Baadhi Wakenya wa Mombasa, jameni acheni ukaidi, mtanasa kwenye siasa za Tanzania kichwa kichwa

Baadhi Wakenya wa Mombasa, jameni acheni ukaidi, mtanasa kwenye siasa za Tanzania kichwa kichwa

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Nimeona baadhi ya Wakenya wa Mombasa wakitishia kugoma kupimwa Corona na kutolea mifano ya Tanzania ambako matikiti maji, mapaipai n.k. zinapmwa na kukutwa na Corona.

Ndugu zangu Wakenya, muhimu tuchangamkie hili zoezi la "mass testing" ambalo linaendelea, tupange foleni na kupimwa kila mmoja wetu, binafsi nakusudia kupima Jumapili ijayo, acheni kuingia kwenye siasa za Tanzania kichwa kichwa, ifahamike wale wamesalia na miezi michache kabla kuingia kwenye uchaguzi mkuu, hivyo kila kitu kwao kwa sasa kinapelekeshwa kwa milengo, mitazamo na misimamo ya kisiasa, hata janga kama hili ambalo ni hatari kwa dunia, ukipitia majukwaa yao ya kisiasa na mitandao ya kijamii, wanajadili hiki kirusi kwa mihemko ya kisiasa.

Tikitaka zao za mananasi, mapaipai oili ya gari n.k. visisababishe tususie hii shughuli kwetu, muhimu tukafahamu juzi tumeona CDC wametolea takwimu za Tanzania kwamba huko hadi sasa wamepima watu 652 pekee yake na kupata idadi ya walioambukizwa kuwa 480, hiyo inaonyesha uwezekano wa kwanini mkulu wao ana hasira, angalia hotuba zake zimejaa hasira balaa.

Ukipitia majukwaa yao ya kisiasa humu JF, nyuzi za tanzia huibuka kila siku, mara waziri kadondoka na kufariki, mara mbunge, pia tunona wanavyotupia video na mapicha ya mambo yanayotendeka kwao, ukikumbuka RC wa Dar mwenyewe aliwahi kunukuliwa akitahadharisha watu wa mikoani wasije Dar maana huko wanapukutika kama majani, ni mwendo wa mazishi.

Jameni jameni chonde chonde Wakenya muhimu tukafahamu kwamba kwa kupimwa na kujua hali yako, itakusaidia kuwalinda uwapendao, inawezekana wewe ukawa na uwezo mkubwa wa kupambana na kirusi, lakini pia ukawaambukiza familia yako na kuwazika kadhaa, ujikute unamzika mkeo au mumeo, au mwanao, hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kujua hali yako kama ilivyo kwa UKIMWI, pima pima pima, hata ikiwezekana kila wiki pima mara moja maana sasa vipimo vimeshaingia mtaani, ushindwe wewe tu.

Pia natoa wito kwa serikali, itie jitihada za kuhakikisha inagharamikia siku ambazo Wakenya wanaishi kwenye karantini, kama vipi mteue shule kadhaa za bweni na kuzigeuza vituo vya karantini, kisha turuhusiwe kuwaletea wapendwa wetu vyakula ili kupunguzia gharama, mjiongeze kimikakati ili Wakenya wachangamkie hili zoezi.

Halafu mheshimiwa Joho gavan wa gatuzi 001, natoa rai achana kabisa na mikwara kwa watu wako wa Mombasa, hasira hazitosaidia kitu, waelimishe taratibu, kama kunao wapambe wa huyu gavana humu, jaribuni kumshauri hili zoezi halitafaulu kwa kutumia hisia kali, Wakennya sio kama Wabongo ambao kule kwao wakikaripiwa na mkulu wanaufyata wote mpaka hata Corona yenyewe inaingia mitini, kwa Wakenya ukiwajia kwa hasira ndio utakua unawapandisha full mzuka na utashindwa kuwatawala au kuwaelekeza.

Naona Watanzania wameanzisha nyuzi za kujiliwaza kuhusu hili

Magufuli aistua Dunia kuhusu vipimo fake vya Corona!, Mombasa wagomea kupima Corona, wamtaja Magufuli amesaidia kustuka, wathibisha JPM is Right!. - JamiiForums

 
MK254,

Hivi kulikua na umuhimu gani wa kuizungumzia na kuikebehi Tanzania kwa kihasi hiki katika huu Uzi?.

Wale wakenya wenye kulalamika kwamba watanzania tunaishambulia Kenya Mara kwa Mara bila sababu wakati wakenya hawana habari na Tanzania mpo wapi?.

Mara nyingi Tanzania tunaishambulia Kenya kama kulipiza mapigo, ila tunajibu kwa nguvu zaidi ya ninyi, ndio sababu mnahisi tunaichukia Kenya. Mkiendelea kutuchokonoa tutawajibu kwa nguvu zote.

cc. Tony254
Sinister
Mwaswast
Geza Ulole
Game over

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We unadhani ukipima ndo unakuwa salama!!!!

