Baadhi ya Motivational Speakers ni matapeli

Baadhi ya Motivational Speakers ni matapeli

kante mp2025

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2022
Posts
631
Reaction score
1,192
Mwanzo nilikuwa muumini mkubwa wa hawa wa kuitwa motivational speakers ilikuwa haipiti siku sijasikiliza mausia yao kuhusu maisha hasa hasa mbinu za kupata utajiri na kufikia malengo maishani.

Sikuishia kuwasikiliza tu nilienda mbali zaidi na kuyaishi maneno yao maana hawa jamaa wana principle za kila kitu, wapo wakukushauri kuhusu ndoa, kufaulu darasani,kupata mchumba, kuepuka madeni n.k

Hitimisho nimegundua hawa jamaa ni wagonga ulimbo tu nao wanajitengenezea kipato kama wagonga ulimbo wengine kupitia nakala zao na video zao pale mjini youtube.

Nimefanya utafiti nikagundua kwenye kufanikiwa kila mtu ana mbinu zake hakuna formula moja kama hawa motivesheni spika wanavodanganya umma


Ukienda huko mjini tiktok madogo wa 2000 wana washauri wao kuhusu maisha na huwaambii kitu kuna mmoja wanamuita chief god love ndio mshauri wao kuhusu mafanikio😂

Mafanikio ni fumbo wagonga ulimbo tuzidi kupambana kwa njia zetu hawa mamotivesheni spika ni matapeli kama wa tuma kwa namba hii
 
Labda ni kweli!! Ila Kwani kazi ya motivational speakers ni ipi? Nadhani iko centred kutumotivate ionekane inawezekana!! Ni kama kuhubiriwa kanisani juu ya imani ya kuhamisha milima..kwaivo binafsi sioni tatizo lao, if you get motivated, do the rest! Matokeo yakiwa hasi move on, na yakiwa positive give five!
 
Wavaa suti ni matapeli wanataka pesa rahisi, hakuna tajiri ana maneno mengi hao jamaa zako wanakariri mambo kweny vitabu.
 
mafanikio moja kwa moja huwa yanalenga kupambana na tabia zako!,sasa kila mtu na tabia zake huwezi kutuambia sote tutumie njia fulani kumbe mwengine pesa anapata lkn natabia yakufuja kupitia starehe!, mwengine mvivu kazi hataki kufanya ama hafanyi kwa ufanisi hatuwezi kuwa sawa kila mmoja ajue nafasi yake na apambane na matabia yake... mambo ni mengi na yanachosha lkn ndio mafanikio yenyewe!.

mwengine anakuambia tunza pesa unatunza halafu hujui utakuja kuifanyia nini na hata kama unajua utaifanyia biashara gani,hiyo biashara huijui vyema babu mambo ni vurugu...🤣
 
mafanikio moja kwa moja huwa yanalenga kupambana na tabia zako!,sasa kila mtu na tabia zake huwezi kutuambia sote tutumie njia fulani kumbe mwengine pesa anapata lkn natabia yakufuja kupitia starehe!, mwengine mvivu kazi hataki kufanya ama hafanyi kwa ufanisi hatuwezi kuwa sawa kila mmoja ajue nafasi yake na apambane na matabia yake... mambo ni mengi na yanachosha lkn ndio mafanikio yenyewe!.

mwengine anakuambia tunza pesa unatunza halafu hujui utakuja kuifanyia nini na hata kama unajua utaifanyia biashara gani,hiyo biashara huijui vyema babu mambo ni vurugu...🤣
😁😂😂Kila mtu anaibuka na jambo lake kama makanisa mapya
 
Mwanzo nilikuwa muumini mkubwa wa hawa wa kuitwa motivational speakers ilikuwa haipiti siku sijasikiliza mausia yao kuhusu maisha hasa hasa mbinu za kupata utajiri na kufikia malengo maishani.

Sikuishia kuwasikiliza tu nilienda mbali zaidi na kuyaishi maneno yao maana hawa jamaa wana principle za kila kitu, wapo wakukushauri kuhusu ndoa, kufaulu darasani,kupata mchumba, kuepuka madeni n.k

Hitimisho nimegundua hawa jamaa ni wagonga ulimbo tu nao wanajitengenezea kipato kama wagonga ulimbo wengine kupitia nakala zao na video zao pale mjini youtube.

Nimefanya utafiti nikagundua kwenye kufanikiwa kila mtu ana mbinu zake hakuna formula moja kama hawa motivesheni spika wanavodanganya umma


Ukienda huko mjini tiktok madogo wa 2000 wana washauri wao kuhusu maisha na huwaambii kitu kuna mmoja wanamuita chief god love ndio mshauri wao kuhusu mafanikio😂

Mafanikio ni fumbo wagonga ulimbo tuzidi kupambana kwa njia zetu hawa mamotivesheni spika ni matapeli kama wa tuma kwa namba hii
Keshatapeliwa mtu hapa. Kazi zao ni zipi hao Motivational Speakers? Binafsi sijawahi kusikiloza waongeacho wala kuwafuatilia na mambo yangu yako byeee tu.
 
Acha kila mtu ajitafutie RIZIKI yake kwa nafasi yake, muhimu tu asivunje sheria ya nchi. Ila wewe ukiingia kwenye 18 zake SHAURI YAKO.
 
Back
Top Bottom