Pre GE2025 Baada ya Wananchi kugomea t-shirt na fedha za Kawawa, ajitokeza na kusema hizo ni fitna za Kisiasa na kuwa wanaichafua CCM

Pre GE2025 Baada ya Wananchi kugomea t-shirt na fedha za Kawawa, ajitokeza na kusema hizo ni fitna za Kisiasa na kuwa wanaichafua CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Siku chache baada ya baadhi ya Wananchi kumjia juu Mbunge wao wa Jimbo la Namtumbo, Vita Rashid Kawawa, ameamua kujibu.

Wananchi wao wa Kijiji cha Mlalamiwa na Matepwende waligoma kupokea zawadi za Mbunge wao ambazo ni fulana na fesha kwa madai kuwa hawawezi kufanya hivyo wakati huduma mbalimbali za Kijamii hazijaimarika.

Akizungumza na Wanachama wa CCM Wanawake jimboni hapo, ambapo imeeleza kulikuwa na Baraza la UWT Wilaya, Vita Rashid Kawawa amedai anachafuliwa na wanaofanya hivyo hawamchafui yeye peke yake bali wanachafua chama chake cha CCM.

Pia soma ~ Wananchi wa Vijiji viwili Jimbo la Namtumbo warudisha t-shirt na fedha za Mbunge wao Vita Kawawa!
 
Haya sawa kwa hiyo tuhuma ni za uongo zote huruma wanazo lalamikia zipo asilimia mia
 
Homera Anafanya haya, kafungua mpaka kituo cha redio kwaajili ya kampeni, ACHA WAUWANE.
 
Hao jamaa wanapitia wakati mgumu mno kuliko nyakati zote #muda usema ukwelii wakati wote..
Haya maisha kila mtu ana msalaba wake ... hakika asiye fanya kazi na asile... dunia uwanja wa mapambano...
 
  • Thanks
Reactions: PFA
Siku chache baada ya baadhi ya Wananchi kumjia juu Mbunge wao wa Jimbo la Namtumbo, Vita Rashid Kawawa, ameamua kujibu.

Wananchi wao wa Kijiji cha Mlalamiwa na Matepwende waligoma kupokea zawadi za Mbunge wao ambazo ni fulana na fesha kwa madai kuwa hawawezi kufanya hivyo wakati huduma mbalimbali za Kijamii hazijaimarika.

Akizungumza na Wanachama wa CCM Wanawake jimboni hapo, ambapo imeeleza kulikuwa na Baraza la UWT Wilaya, Vita Rashid Kawawa amedai anachafuliwa na wanaofanya hivyo hawamchafui yeye peke yake bali wanachafua chama chake cha CCM.

Pia soma ~ Wananchi wa Vijiji viwili Jimbo la Namtumbo warudisha t-shirt na fedha za Mbunge wao Vita Kawawa!
Kukataa zawadi ni kumchafua mtu?
 
Mbunge wa Jimbo la Namtumbo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Vita Kawawa, ameainisha mafanikio ya miradi ya maendeleo iliyotekelezwa katika jimbo lake kwa kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake huku akitoa wito kwa wanaotamani kugombea nafasi yake kusubiri hadi Julai 2025 ili kumpa nafasi ya kumaliza kazi aliyoianza.

Kawawa ameyasema hayo wakati akihutubia wananchi wa Kata ya Ligera Tarafa ya Sasawala wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma amesema kuwa ni muhimu azungumzie miradi mbalimbali ya maendeleo aliyoifanya kwa sababu watu wameanza kumchafua kana kwamba CCM na serikali yake haijafanya kitu. Ameeleza kuwa serikali imewekeza mabilioni ya shilingi katika sekta za afya, elimu, na miundombinu kwa manufaa ya wakazi wa Namtumbo.

Mbunge Kawawa amebainisha kuwa serikali imejenga Kituo cha Afya katika Kata ya Ligera kwa gharama ya shilingi milioni 500, pamoja na kuleta vifaa tiba. Amesema juhudi hizi ni sehemu ya mpango wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan wa kuboresha huduma za afya kwa akina mama, watoto, na wazee.

"Kama Mbunge, mimi nawajibika kuwasilisha changamoto za wananchi kwenye ngazi ya taifa, ambapo fedha za miradi kama vituo vya afya na zahanati hutolewa," amesema Kawawa.

Katika sekta ya elimu, Mbunge Kawawa ameeleza kuwa shule mpya ya msingi imejengwa katika Kijiji cha Mtelawamwahi kwa gharama ya shilingi milioni 360. Pia, shule ya msingi Lukimwa imepata madarasa mapya na maabara, huku bweni likikamilishwa kwa msaada wa mifuko ya saruji 100 na fedha za serikali kiasi cha milioni 30.

Kwa shule ya msingi Ligera, shilingi milioni 59 zilitumika kujenga madarasa mawili na vyoo, huku shule ya Njomlole ikipokea milioni 46 kwa ajili ya madarasa mawili na milioni 4 kwa ukarabati.

Kuhusu barabara, Kawawa amesema mvua zinazoendelea kunyesha zimeathiri miundombinu, lakini fedha za kuweka kifusi tayari zimetengwa na kazi itaanza mara fedha hizo zitakapoingia.