Be reasonable kijana acheni kuiga iga

Elimika acha kukurupuka, unapima ili uweze kuwalinda uwapendao, sio kila mmoja wetu ana uwezo wa kuhimili hiki kirusi, hivyo ukigundua unacho kabla kuanza kutema mbegu kila mahali, utajaribu namna za kujizuia aidha ujifungie ndani na kutoruhusu yeyote kukukaribia.
Tusipokua makini tutaanza kuona video kama hizi za Tanzania

 
Elimika acha kukurupuka, unapima ili uweze kuwalinda uwapendao, sio kila mmoja wetu ana uwezo wa kuhimili hiki kirusi, hivyo ukigundua unacho kabla kuanza kutema mbegu kila mahali, utajaribu namna za kujizuia aidha ujifungie ndani na kutoruhusu yeyote kukukaribia.
Tusipokua makini tutaanza kuona video kama hizi za Tanzania

ujinga nayo,Apo sio semunge
 
Hivi kulikua na umuhimu gani wa kuizungumzia na kuikebehi Tanzania kwa kihasi hiki katika huu Uzi?.

Wale wakenya wenye kulalamika kwamba watanzania tunaishambulia Kenya Mara kwa Mara bila sababu wakati wakenya hawana habari na Tanzania mpo wapi?.

Mara nyingi Tanzania tunaishambulia Kenya kama kulipiza mapigo, ila tunajibu kwa nguvu zaidi ya ninyi, ndio sababu mnahisi tunaichukia Kenya. Mkiendelea kutuchokonoa tutawajibu kwa nguvu zote.

cc. Tony254
Sinister
Mwaswast
Geza Ulole
Game over

Sent using Jamii Forums mobile app
Bwana wao anaondoa lock down




Ngoja tuone kaharisha nani Kunyaland itafanya nini!
 


MY TAKE
grapevine news say the young girl succumbed to coronavirus that deliberately been claimed accident! May her soul RIP!

Now they say she fell the cause of falling at this moment?? coronavirus!

 
mombasa wanakaa binadamu wenye kufikiri,kama ambavyo wanaweza kuwepo wengine sehemu nyingine kenya.kwanini uwapangie cha kufikiri!!!!

mmewekeza bidii katika kujua idadi ya wagonjwa,wakati dawa ya kutibu haipo.mnabeza juhudi zetu za kienyeji katika kujaribu kupambana na huu ugonjwa.

yaani ni kama mnataka mpate wa kuwafungia ndani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mombasa wanakaa binadamu wenye kufikiri,kama ambavyo wanaweza kuwepo wengine sehemu nyingine kenya.kwanini uwapangie cha kufikiri!!!!

mmewekeza bidii katika kujua idadi ya wagonjwa,wakati dawa ya kutibu haipo.mnabeza juhudi zetu za kienyeji katika kujaribu kupambana na huu ugonjwa.

yaani ni kama mnataka mpate wa kuwafungia ndani.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sasa hivi hairuhusiwi watu kukaidi ushauri wa kitaalam, jua hali yako ili ujizuie kutema mbegu, uzuie kuwaambukiz ndugu na jamaa, ukishajua hali yako utaacha kutangatanga....
 
KunyaLand mmekubali kuwa watumwa wa kichina ndo maana juzi wachina waliwacharaza vibiko laia wenu na hamwezi kuwafanya lolote...Bandari inabebwa na wachina, sgr nayo inasepa Kwa sababu mnakubari kizembe kuwa watumwa simply because hamtaki kujisimamia kama Taifa huru lenye misingi na utaratibu wake.KunyaLand badilikeni Bana sio kila kitu mnacopy na kupest from Western.
China is selling fear globerly at the end they vaccine every one who agrees....and KunyaLand will be namba one.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KunyaLand mmekubali kuwa watumwa wa kichina ndo maana juzi wachina waliwacharaza vibiko laia wenu na hamwezi kuwafanya lolote...Bandari inabebwa na wachina, sgr nayo inasepa Kwa sababu mnakubari kizembe kuwa watumwa simply because hamtaki kujisimamia kama Taifa huru lenye misingi na utaratibu wake.KunyaLand badilikeni Bana sio kila kitu mnacopy na kupest from Western.
China is selling fear globerly at the end they vaccine every one who agrees....and KunyaLand will be namba one.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sio fear, watu wanakufa kote, ipo na inatendeka, acheni ukaidi na kufukia vichwa ardhini, muhimu kupima ujue hali yako ili uwalinde uwapendao, ukae mbali nao......
 
Tukinyoosha mpaka pale ulipopinda mombasa ni tz.

Kilimanjaro irudi kwetu kwanza ndio tuongee mengine...hehehehe!! Na hata Mombasa ikituacha labda apewe Sultani wa Zanzibar sio kumkabidhi Msukuma, na huyo Sultani lazima aje atuambie hii Afrika kabla hajaja ina maana hakuwakuta watu....
 
Back
Top Bottom