rahisi kwako kuacha kwakua umekua ukivuta kwa kujificha,hukujiamini...
 
Hongera mkuu

Epuka kuwa maeneo yanayoshawishi kuvuta 🚬 ili usirudie uvutaji.
 
Mimi navuta bange plus sigara asee najitajidi kuacha wapi ..mwenye kuweza nishauri Cha kufanya ..tiririka hapa.
 
Mimi navuta bange plus sigara asee najitajidi kuacha wapi ..mwenye kuweza nishauri Cha kufanya ..tiririka hapa.

Anza kwa kupunguza taratibu kama ulikuwa unavuta 5 kwa siku weka 3 kwa muda wa mwezi mmoja, then punguza mpka 1 kwa siku kwa miezi 2 then hamia kwa kuvuta sigara 1 kwa wiki.

au nenda kanywe mafuta ya upako ya bulldozer kuna mwan jirani kila akivuta fegi anatapika kwasababu mke wake alimwekea mafuta ya upako kweny msosi
 
Hongera sana mkuu, ingawa siamini kama ilikuwa addicted kiivyo kwako nimeangalia hata interval ya uvutaji wako kwa siku bado ilikuwa ni namba ndogo (three times a day?)

Hivi ushawahi kukaa na mtu akipata chance ya kwenda chooni tu lazima ashtue ?? 😂 kuna wale wana akisikia harufu apo lazima alipue.
Wakati wa College kulikuwa na professor wetu mmoja kipindi cha 2hrs anaweza kuwapa hata breaks mara nne ili mradi atoke kuwashaa 😂 na unaona kuna mda mpaka mikono inamtetemeka ubaoni.

I used to be a cigarette smoker na uvutaji wangu haswaa ulikuwa wakati wa kunywa au nikiwa nimesizi na herbs 🌿 nikianza kupiga safari mbili tatu lazima nianze kuwasha baadae mazoea yakazaa tabia ikawa lazima nikitembea niwe na pakti la “embanga” ubalozi nimeuweka kwenye mfuko wa shati, over 5 yrs nikaja kuona haikuwa vitu vyangu ila ni ile mob na kujaribu kufit in, nikaamua kuachana nayo. Haikuwa issue kubwa course haikuniingia kama wanangu na njia kubwa ninayoitumia ni kuvuta sanaa “Herbs” imenisaidia. Ila shida nikiwa sober na hakuna herbs 🌿 hapo lazima nichome.
 
Back
Top Bottom