Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 20,137
- 26,189
Ama kweli majumba makubwa hustiri mambo hii kauli kwa namna fulani inashibahiana na hali inayomkuta sasa msanii Enock Bella
Huyu kijana kipindi yupo yamoto band aliwahi kutamba sana na sauti yake nzito na tungo tata zilizowachanganya vilivyo akina dada.
Mwanzoni huyu kijana alikuwa ni dancer tu wakawaida ila mkubwa fella akatumia kila aina ya ushawishi ili huyu jamaa naye aimbe kama wenzake kwenye kundi na akamsifia vilivyo kwamba sauti yake itaziba pengo la marehemu Muhiddin Gurumo lakini siku zote bwana mtu kama huna kipaji huna tu hata ufanye nini.
Alipokuwa Yamoto alijificha nyuma ya wenzake na kuimba maneno mawili matatu na hakuweza kugundulika kirahisi kwamba jamaa ni debe tupu ila tangu kundi livunjike huyu jamaa ana hali mbaya sana kimuziki na hilo limejidhihirisha mara baada ya kutoa wimbo kama solo artist uitwao Sauda.
Aisee huu wimbo ni mbaya mbaya mbayaa kupita maelezo hausikiliziki hauchezeki kwa kifupi hauvutii kabisa au kwa maneno mengine naweza kusema huu ndio wimbo mbovu zaidi kwa mwaka huu 2017/2018.
Jamaa bora aangalie tu ustaarabu mwengine mziki hawezi.
Huko IG watu wachache wamejitokeza kumsapoti lakini wapi ngoma haisapotiki ,imedoda.
Pole sana Enock Bela tafuta kazi nyingine tu huku kwenye mziki unatukera huna ulichobakiza.
Huyu kijana kipindi yupo yamoto band aliwahi kutamba sana na sauti yake nzito na tungo tata zilizowachanganya vilivyo akina dada.
Mwanzoni huyu kijana alikuwa ni dancer tu wakawaida ila mkubwa fella akatumia kila aina ya ushawishi ili huyu jamaa naye aimbe kama wenzake kwenye kundi na akamsifia vilivyo kwamba sauti yake itaziba pengo la marehemu Muhiddin Gurumo lakini siku zote bwana mtu kama huna kipaji huna tu hata ufanye nini.
Alipokuwa Yamoto alijificha nyuma ya wenzake na kuimba maneno mawili matatu na hakuweza kugundulika kirahisi kwamba jamaa ni debe tupu ila tangu kundi livunjike huyu jamaa ana hali mbaya sana kimuziki na hilo limejidhihirisha mara baada ya kutoa wimbo kama solo artist uitwao Sauda.
Aisee huu wimbo ni mbaya mbaya mbayaa kupita maelezo hausikiliziki hauchezeki kwa kifupi hauvutii kabisa au kwa maneno mengine naweza kusema huu ndio wimbo mbovu zaidi kwa mwaka huu 2017/2018.
Jamaa bora aangalie tu ustaarabu mwengine mziki hawezi.
Huko IG watu wachache wamejitokeza kumsapoti lakini wapi ngoma haisapotiki ,imedoda.
Pole sana Enock Bela tafuta kazi nyingine tu huku kwenye mziki unatukera huna ulichobakiza.