KERO Baadhi ya Migahawa ya Ifakara Mjini haizingatii usafi, Mamlaka zinazohusika ziingie mtaani kufuatilia

KERO Baadhi ya Migahawa ya Ifakara Mjini haizingatii usafi, Mamlaka zinazohusika ziingie mtaani kufuatilia

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mwanongwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2023
Posts
611
Reaction score
567
WhatsApp Image 2025-01-23 at 12.17.43_ed7f486c.jpg
Habari ndugu zangu wa jukwaa hili ambalo limekuwa sauti Kwa wasiyo sikika.

Ndugu yenu katika pitapita zangu nikajikuta nimeibukia Wilayani Kilombero Mkoa wa Morogoro, nilichokutana nacho kwa baadhi ya Mama Lishe ni hali ambayo inaweza kuwa hatari sana kwa afya za Watu.

Mama Lishe wa Ifakara maeneo ya Mjini hasa Mtaa wa Nduna hawazingatii usafi jambo ambalo linaweza kuwa na athari katika kuchangia maambukizi ya magonjwa ya tumbo pamoja na Kipindupindu, pia mazingira.

Nilichobaini ni kuwa wengi wao hawana vifaa vya usafi, vyombo ambavyo vinatumiwa kwa ajili ya chakula vinawekwa katika mazingira machafu, sehemu zao za kupikia pia hazijasafishwa.

Wakati hali ikiwa hivyo, Uongozi wa Halmashauri naona wapo kimya kama hawaoni vile kinachoendelea, mpaka magonjwa ya mlipuko yatokee ndiyo wataanza kuhaha kusimamia usafi wa Migahawa hiyo.

Tukumbuke hivi karibuni wenzao wa Mbeya wamekuwa na wakati mgumu kama ilivyo kwa Simiyu kutokana na Kipindipindu, wanasema mwenzako akinyolewa...

Mwanongwa nawakumbusha tu kinga ni Bora kuliko tiba.
WhatsApp Image 2025-01-23 at 12.17.43_81cc8f44.jpg

WhatsApp Image 2025-01-23 at 12.17.43_e225a199.jpg
 
Sio ifakara tu,,,,mama lishe karibia wote sio wasafi na mazingira kwa ujumla ni machafu sana !
Cha kufanya nenda kale sehemu unapoona ni hadhi yako ,,,, walau kwa mlo mmoja uwe na kuanzia 5000 kwa restaurant zenye hadhi ya kati, je ni wangapi wanaweza ku-afford wali tu alipe kaki ??

Huko kwa buku buku kunaokoa sana, kila mtu ana kipato chake , watu hawafanani !!
 
Picha linaanza anaesave anaepron chafu alafu anakitoto kidogo mgongoni..jagi la maji ya kunywa na chumvi iko mezani nzi wamejaa ugali na wali umefungwa kwenye nailoni ndani ya sufuria ili kisipoe..inahitaji moyo kuyakubali hayo mazingira otherwise uwe mjamzito au unakipato duni utaendana na kasi ya uchafu wa mazingira ya mama ntilie
 
Habari ndugu zangu wa jukwaa hili ambalo limekuwa sauti Kwa wasiyo sikika.

Ndugu yenu katika pitapita zangu nikajikuta nimeibukia Wilayani Kilombero Mkoa wa Morogoro, nilichokutana nacho kwa baadhi ya Mama Lishe ni hali ambayo inaweza kuwa hatari sana kwa afya za Watu.

Mama Lishe wa Ifakara maeneo ya Mjini hasa Mtaa wa Nduna hawazingatii usafi jambo ambalo linaweza kuwa na athari katika kuchangia maambukizi ya magonjwa ya tumbo pamoja na Kipindupindu, pia mazingira.

Nilichobaini ni kuwa wengi wao hawana vifaa vya usafi, vyombo ambavyo vinatumiwa kwa ajili ya chakula vinawekwa katika mazingira machafu, sehemu zao za kupikia pia hazijasafishwa.

Wakati hali ikiwa hivyo, Uongozi wa Halmashauri naona wapo kimya kama hawaoni vile kinachoendelea, mpaka magonjwa ya mlipuko yatokee ndiyo wataanza kuhaha kusimamia usafi wa Migahawa hiyo.

Tukumbuke hivi karibuni wenzao wa Mbeya wamekuwa na wakati mgumu kama ilivyo kwa Simiyu kutokana na Kipindipindu, wanasema mwenzako akinyolewa...

Mwanongwa nawakumbusha tu kinga ni Bora kuliko tiba.
Mbona Hapo kusafi tembea tembea uone ..
 
Back
Top Bottom