#COVID19 Baadhi ya mafundi tuliojenga miradi ya UVIKO-19 (hasa madarasa) tunanyanyaswa sana

#COVID19 Baadhi ya mafundi tuliojenga miradi ya UVIKO-19 (hasa madarasa) tunanyanyaswa sana

mwanga mweusi

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2020
Posts
276
Reaction score
452
Niseme kwamba mafundi tuliojenga majengo haya ya uviko hasa madarasa tumeteswa sana na bado tunateseka sana.

Kwa hii wilaya niliyopo tuliingia mkataba na serikali kujenga haya majengo tukakubaliana bei na kamati ya kujenga madarasa yakamilike kwa muda japo muda ulikua mdogo sana yani wiki 3 ukamilishe mradi mkurugenzi akaongeza muda wa siku 15.

Kimbembe kikaza pale mkuu wa mkoa alipopanga ratiba ya kutembelea huku tukaambiwa kazi usiku na mchana hakuna miundombinu yakuwezesha kazi kufanyika usiku mkuu wa wilaya hataki kuelewa hilo mkuu wa shule nae anakwambia kanunue sola umalize kazi yako mkuu akaagiza tuwekwe sero yani hapa ndipo niliona ugumu wa kazi za serikali.

Kwenye umaliziaji bado mambo yalikua magumu vifaa hamna wakubwa wanataka kazi iishe hadi kutishiwa kunyang'anywa kazi ukicheki ushapiga plasta tail body bado kuskim poda hamna unyang'anywe kazi kweli.

Engineer anataka kazi yake iwe hivi mkuu wa shule anasema fanya hivi sababu hela ya kununua vifaa hamna ukiwaandikia barua wanasema tutatumia pesa yako ya ufundi ubaki unatudai fundi unabaki upo katikat unashindwa chakufanya malipo hayapitishwi bila kutoa rushwa kwa kamati watakuja na mambo kibao.

Tumemaliza kazi hadi leo tarehe 3/3/2022 hakuna anaetujali tena tumepitia shida nyingi lakini toka tumalize kazi tuna karibu miezi 2 hatuja kaguliwa ili malipo yafanyike na wala hakuna mtu anaefwatilia kil mtu na mambo yake tunao umia ni sisi tupo mashuleni huku kama watumwa hadi mkuu wa shule ananiambia ili anipitishie malipo nifagie nje ya majengo wakati wanafunzi ndio wanatupa matakata huko.

Nasikia kuna mwingine amejenga kiwere amepigishwa deki tena la chuma mboga lile la kusimama ni kwajili ya wanafunzi [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hela yenyewe nabaki nayo laki 3 nyingine nilip madeni lakini hawajua wanajua ni yangu yote wanataka hela. ningekua sidaiwi ningeacha nirudi nyumbani nikahudumie familia yangu.

Dahh ukitaka kufa kabla ya muda fanya kazi za serikali huku sikonge.

TUNAOMBA MSAADA WENU JAMANI.

Mimi sio mwandishi mzuri ila anaejua machungu nayopitia ni Mungu asanteni
 
Usifanye na serikali

Way back nikiwa shule ya bweni wazabuni walikuwa wanasumbuliwa sana.kwenye malipo yao baada ya kuleta msosi

Matokeo mnakula hamshibi au msosi mbaya

Vivyo hivyo ofisi zingine ukifanya kazi na ofisi ya serikali tegemea maumivu maana maamuzi hayafanywi na mtu mmoja tena hadi wakae kikao.

Ndio cheki iandikwe.
 
Mkuu nikweli kabisa kifupi fosi akaunt ingefutwa kabisa majengo hayana ubora kamati yote inataka rushwa ndio ulipwe yani acha tu ni usumbufu wa hatari unaweza pata presha
 
Mkuu nikweli kabisa kifupi fosi akaunt ingefutwa kabisa majengo hayana ubora kamati yote inataka rushwa ndio ulipwe yani acha tu ni usumbufu wa hatari unaweza pata presha
Kwa walio pitia huku wanaelewa sana mmbo yalivyo
 
Ungekuwa foreigner ungeshalipwa hela yako.

Ila kwakuwa ni mtanzania, imekula kwako.
 
Niseme kwamba mafundi tuliojenga majengo haya ya uviko hasa madarasa tumeteswa sana na bado tunateseka sana.

Kwa hii wilaya niliyopo tuliingia mkataba na serikali kujenga haya majengo tukakubaliana bei na kamati ya kujenga madarasa yakamilike kwa muda japo muda ulikua mdogo sana yani wiki 3 ukamilishe mradi mkurugenzi akaongeza muda wa siku 15...
Serikalini kumejaa majizi yenye vitisho na nguvu kubwa
 
Kati ya watu wanao nyanyasika kwenye taaluma yao ni mafundi kwa ujumla.

Fundi hana thamani baada yakazi kuisha.
 
Back
Top Bottom