Mbunge huyo amezungumzia changamoto ya maji katika Kata ya Ligera, akieleza kuwa juhudi za kuchimba kisima kirefu katika eneo la Namahoka zilikumbwa na matatizo ya vifaa vya kuchimba kutumbukia shimoni. Hata hivyo, juhudi zinaendelea kutafuta eneo mbadala kwa ajili ya mradi huo.

Kawawa amewataka wananchi kupuuza maneno ya wapinzani na kuendelea kumuunga mkono, akisema kazi kubwa ya maendeleo inaendelea kufanyika.

"Wananchi wasikubali kurubuniwa na madalali wa siasa, bali wasubiri muda ufike kwa ajili ya uchaguzi," amesema.

Stawa Ndauka, mkazi wa Ligera, amesema wanaridhishwa na juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na Mbunge Kawawa, hasa katika huduma za afya, elimu, na miundombinu.
 

Attachments

  • Screenshot_20250126-132124.png
    Screenshot_20250126-132124.png
    477.3 KB · Views: 4
Anawazungumziaje madalali waliopiga usanii kwa miaka zaidi ya sitini na wengine wapo Namtumbo wanaendeleza uongouongo muda huu?
 
Mbunge wa Jimbo la Namtumbo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Vita Kawawa, ameainisha mafanikio ya miradi ya maendeleo iliyotekelezwa katika jimbo lake kwa kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake huku akitoa wito kwa wanaotamani kugombea nafasi yake kusubiri hadi Julai 2025 ili kumpa nafasi ya kumaliza kazi aliyoianza.

Kawawa ameyasema hayo wakati akihutubia wananchi wa Kata ya Ligera Tarafa ya Sasawala wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma amesema kuwa ni muhimu azungumzie miradi mbalimbali ya maendeleo aliyoifanya kwa sababu watu wameanza kumchafua kana kwamba CCM na serikali yake haijafanya kitu. Ameeleza kuwa serikali imewekeza mabilioni ya shilingi katika sekta za afya, elimu, na miundombinu kwa manufaa ya wakazi wa Namtumbo.

Mbunge Kawawa amebainisha kuwa serikali imejenga Kituo cha Afya katika Kata ya Ligera kwa gharama ya shilingi milioni 500, pamoja na kuleta vifaa tiba. Amesema juhudi hizi ni sehemu ya mpango wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan wa kuboresha huduma za afya kwa akina mama, watoto, na wazee.

"Kama Mbunge, mimi nawajibika kuwasilisha changamoto za wananchi kwenye ngazi ya taifa, ambapo fedha za miradi kama vituo vya afya na zahanati hutolewa," amesema Kawawa.

Katika sekta ya elimu, Mbunge Kawawa ameeleza kuwa shule mpya ya msingi imejengwa katika Kijiji cha Mtelawamwahi kwa gharama ya shilingi milioni 360. Pia, shule ya msingi Lukimwa imepata madarasa mapya na maabara, huku bweni likikamilishwa kwa msaada wa mifuko ya saruji 100 na fedha za serikali kiasi cha milioni 30.

Kwa shule ya msingi Ligera, shilingi milioni 59 zilitumika kujenga madarasa mawili na vyoo, huku shule ya Njomlole ikipokea milioni 46 kwa ajili ya madarasa mawili na milioni 4 kwa ukarabati.

Kuhusu barabara, Kawawa amesema mvua zinazoendelea kunyesha zimeathiri miundombinu, lakini fedha za kuweka kifusi tayari zimetengwa na kazi itaanza mara fedha hizo zitakapoingia.

Mbunge huyo amezungumzia changamoto ya maji katika Kata ya Ligera, akieleza kuwa juhudi za kuchimba kisima kirefu katika eneo la Namahoka zilikumbwa na matatizo ya vifaa vya kuchimba kutumbukia shimoni. Hata hivyo, juhudi zinaendelea kutafuta eneo mbadala kwa ajili ya mradi huo.

Kawawa amewataka wananchi kupuuza maneno ya wapinzani na kuendelea kumuunga mkono, akisema kazi kubwa ya maendeleo inaendelea kufanyika.

"Wananchi wasikubali kurubuniwa na madalali wa siasa, bali wasubiri muda ufike kwa ajili ya uchaguzi," amesema.

Stawa Ndauka, mkazi wa Ligera, amesema wanaridhishwa na juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na Mbunge Kawawa, hasa katika huduma za afya, elimu, na miundombinu.
Hapo anaongea na wana ccm si wananchi. Mbunge kama hujafanya lolote there is no hiding
 
Hajazungumzia harakati za RC wa Mbeya Juma Homera kutaka kumnyang'anya jimbo?
 
Mbunge wa Jimbo la Namtumbo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Vita Kawawa, ameainisha mafanikio ya miradi ya maendeleo iliyotekelezwa katika jimbo lake kwa kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake huku akitoa wito kwa wanaotamani kugombea nafasi yake kusubiri hadi Julai 2025 ili kumpa nafasi ya kumaliza kazi aliyoianza.
Watu wameamka aache ujinga
 
Back
Top Bottom